Kubwajinga
JF-Expert Member
- Jan 23, 2008
- 2,193
- 299
lowasa aliliingizia taifa hasara ya shilingi ngapi kutokana na kashfa za ufisadi alizonazo?
Hiv escrow yumo,epa je,meremeta je, kama yupo niambie nihame ukawa
Magufuli akaongoze ng'ombe
kinana yuko wapi jamani simsikii kabisaa?? nataka nimuulize kmapeni zimeishA au?? mbona kimya saana
Wee Nyengo, mie sikuwezi kabisa. Naona umemkosesha usingizi 'kubwajinga'. Wala haina haja ya kusubiri, kwani dawa na dozi uliyotoa imemuingia na kupenyeza kisawasawa. Hebu angalia jinsi anavyohangaika kureply kila baada ya dakika mbili. Umefanikiwa sana nyengo, pongezi. Hivi ndivyo inavyotakiwa, ... dunga, kisha subiri uone wanavyotabika kujitetea. Hawa hawawezi kukatiza. Siwalaumu, kwani ni kawaida kiumbe kipige mateke saa ya kuaga ifikapo. Poleni magamba masisyemu.
Hakufai wewe na nani? wanaokufaa ni wale walioiba pesa za escrow?waliouza pesa za mabehewa feki, wanakufaa wale walioiba pesa za kivuko feki cha Bagamoyo?
malizia kujibu kitu ulicho quote hadi mwisho nasubiri ujibu niendelee hujaongelea huo ufisadi mwingine lowasa alihusika au ufisadi ni richmond pekee nyingine zote zilikua takrima au hazikuliingizia taifa hasara
Lowasa fisadi sawa ila tutamchagua tu kama sentensi hii mpe mchawi akulelee mwanao ila CCM imetuumiza sana huu muda wa mabadiliko.
yani mkuu hii nguvu unayotumia kumponda lowasa ungetumia kumnadi magufuli na kueleza ilani yake angalau ungeonekana umekua ila tatizo nyie mnadhani wananchi wanataka kujua ufisadi wa lowasa hata mkimchafua vp hamshawishi watu kupigia kura ccm cha msingi ungeelezea utekelezaji wa ilani ya ccm tena kwa msisitizo wa kubold hivihivi labda utasikilizwa ila ukija kwa gia hii ya kumchafua lowasa imeshafeli mara nyingi
Sera mbovu za CCM ndo zimeua hiki chama.
adui mwingine huyu hapa!
#Unalipwa 600,000 Ukatwe kodi ya PAYE 18% ya
mshahara
600,000-108000= 492000
Ukatwe 18% mkopo wa boom
ulioupata chuo
492000-108,000=384,000
Kodi ya nyumba
384,000-100,000=284,000
NSSF wakate hapo
284,000-80,000=204,000
Bili ya umeme
204,000-20,000= 184,000
Dala dala kwenda kazini kurudi
home
800*30=24,000
184,000-24,000=160,000
Bili ya maji =10,000
160,000-10,000=150,000
Chakula mchana uwapo kazini
2000*30=60,000.
150,000-60,000= 90,000
Chakula cha usiku
2000*30=60,000
90,000-60,000=30,000
Chai 1000*30= 30,000
30,000-30,000=0
Hapo vocha ya 500*30=15,000
0-15,000= -15,000
Ulijisahau ukanywa soda
kwenye pita pita zako 600 -15,000-600=-15,600
Usivae
Ukivaa unakuza deni lako
Na hapo ni hesabu za mshahara
wa kima cha chini
kikiwa 600,000 Huna mke wala mtoto wala
tegemezi ya aina
yoyote
Kwa sasa mshahara kima cha
chini hakija fika
315,000 hali ikoje kwa watumishi wa serikalini kada
ya chini.
#Elimu bure itampunguzia masikini mzigo mkubwa #Bima za afya zitawapunguzia maskini mzigo
mkubwa
#kupunguza kodi na iwe katika level ya kimataifa
itampunguzia mfanya kazi
mzigo. #tafakari chukua hatua Usifanye makosa uchaguzi huu
leta mabadiliko
tumia kura yako.
.......halafu unakuta mjinga anashabikia ccm ....inakuwa ni akili zilizopigwa strock.....katika maisha uthubutu ni kitu cha mhimu sana!! mwaka huu tumedhamiria kuthubutu kubadili mfumo!!!!
Jamaa yangu usidanganyike mabadiliko kupitia CCM ni ndoto ya mchana kweupe.. mi mwenyewe mwana CCM lakini kura yangu ni kwa Lowasa... ikiwa CCM ilifutilia mbali maoni ya wananchi ktk katiba ni dhahiri kwamba CCM haitakuwa/haipo tayari kufanya mabadiliko yatakayoiumiza.
Maana ili ufanye mabadiliko ni lazima CCM iumie kwani CCM inauroho wa madaraka sana...na vigogo na watoto wao wachache wa CCM ndio wanaomiliki uchumi wa nchi na raslimali.
Usishangae jamaa yangu ni kwamba watanzania wameamua kwa dhati na kwa ujumla wao kuiadhibu CCM kutokana na mfumo wake wa kulindana na kuongeza maadui 2 zaidi Ufisadi na rushwa na kimsingi ukitazama kwa makini Lowassa kaachia ngazi za kiserikali toka 2007 miaka 8 takribani lakini ufisadi umeongezeka maradufu kumbe tatizo sio Lowassa ni mfumo CCM.
