manning
JF-Expert Member
- Apr 1, 2013
- 5,092
- 11,947
Wakuu wana jf
Sisi wakazi wa Vijiji vya Nzali , Mlimwa , Membe,Dabaro na vijiji vingine vya eneo hili hakika hatuna mbunge. Nadiriki kusema hivyo kwa sababu kwa miaka kibaao tangu dunia iumbwe tunakuwa kisiwani msimu wote wa mvua zinaponyesha na hata kunapokuwa hakuna mvua miezi kama hii kutokana na kukosa daraja la kupitisha maji kwa chini badala yake kuna ( flat screen tunavyoliita wenyeji)katika bonde la mto Nyasungu ambalo liko mpakani mwa vijiji vya Nzali na Mahama kata ya Chilonwa. Jambo hili limekuwa kero na kilio cha wananchi wa maeneo niliyotaja kwa mda mrefu tangu mbunge wetu akiwa Naibu Waziri wa ujenzi mpaka leo bado suluhu haijapatikana. Aidha Mbunge wetu hatukusikia anazungumza lolote kuhusu adha hii wakati bajeti ya Magufuri ilipowasilishwa. Kwa adha tunayopata sisi wananchi wa maeneo haya tunadiriki kusema hatuma Mbunge kwani hatusaidii kwa lolote wakati alipo Bungeni Dodoma mpaka sehemu husika ni kilomita 45. Wakati wa mvua kali mbunge huyo aliitwa na akaja kujionea hali halisi. Watu kwa hasira walimlazimisha avuke kwenda Nzali lakini aligoma Kabisa kwa khofia maisha yake , kwa hali hii tunadiliki kusema hatuna mbunge na tunaomba wenye kutaka ubunge wenye uchungu na wananchi wajitokeze kwa wingi mwaka 2015 nasi tutawapa kura bila kujari chama wa upinzani atapewa uzito mkubwa. manake huyu ameongoza kwa zaidi ya miaka 20 amejisahau kabisa
NAWASILISHA WANA JF NJOONI MTUSAIDIE
Sisi wakazi wa Vijiji vya Nzali , Mlimwa , Membe,Dabaro na vijiji vingine vya eneo hili hakika hatuna mbunge. Nadiriki kusema hivyo kwa sababu kwa miaka kibaao tangu dunia iumbwe tunakuwa kisiwani msimu wote wa mvua zinaponyesha na hata kunapokuwa hakuna mvua miezi kama hii kutokana na kukosa daraja la kupitisha maji kwa chini badala yake kuna ( flat screen tunavyoliita wenyeji)katika bonde la mto Nyasungu ambalo liko mpakani mwa vijiji vya Nzali na Mahama kata ya Chilonwa. Jambo hili limekuwa kero na kilio cha wananchi wa maeneo niliyotaja kwa mda mrefu tangu mbunge wetu akiwa Naibu Waziri wa ujenzi mpaka leo bado suluhu haijapatikana. Aidha Mbunge wetu hatukusikia anazungumza lolote kuhusu adha hii wakati bajeti ya Magufuri ilipowasilishwa. Kwa adha tunayopata sisi wananchi wa maeneo haya tunadiriki kusema hatuma Mbunge kwani hatusaidii kwa lolote wakati alipo Bungeni Dodoma mpaka sehemu husika ni kilomita 45. Wakati wa mvua kali mbunge huyo aliitwa na akaja kujionea hali halisi. Watu kwa hasira walimlazimisha avuke kwenda Nzali lakini aligoma Kabisa kwa khofia maisha yake , kwa hali hii tunadiliki kusema hatuna mbunge na tunaomba wenye kutaka ubunge wenye uchungu na wananchi wajitokeze kwa wingi mwaka 2015 nasi tutawapa kura bila kujari chama wa upinzani atapewa uzito mkubwa. manake huyu ameongoza kwa zaidi ya miaka 20 amejisahau kabisa
NAWASILISHA WANA JF NJOONI MTUSAIDIE