Haya ndiyo aliyonieleza mfanyakazi wa mwenye nyumba siku niliyokuwa nahama

Bigbootylover

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
2,847
1,828
Yeye:Aiseee, vipi mbona unahama? Umekaa kidogo tu

Mimi:Aah nimepata chumba kingine tu huko mjini

Yeye:Aah sio mbaya, japo umejitahidi, wengi huwa hawadumu hapa, huwa wanakaa kidogo tu na mambo yao lazima yaende vibaya, na hatimae huondoka.

Mimi: (Nikashtuka kidogo sababu kilichonifanya nihame ni kweli, ni kutokana na hali mbaya iliyonikabili, niliona nisingeweza tena kulipa kodi ya chumba na sebule, self contained kwa hali yangu ilivyogeuka haraka, toka juu kwenda chini kwa haraka sana, hela inaisha kimazingara sana) Nikamuuliza, kweli? Kwa nini?

Yeye: Huyu boss wangu ni mtu "mbaya"(Ushirikina), inaelekea anamchezo mbaya huwa anafanya, hata baadhi ya wafanyabiashara wenzake wanamlalamikia, wateja wake pia(Maana, anaduka pekee mtaa mzima, wengine wameshindwa kuanzisha na watakaoanzisha duka lazima waibiwe).

Mimi:Nikamkumbuka kaka yangu ambaye alikuja tukae nae, yeye pia alikuwa analalamika mambo yake yameanza kuwa mabaya toka aje hapo kwangu, nikajumlisha na hali yangu then nikaunganisha dots, kiukweli niliwaza sana. Japo mimi siamini katika haya mambo lkn kiukweli nimeona hapa kuna chembe flan ya ukweli, najua ni muda ambao biashara haziendi sawa, lakini Mwenyenyumba wangu mambo yako vizuri tu.

Kilichokuja kunishtua zaidi huyu mfanyakazi katika maongezi yetu tuliligusia swala la yeye kulala, anafanya kazi kama mlinzi lakini hata ukifika mchana hana pa kupumzika, inamaana ye ni mlinzi forever, hajapewa chumba, nilipojaribu kumuuliza kuna uhaba wa vyumba?

Hapana kuna vyumba vingi lakini kuna viwili ni kwa ajili ya watoto wakija
likizo, kuna vingine VIMEFUNGWA KWA AJILI YA "VITU VYA DUKANI".

Aisee, Generally nimelifikiria sana hili suala, japo bado sijaelekea sana kwenye kuamini mambo ya kishirikina, lakini kama ni kweli basi sisi tusioyaamini haya mambo na IMANI ZETU HAZINA NGUVU SANA, AMBAO TUPO WENGI, TUNAONEWA SANA NA WATU WA AINA HII, pia tujitahidi kuulizia vizuri nyumba za kupanga, kisa cha waliopita kuhama.

TUMUOMBE SANA MUNGU AU KUVIOMBEA VYUMBA AU NYUMBA TUNAZOTAKA KUHAMIA. TUWE MAKINI NA MAJUMBA YA WATU TUNAYOPANGA AU TUNAYOTAKA KWENDA KUPANGA.

Hapa makazi mapya, japo sijapasoma vizuri ila naona wapangaji tupo wengi na watu wanamishe zao kama kawa. Kitu kingine pia kule nilipotoka, kipindi nahamia kuna jamaa chumba cha pili ndo alikuwa anahama sikupata hata muda wa kuongea nae, ile nyumba inavyumba viwili tu vya kupanga.

TUWE MAKINI
 
Yeye:Aiseee, vipi mbona unahama? Umekaa kidogo tu

Mimi:Aah nimepata chumba kingine tu huko mjini

Yeye:Aah sio mbaya, japo umejitahidi, wengi huwa hawadumu hapa, huwa wanakaa kidogo tu na mambo yao lazima yaende vibaya, na hatimae huondoka.

Mimi: (Nikashtuka kidogo sababu kilichonifanya nihame ni kweli, ni kutokana na hali mbaya iliyonikabili, niliona nisingeweza tena kulipa kodi ya chumba na sebule, self contained kwa hali yangu ilivyogeuka haraka, toka juu kwenda chini kwa haraka sana, hela inaisha kimazingara sana) Nikamuuliza, kweli? Kwa nini?

Yeye: Huyu boss wangu ni mtu "mbaya"(Ushirikina), inaelekea anamchezo mbaya huwa anafanya, hata baadhi ya wafanyabiashara wenzake wanamlalamikia, wateja wake pia(Maana, anaduka pekee mtaa mzima, wengine wameshindwa kuanzisha na watakaoanzisha duka lazima waibiwe).

