MakinikiA
JF-Expert Member
- Jun 7, 2017
- 5,695
- 7,872
Waisraeli kutoka nyanja zote za kisiasa wameonyesha hasira siku ya Jumatatu kutokana na habari za makubaliano ya kusitisha vita kati ya Marekani na Iran, wakiita hatua hiyo kuwa janga kwa Israeli na kuelekeza hasira zao kwa Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu.
Kiongozi huyo wa Israel alisema katika mkutano na waandishi wa habari Jumatatu kwamba "kwa makubaliano au bila makubaliano," antaendelea kupigana ili kuizuia Iran kupata silaha za nyuklia, jambo ambalo Tehran imesisitiza kwa muda mrefu kwamba haijaribu kufanya hivyo, ikisema mpango wake wa nyuklia ni kwa madhumuni ya raia.
"Mradi mimi ni Waziri Mkuu wa Israeli, haitatokea," Netanyahu alisema, akisisitiza kwamba makubaliano hayo yalifikiwa na Marekani, wala sio Israeli, na kwamba hakukubali ombi la Iran la kujiondoa kwa Israeli kutoka Lebanon kuwe sehemu ya makubaliano hayo.
"Iran ilitaka tuondoke huko, lakini hilo halikutokea. Unajua ni kwa nini halikutokea, miongoni mwa sababu zingine? Kwa sababu nilisimama kidete," alisema.
Lakini maafisa wengine wa serikali ya Israeli, wapinzani, wanasiasa na wachambuzi walikuwa wepesi kukosoa makubaliano ya awali, wakiashiria aina ya kura ya maoni isiyo rasmi kuhusu muda wa waziri mkuu huyo kabla ya uchaguzi.