CalvinKimaro
JF-Expert Member
- Sep 11, 2017
- 245
- 314
Jumanne wiki ijayo Benki ya Dunia inakusudia kuidhinisha mkopo wa dola za kimarekani milioni 500 kwa serikali ya Tanzania. Mkopo huu nia yake ni kuboresha elimu kwa wasichana ili waweze kupata elimu ya sekondari.
Kumejitokeza kikundi cha wanaojiita CONCERNED CITIZENS OF TANZANIA CIVIL SOCIETY wameandika barua kuomba Benki ya Dunia isitoe mkopo huo kwa serikali ya Tanzania mpaka eti iruhusu wanaobeba mimba mashuleni waendelee kukaa madarasani.
Pia sababu nyingine ni kupinga kauli ya Raisi kuwa watu waachane na mpango wa uzazi. Sababu nyingine ni tamko la serikali kupinga ushoga eti ni kuingilia uhuru na haki za mashoga!
Wanadai kuzaa bila uzazi wa mpango ni mbaya kwa wanawake! Eti kuipa Serikali ya Tanzania mkopo huu itakuwa benki ya Dunia imeshiriki kuwadhalilisha wanawake! Wanadai kauli ya Rais imesababisha wanawake kushambuliwa nchini Tanzania. Walioandika barua hii wameomba majina yao yasitajwe!
Benki ya Dunia imesema haiwezi kuamua ombi hili inasubiri kikao cha Bodi jumanne.
Ikumbukwe kuwa mwezi September 2019 watu hawa hawa walipinga mkopo wa dola 450 milioni lakini Benki iliutoa ili kusaidia juhudi za serikali kupambana na umasikini (poverty reduction) na iliwaeleza hawa kuwa serikali inashughulikia malalamiko yao.
Kikundi hiki kinadai toka serikali ipewe dola 450 milioni haijarekebisha malalamiko yao. Katika lalamiko la huo mkopo wa September Zitto Kabwe aliandika barua binafsi kuelezea kutoridhishwa kwake.
Sehemu moja ya barua yake ambayo aliituma kwa siri na kuomba isionyeshwe anasema hivi “Regrettably, it appears the bank’s approval of the . . . project in September only emboldened this government,” (mwisho wa kunukuu). Barua hii aliituma kwa siri Kwa gazeti la FT (gundua mwenyewe).
Katika barua hiyo Zitto Kabwe ameibua suala la Kabendera kuwa kushikiliwa kwake ni ishara kuwa serikali haijajirekebisha hivyo haistahili kupewa mkopo wa milioni 500 jumanne ijayo. Zitto pia ameibua suala la uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kudai kuwa serikali ndiyo iliwaengua wao hawakususa! Anadai serikali ya CCM ni ya watu wachache na imepoteza uhalali wa kutawala Kwa hiyo haistahili kukopeshwa.
Kwa hiyo huhitaji kukuna akili kujua hiki kikundi kinachojiita CONCERNED CITIZENS OF TANZANIA CIVIL SOCIETY ni kina nani.
Napendekeza serikali imuite Zitto imhoji. Haiwezekani mtu mmoja au kikundi cha watu wachache wafanye jitihada kukwamisha maendeleo ya wengi. Hivi sio kosa mtu kuandika barua kama iliyoandikwa na hiki kikundi na ile ya Zitto? Hii haiangukii kosa la uhujumu uchumi?
Wahusika walijidanganya kuwa barua zao zitakuwa siri. Wanachosahau ni kuwa uliandika barua ukaituma duniani usiri unatoweka! Wapo wenye nia njema na Tanzania! Hakuna Siri! Sasa barua zao sio siri tena.
Serikali iziite hizo asasi zikizojiorodhesha na iziadhibu ipasavyo ili vitendo hivi vya kihaini vikome.
Ninaamini kabisa Jumanne ijayo Bodi ya Benki ya Dunia itaidhinisha mkopo WA dola milioni 500 ili wasichana wawezeshwe kupata elimu ya sekondari.
Ni vyema pia wapiga kura wakaelezwa jinsi ambavyo wanaotaka kura zao wanavyohujumu maslahi yao nje ya nchi. Hivi anayeumia ukipinga mkopo wa kusomesha wasichana au mkopo wa kupunguza umasikini ni Magufuli? Ni CCM? Sio wasichana na masikini nchini Tanzania?
Hawana huruma na wananchi. Hivi mashoga wanathamani kwao kuliko wasichana na masikini? Hivi Kabendera ana thamani kuliko mamilioni ya watoto wa kike wa watanzania?