Mimi:Nikamkumbuka kaka yangu ambaye alikuja tukae nae, yeye pia alikuwa analalamika mambo yake yameanza kuwa mabaya toka aje hapo kwangu, nikajumlisha na hali yangu then nikaunganisha dots, kiukweli niliwaza sana. Japo mimi siamini katika haya mambo lkn kiukweli nimeona hapa kuna chembe flan ya ukweli, najua ni muda ambao biashara haziendi sawa, lakini Mwenyenyumba wangu mambo yako vizuri tu. Kilichokuja kunishtua zaidi huyu mfanyakazi katika maongezi yetu tuliligusia swala la yeye kulala, anafanya kazi kama mlinzi lakini hata ukifika mchana hana pa kupumzika, inamaana ye ni mlinzi forever, hajapewa chumba, nilipojaribu kumuuliza kuna uhaba wa vyumba? Hapana kuna vyumba vingi lakini kuna viwili ni kwa ajili ya watoto wakija
likizo, kuna vingine VIMEFUNGWA KWA AJILI YA "VITU VYA DUKANI". Aisee, Generally nimelifikiria sana hili swala, japo bado sijaelekea sana kwenye kuamini mambo ya kishirikina, lakini kama ni kweli basi sisi tusioyaamini haya mambo na IMANI ZETU HAZINA NGUVU SANA, AMBAO TUPO WENGI, TUNAONEWA SANA NA WATU WA AINA HII, pia tujitahidi kuulizia vizuri nyumba za kupanga, kisa cha waliopita kuhama, TUMUOMBE SANA MUNGU AU KUVIOMBEA VYUMBA AU NYUMBA TUNAZOTAKA KUHAMIA. TUWE MAKINI NA MAJUMBA YA WATU TUNAYOPANGA AU TUNAYOTAKA KWENDA KUPANGA. Hapa makazi mapya, japo sijapasoma vizuri ila naona wapangaji tupo wengi na watu wanamishe zao kama kawa. Kitu kingine pia kule nilipotoka, kipindi nahamia kuna jamaa chumba cha pili ndo alikuwa anahama sikupata hata muda wa kuongea nae, ile nyumba inavyumba viwili tu vya kupanga. TUWE MAKINI
Pole mkuu bora machale yamekucheza la sivyo ulikuwa ugeuzwe msukule.....Katoe sadaka either kanisan/msikitini au popote pale kwa wahitaji maana ilikuwa imebakia nukta tu......
 
Pole mkuu katika nyumba nyingi za kupanga mambo haya yapo sana.
 
Ku....... Ndili mk............... But ndili kubortown nini kaka?
 
Hahaaa, mkuuu nyumba za kupanga ishu,kuna frem flani za duka ziko buguruni kwa mnyamani,frem nzuri kweli na ziko eneo zuri kweli, kodi bei cheee, ila hazina wapangaji,kila anayefungua biashara anakimbia, sister angu alipata hizo fremu, hakujua lolote akajua kapata booonge la frem na alitegemea angeuza kweli kweli, daaa, aliyokutana nayo hana hamu, mauzauza usipime, mpaka anaondoka hapo robo tatu ya mtaji wake ulishaisha
 
Nimekutana nayo maeneo ya mwananyamala katika nyumba ya kwanza niliyopanga. Nilitonywa Na majirani nikaacha kodi yangu kabla hata haijatimiza nusu
du...pole!siku nyingine niite nije niangushe maombi usiache hela kirahisi hivyo!
 
Nilinunua nyumba kwa mzee mmoja huku kusini na tulilipana haki bin haki hakuna aliekuwa anamdai mwenzake, kwa kweli mpaka kuja kulala kwenye hiyo nyumba nilifanya kazi ya ziada wakuu. Ushuhuda wa kweli kabisa
 
Pole mkuu bora machale yamekucheza la sivyo ulikuwa ugeuzwe msukule.....Katoe sadaka either kanisan/msikitini au popote pale kwa wahitaji maana ilikuwa imebakia nukta tu......
Mkuu hali mbaya tu imeniondoa, otherwise ningeendelea kukaa, pia huyu jamaa nilikuwa sijazoeana nae sana, ilikuwa salam tu natoka zangu, salam tu narudi ila kumbe angeniambia kitambo,
 
Umenikumbusha mbali sana mkuu,2009 K/ndoni Mkwajuni yalinikuta haya..ilikuwa lazima kila siku saa10 alfajiri nistuke usingizini na nilichokuwa nakiona ni kama watu wapo chumbani wanacheza mdumango,nilikomaa mpaka kodi yangu ilipoisha.ila nilichogundua wanaofanya sana haya mambo ni wale wenye nyumba wanaozitegemea nyumba zao kwakila kitu hawana shughuli nyingine yakufanya.
 
Back
Top Bottom