Baada ya kusumbuliwa na panya kwa muda nikaamua kutafuta paka, kweli since then panya kwangu hakunaa. Huyo paka akazaa dume..sasa tokea hapo huyo dume ndio amekuwa mume wa paka mama na cha ajabu kabisa wameanzisha tabia ya kupigana miti mbele zetu hata mbele ya wageni yaani wenyewe ni popote pale. Inakera sana. Yaani wanaanza romance mpaka kuchapana dushelele mbele ya familia.
Milio ile ya nuksi nuksi kama watoto wanalia wenyewe wanaipiga tena mchana kweupe bila woga
Je, hii ni nuksi au kawaida au ndio utandawazi.
Na juzi juzi hapa kazaa vipaka vibubu havilii vyenyewe ni kutoa macho tu ndani ya miezi miwili sijawahi kuvisikia vinalia hata tone. Nimesha dash out. Wamebakia hawa vicheche-nyegere paka.
Nawagawa wallah watake wasitake!!