Hawafai kuwapa kura!
ONYO: ukinakili ukajifanya ni makala yako na huna hizo barua ukikabwa usinifuate.
Kumejitokeza kikundi cha wanaojiita CONCERNED CITIZENS OF TANZANIA CIVIL SOCIETY wameandika barua kuomba Benki ya Dunia isitoe mkopo huo kwa serikali ya Tanzania mpaka eti iruhusu wanaobeba mimba mashuleni waendelee kukaa madarasani.
Pia sababu nyingine ni kupinga kauli ya Raisi kuwa watu waachane na mpango wa uzazi. Sababu nyingine ni tamko la serikali kupinga ushoga eti ni kuingilia uhuru na haki za mashoga!
Wanadai kuzaa bila uzazi wa mpango ni mbaya kwa wanawake! Eti kuipa Serikali ya Tanzania mkopo huu itakuwa benki ya Dunia imeshiriki kuwadhalilisha wanawake! Wanadai kauli ya Rais imesababisha wanawake kushambuliwa nchini Tanzania. Walioandika barua hii wameomba majina yao yasitajwe!
Benki ya Dunia imesema haiwezi kuamua ombi hili inasubiri kikao cha Bodi jumanne.
Ikumbukwe kuwa mwezi September 2019 watu hawa hawa walipinga mkopo wa dola 450 milioni lakini Benki iliutoa ili kusaidia juhudi za serikali kupambana na umasikini (poverty reduction) na iliwaeleza hawa kuwa serikali inashughulikia malalamiko yao.
Kikundi hiki kinadai toka serikali ipewe dola 450 milioni haijarekebisha malalamiko yao. Katika lalamiko la huo mkopo wa September Zitto Kabwe aliandika barua binafsi kuelezea kutoridhishwa kwake.
Sehemu moja ya barua yake ambayo aliituma kwa siri na kuomba isionyeshwe anasema hivi “Regrettably, it appears the bank’s approval of the . . . project in September only emboldened this government,” (mwisho wa kunukuu). Barua hii aliituma kwa siri Kwa gazeti la FT (gundua mwenyewe).
Katika barua hiyo Zitto Kabwe ameibua suala la Kabendera kuwa kushikiliwa kwake ni ishara kuwa serikali haijajirekebisha hivyo haistahili kupewa mkopo wa milioni 500 jumanne ijayo. Zitto pia ameibua suala la uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kudai kuwa serikali ndiyo iliwaengua wao hawakususa! Anadai serikali ya CCM ni ya watu wachache na imepoteza uhalali wa kutawala Kwa hiyo haistahili kukopeshwa.
Kwa hiyo huhitaji kukuna akili kujua hiki kikundi kinachojiita CONCERNED CITIZENS OF TANZANIA CIVIL SOCIETY ni kina nani.
Napendekeza serikali imuite Zitto imhoji. Haiwezekani mtu mmoja au kikundi cha watu wachache wafanye jitihada kukwamisha maendeleo ya wengi. Hivi sio kosa mtu kuandika barua kama iliyoandikwa na hiki kikundi na ile ya Zitto? Hii haiangukii kosa la uhujumu uchumi?
Wahusika walijidanganya kuwa barua zao zitakuwa siri. Wanachosahau ni kuwa uliandika barua ukaituma duniani usiri unatoweka! Wapo wenye nia njema na Tanzania! Hakuna Siri! Sasa barua zao sio siri tena.
Serikali iziite hizo asasi zikizojiorodhesha na iziadhibu ipasavyo ili vitendo hivi vya kihaini vikome.
Ninaamini kabisa Jumanne ijayo Bodi ya Benki ya Dunia itaidhinisha mkopo WA dola milioni 500 ili wasichana wawezeshwe kupata elimu ya sekondari.
Ni vyema pia wapiga kura wakaelezwa jinsi ambavyo wanaotaka kura zao wanavyohujumu maslahi yao nje ya nchi. Hivi anayeumia ukipinga mkopo wa kusomesha wasichana au mkopo wa kupunguza umasikini ni Magufuli? Ni CCM? Sio wasichana na masikini nchini Tanzania?
Hawana huruma na wananchi. Hivi mashoga wanathamani kwao kuliko wasichana na masikini? Hivi Kabendera ana thamani kuliko mamilioni ya watoto wa kike wa watanzania?
Hawafai kuwapa kura!
ONYO: ukinakili ukajifanya ni makala yako na huna hizo barua ukikabwa usinifuate.