Haya Ndio Mataifa huru duniani

Cash Generating Unit

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2019
Posts
13,284
Reaction score
39,491
Dunia ina jumla ya Nchi 195 lakini ni Mataifa 5 tu ndiyo yako huru kisiasa, kiuchumi, kijeshi nknk. Tunavyozungumzia Mataifa huru ni yale ambayo hayaingiliwi kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni na siyo kibaraka wa taifa fulani.

Mataifa haya huwa yanafanya maamuzi magumu pindi usalama wa nchi unapokuwa hatarini. Yanajiweza kijeshi, technolojia, hayaingiliwi kisiasa na taifa lolote lile. Na pia hayaogopi taifa lolote lile linapokuja suala la usalama wa nchi.

Mataifa 5 tu yako huru ambayo ni:
1. Russia

2. USA

3. China

4. Iran

5. North Korea

Hayo ndiyo Mataifa huru Duniani it’s crazy lakini ndio hali halisi. Ni huzuni kuona Mataifa makubwa kama Ufaransa, Ujerumani, Japani na UK hayako huru.

Hata WW3 itatokea bhas hayo Mataifa juu yatakua chanzo.
 
6. Cuba
7. Venezuela
 
Ni uzuni kwakweli mpaka Tz yangu nayo haipo huru
 
mkuu, mataifa huru kwa tafsiri yako ni mawili tu hapa duniani, hao uliowaweka namba 1 &2......

Iran na Korea bila backup ya Russia wanapotezwa hata kesho!

China hata haeleweki, usimweke kwenye mzani mmoja na Russia + US, hajawahi pigana vita yoyote kubwa na akashinda, hata ule uchumi wake haujawahi pigwa gwaride... jeshi lake hata hatujui likoje
 
Wewe sijui shule umesomea wapi braza, Taifa huru duniani ni USA tu, yalobaki ni vibaraka tu hawana lolote, Russia yako hiyo haiwezi kusimama agenda pale UN hadi ikapita au kuungwa mkono sasa huo uhuru wako unaoizungumzia iko wapi.

China wanaminywa makende na USA hadi this time, hawawezi chochote mbele ya USA labda kwa majirani tu, angekuwa huru Huawei isingepotea kwenye ramani duniani braza, baba wa dunia ni USA

Russia kavimbiwa hadi Ukraine, Prighozin, etc sasa huo uhuru unazungumzia nini, najua lengo lako ni kutaka kuweka Russia na USA katika level 1 bt Russia bado braza
 

hata US maamuzi yake yanaweza yasipite kwa sababu ya VETO ya urusi. UN ni mbwa asiye na meno kwa hao wababe US na urusi. Ndio maana huamua kuvamia nchi bila ruhusa ya UN.
 
Hayo ndiyo Mataifa huru Duniani it’s crazy lakini ndio hali halisi. Ni huzuni kuona Mataifa makubwa kama Ufaransa, Ujerumani, Japani na UK hayako huru.

Israel inaingiliwa uhuru wake na nchi ipi? (Tafadhali usiitaje Marekani)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…