Haya maneno ya Waziri wa Fedha yamenifanya nitafakari sana na kujiuliza hivi hili Taifa letu lipo serious kweli kwa tathimini za kiuchumi Kama hizi?

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Oct 6, 2016
10,205
12,721
".... Kila kipato kinapoongezeka na matamanio nayo yanaongezeka, hiki ndicho kinachosababisha ugumu wa maisha.

..... Nilipita hapa mjini juzi, kila baada ya gari mbili unakutana na namba 'E' zinafululiza kama tano ndiyo zinakuja namba nyingine.Nenda kalinganishe na miaka miwili au mingine huko nyuma"

"Zipo hatua tumepiga.Nenda hata benki unakuta viti vimejaa na wengine wengi wamesimama.

... Nenda kwenye harusi kaangalia, huko nyuma hata michango tu ya harusi ilikuwa inatupiga chenga wakati huo.

"Hili jambo la ugumu wa maisha kuanzia tu unapozaliwa ni mpaka unapomaliza. Ndio maana wanasema mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi ni chache tena zilizojaa tabu.

Hamna siku hilo la ugumu litaisha ndio maana hata matajiri wakubwa duniani wanajirusha na kujiua."

Kubwa zaidi tunaloliangalia kama serikali ni uwekezaji mkubwa unaoelekezwa kwenye shughuli za uwekezaji kwasababu huo unaenda kupunguza pengo kati ya walionacho na wale wasionacho.

"...Uwekezaji unaolenga kwenye kukuza sekta binafsi na kwenye sekta inayoajiri watu wengi zaidi ndio unaotoa jawabu la kudumu kwenye maisha na ustawi wa watanzania.

- Mwigulu Nchemba
Waziri wa fedha Tanzania

Maswali yangu: je ni kweli uchumi wa nchi hupimwa kwa kutazama kumbi za harusi, namba E za magari barabarani?!

Kama ni hivi tuna safari ndefu sana katika taifa let hili (Tanzania).
 
Inasikitisha sana kuwa na viongozi kama hawa. Hajui hata azungumzie vipi ugumu wa maisha ya wananchi wake, halafu eti ndiyo waziri wa fedha na uchumi wa nchi.
 
Leo nimekula mlo mmoja,sijanywa juice tangu mwaka juzi,,,sio kwakumfuata dk janabi bali sina uwezo,usiwasikilize waliovimbiwa kwa kodi zetu mwigulu ni mwekezaji mkubwa anatunishiana misuli na GSM na MO
 
Inasikitisha sana kuwa na viongozi kama hawa. Hajui hata azungumzie vipi ugumu wa maisha ya wananchi wake, halafu eti ndiyo waziri wa fedha na uchumi wa nchi.
Na ni PhD pia wa uchumi eti!! Mimi ndiyo maana siku zote huwa namoima mtu kwa akili yake ya kichwani, na siyo idadi ya madesa aliyosoma na kukariri chuoni.
 
Kuna factor nyingi Sana za kuangalia kama kuna "booming economy" au kuna decline ya kiuchumi...
Alizotaja Mwigulu zote ni viasharia vya "booming economy "..

Zipo nyingi hata idadi ya harusi ...
Idadi ya new business registration huko brela n.k...

Booming economy haimaanishi maisha ni "Safi Kwa kila mtu"au Kwa Wengi.......

Hata wakati wa Kikwete watu waliimba "laki si pesa"...huku Wengi wanalalamika maisha magumu..
Alipoondoka Kikwete Tu ndo ikaanza "vyuma vimekaza"...
 
Back
Top Bottom