Dar ilitakiwa iwe somo kwa wenye mamlaka lakini utaona bado hakuna tulipojifunza na kuendelea kurudia makosa yaleyale..
90% ya wakazi wa dar tunaishi kwenye vibanda umiza, kifupi Dar hata uwe na nyumba nzuri vipi bado unaishi kwenye skwata area tu, huna pakutupa taka, huna barabara nzuri za kupita, kiwanja unachoishi ni 20mx20m, Ona Sinza, Msasani, Mikocheni, Kijitonyama kulivyobanana na watu wanavyosifia na kurank hayo maeneo lakini uhalisia maeneo hayo ni hatari kwa Afya kwasababu ya mbanano uliofunga mpaka njia za maji na mzunguko wa hewa..hapo bado eneo kubwa la Manzese, Tandale, Magomeni, Ubungo, Buguruni, Tandika, Vingunguti, Kiwalani, Mtoni, Tandika, Mbagala, Kariakoo, Kigogo nk.. Hivyo utaona sehemu kubwa ya jiji lilivyo chafu na ukiwa angani ndio utaelewa haya.. Makosa yaleyale yanarudiwa kwenye maeneo mapya kama, Mbezi, Goba, Bunju, Kijichi, Chamazi, Kibaha, kibamba, Kiluvya, Tegeta, Bunju, Boko nk..
Watanzania tujifunze sasa, kujenga kuachiwe makampuni yajenge apartments zilizopangiliwa kwa ramani za miji, watu wauziwe apartments kwa bei rafiki iwe cash au mikopo, Serikali isimamie hili kwa kutoa unafuu mkubwa wa kodi kwenye vifaa vya ujenzi na viwanda vyote vinavyozarisha humu ndani vipewe punguzo kubwa ili bei ya bidhaa za ujenzi iwe nafuu na watanzania wakae kwenye nyumba bora, Biashara ya kupangisha nyumba waachiwe estates agency na si kila mtu ili pia nyumba hizo ziwe bora na nafuu..