Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,708
Wazazi wa vijana hawa wawili wanaishi pamoja kama mume na mke,na wameishi hivyo kwa miaka mitano,lakini wote wawili wana umri mkubwa,baba 52 mama 50,wakati wanakutana wote walikuwa na watoto hawa kabla,watoto hawa walifahamiana na kuanzisha mahusiano baada ya wazazi wao kuwa pamoja binti ana miaka 25 na kijana ana 29,binti ndo alianzisha uhusiano kwa kumwambia kijana hisia zake,kijana akawa mgumu kutokana wazazi wake,lakini baada ya muda kupita akawa amekubaliana na binti,sasa wanajiuliza kama wanaweza kufunga ndoa kwani uhusiano wa gf na bf sio sawa na ndoa,ndoa ni kubwa zaidi,kabla hawajalipeleka jambo hili kwa wazazi wanaomba ushauri,alielileta kwangu ni kijana ambae ni rafiki yangu na pia ni alikuwa mfanyakazi mwenzangu!Nitashukuru kwa maoni na mitazamo yote!Je wanaweza kuoana wakati wazazi wao ni wanandoa?Kumbuka hawa hawajashare mzazi hata mmoja,mama wa binti na baba wa kijana waliwapata hawa watoto wao kabla hawajawa pamoja!