Kumbe adhabu ya mafisadi nchi hii ni kuwanyima fursa ya kugombea urais na mambo yanaishia hapo..?! cc: Kubwajinga
Anayetufaa;
MAGUFULI = MSAFI + MTENDAJI
Adui na bundi wa chama cha CCM wapo ndani ya CCM na sio nje ya CCM.
Hapa ni baadhi ya hao maadui nitajaribu kuwataja
1.Mkapa kajilimbikizia mali yeye,familia yake na marafiki zake na na akijua kuwa ni kinyume cha maadili ya CCM. Dharau, majigambo na matusi yalikuwa yakiwafanya baadhi ya wana CCM kujisikia kuwa hawana haki ya chama kilichokuwa kikiitwa chama cha wanyonge. Kibuli chake cha kutosikiliza wana CCM na Watanzania kiliwafanya wengi kukichukia chama cha CCM
2.Hapa Kikwete hawezi akakosekana..Kikwete kaiongoza nchi hii kiushikaji bila kujali hata maslahi ya wana CCM wenyewe..CCM alioianzisha Nyerere ilikuwa ni kwa maslahi ya wana CCM na Watanzania kiujumla Kuna wazee wa CCM wamelitumikia taifa hili kwa juhudi zote lakini hawakufikiriwa kuongezewa maslahi yao na badala yake vijana au watoto wadogo ambao kwa mda mchache wamekuwa na utajiri wa kukithiri..Je kuna mtu ambae atawasahau wale wazee waliofanya kazi ktk Jumuia ya Afrika Mashariki???Wazee wengine wako mbele ya haki na hawajapata chochote Masikini walimu na madaktari!!!
Kikwete kapuuzia maoni ya rasimu ya Katiba ilioandaliwa na Warioba..Hapa baadhi ya ana CCM wenye kuipenda nchi hii wakaanza kujitoa kwa kuona kuwa katiba iliyotungwa na Vijisenti na Sitta ilikuwa ni kwa ajili ya "wateule wachache"
Ufisadi mkubwa ambao ulikuwa wazi(RICHMOND,EPA,MEREMETA .ESCROW
NK)kaufumbia macho bila kuchukua hatua zozote
4. Makinda naye kaliendesha Bunge la Tanzania kama yuko ndani ya kikao cha chama cha CCM.Hakusikiliza hoja muhimu la taifa hili.Aliruhusu matusi na kejeli kutumika na akiwaachia wana CCM kuvunja kila aina ya kanuni pale mjengoni na huku akijua anakwenda kinyume na maslai ya taifa..wananchi wengi na hata wana CCM wengine hawakuridhishwa na utaratibu huo ambao mambo mengine yalikuwa ni maslahi mapana ya Taifa na sio ya chama cha CCM Mswaada kama wa Mafuta na gesi umewaumiza wananchi wengi na hata wana CCM wenyewe
5.Sitta kawa ni adui mmoja mkubwa sana..Huyu hataweza kusahaulika kwa Watanzania wengi na hata kwa wana CCM..Huyu alisahau kuwa waliotoa maoni katika rasimu ya Warioba walikuwa pia wana CCM..mpaka sasa hivi yeye na baadhi ya wana CCM wanadhani rasimu alioiandaa Warioba ni ya maoni ya wana UKAWA peke yake na kwamba wana CCM hawakushirikishwa..Baadhi ya wana CCM na wapenda nchi hii ikabidi waichukie CCM na uongozi wake wakijua kuwa Rasimu ya Chenge ni kwa ajili ya "wateule" peke yao..
Sitta ndio alioisababisha kuzaliwa kwa UKAWA..Kwa hiyo kufa kwa CCM kumerahisishiwa sana na Sitta. Watanzania na wana CCM wengi hawataweza kumsahau Sitta kwa kuiua CCM mapema
3.Nape amekuwa akitoa matusi na kejeli sio kwa wapinzani peke yake bali hata kwa wana CCM Hayuko mtu atakaesahau alivyosema CHADEMA ni chama cha Wachaga na huku akisahu kuwa ndani ya CCM kuna Wachaga Mke wa Mkapa ni Mchaga..ndio kusema Wachaga walio ndani ya CCM inabidi watoke na waende kwa "wachaga" wenzio huko CHADEMA na mbaya zaidi hivi kalibuni alivyomtukana mzee Warioba kuwa ni "ni mzee na anasubiri " sasa kwa kauri kama hizi ziliwafukuzisha baadhi ya makundi yaliyotengwa
4. Lugha,kejeli,majigambo, matusi nk ya viongozi wa CCM imewafukuzisha watu wenye busara zao kuona kuwa CCM sio ile ya Nyerere..Lugha kama "ninaapa kuwa Raisi hawezi kutoka kaskazini" imeua mori ya wana ccm na hata wale ambao wangeshawishika kujiunga au kukirudia hicho Chamahayuko mtu atakaesahau kauli kama
"hata nyasi mtakula lakini ndege ya Raisi itanunuliwa","kila mtu atabeba msalaba wake mwenyewe", "Vijisenti", "hela ya mboga",Kama huna nauli piga mbizi"," Buziku wanye barabarani wasambaze kinyesi iwe rami"
Hao ni baadhi ya maadui wa CCM mengine malizia naenda kulala[/QUOTE
Mleta maada hujitambui.
anakufaa wewe!
UNAKARIBISHWA KABLA Ya 25/10 KUMPIGA VITA FISADI PAPA = LOWASSA