Na ndio maana nikasema hapo kwenye mada kuwa uumbaji wa kwanza ulikamilika baada ya siku sita baada ya hapo kila kitu kiliingia kwenye automation modeStages!
hapo mwanzo pia wanasayansi walijua mimba hutungwa ikiwa ktk umbo kamili la kibinadam!hawakujua kukusu stages kwamba manii ikiingia huanza na tone la damu kisha pande la nyama hadi kuja kutokea kiumbe chenye muonekano wa kibinadamu.
Kuna kitu me na nyie hatukifahamu je mungu hadi sasa bado anaumba binadam na kuwapulizia pumzi kama alivyofanya kwa adam?!adam alimuumba kwa mikono je mimba za sasa anaumba hivyohivyo au photocopy?!kila mtu na uelewa wake ila me naamini haumbi kama alivyofanya kwa adam isipokuwa ameshaweka hichi kitu aumatomatic kinachojiendesha chenyewe.yeye ndo mjuzi zaidi na ndio anajua zaidi sisi ametutaka tutafte elimu ikiwemo kuuliza mambo haya yasiyokuwa na majibu
Na ndio maana nikasema hapo kwenye mada kuwa uumbaji wa kwanza ulikamilika baada ya siku sita baada ya hapo kila kitu kiliingia kwenye automation mode
-mwanadamu aliyeumbwa na Mungu si huyu wa sasa..! Sasa hivi kuna Kituko
-Dunia iliyoumbwa na Mungu sio hii ya sasa... sasa hivi kuna mfano wa dunia, wanyama mimea hata vitu vunavyotuzunguka
Kimsimgi kilichopo sasa ni
Binadamu toleo la mwisho
Wanyama toleo la mwisho
Mimea na nk toleo la mwisho [emoji144] [emoji144] [emoji30] [emoji87] watu wameji edit mpaka wamekuwa kama vinyago
Kasie huwa mara nyingi nasema kwa uwazi kabisa kuwa huenda ikawa hawa wazungu sio viumbe wa hii dunia kutokana na mambo yao ya ajabu ajabu lakini vyovyote iwavyo hawataweza kuvunja ule mnyororo wa mtiririko wa maisha kwenye uumbaji. ..hivyo viwanda watafanikiwa kuvianzisha (ni kanuni ileile ya uumbaji, vitakua vitastawi hatimaye vitaleta madhara ya kufa huku vikibadilishwa matumiziUmenikumbusha..... nilisikia BBC News wakitangaza kuwa wanasayansi wanafikiria kuanzaisha maabara itakayozalisha chakula kwa ajili ya binadamu na kuiacha dunia ibaki kuwa sehemu ya starehe. Yaani nyama, maziwa, mayai, matunda n.k. n.k. vyote vitengenezwe maabara kutokana na vimelea vya bidhaa hizo......
Hapo inamaana binadamu anasitisha uumvajj na mpango aliouacha Mungu?
Just thinking loud..
Kisu kwny mfupa kaka kimenatiaNa ndio maana nikasema hapo kwenye mada kuwa uumbaji wa kwanza ulikamilika baada ya siku sita baada ya hapo kila kitu kiliingia kwenye automation mode
-mwanadamu aliyeumbwa na Mungu si huyu wa sasa..! Sasa hivi kuna Kituko
-Dunia iliyoumbwa na Mungu sio hii ya sasa... sasa hivi kuna mfano wa dunia, wanyama mimea hata vitu vunavyotuzunguka
Kimsimgi kilichopo sasa ni
Binadamu toleo la mwisho
Wanyama toleo la mwisho
Mimea na nk toleo la mwisho [emoji144] [emoji144] [emoji30] [emoji87] watu wameji edit mpaka wamekuwa kama vinyago
safi sanaView attachment 362038Najua fika kwamba wengi watadhani ni ule uumbaji wa Kimungu uumbaji ule wa dunia na kila kilichopo
Hapa nazungumzia uumbaji wa uundaji japo kuna mfanano wa ajabu kwamba dunia iliumbwa kwa siku sita na ya saba ikawa mapumziko...lakini ukija kuangalia hiyo siku ya saba Aliyepumzika ni Mungu na si vile alivyoumba
Kimsimgi uumbaji hauna mwisho kazi ya kuumbwa inapokamilishwa na muumbaji, kilichoumbwa huanza safari ya kujiendeleza uumbaji...sasa kabla hatujafika huko hebu tuone hatua hizi sita za uumbaji
1. Hatua ya kwanza ni wazo... binadamu hushauriana na nafsi yake na ufahamu wake! Hapa ni yeye pekeyake baadae huwajulisha wengine nje ya ufahamu wake na nafsi yake au hufanya mwenyewe, dhana ya umoja na wingi! Mungu akasema na 'tuumbe mtu kwa mfano wetu'
2. Matayarisho: wazo linapokubalika matayarisho huanza ya vifaa ya pesa ya watu ya eneo nk nk...Mungu yeye alikwisha andaa bustani ya eden
3. Uumbaji: baada ya matayarisho yote muhimu kukamilika kazi ya uumbaji/uundaji huanza hapa Inategemea na ukubwa au udogo wa kitu , uundaji wa meli ni tofauti na uundaji wa kitanda, Mungu alitumia siku sita kuumba ulimwengu na kuunda kila kilichopo (siku sita hizi hatujui kwa hakika kama ni hizi tunazozijua ama la)
4. Kitu kipya hutokea baada ya uumbaji kukamilika, hiki ni kitu kipya baada ya kukamilika kazi ya uumbaji, kamwe hakiwezi kuwa kipya tena daima dawamu, wala huwezi kurudia ule mchakato hata iweje....kwamba kilichoumbwa kimeumbwa na ndio maana hata Mwenyezi Mungu baada ya uumbaji ule na maudhi aliyofanyiwa na nyoka kule mbinguni na Adam na Eva kule Eden hakuweza tena kuwateketeza au kuwarudisha alikowatoa au kutengua uumbaji wa dunia na kila kilichopo
5. Uchakavu: chochote kipya kitapotoka kuundwa huanza kuchakaa hapo hapo hata kama hakitatumika kitachakaa tuu....mtoto anapozaliwa amezaliwa huwezi kumrudisha tena tumboni mwa mama yake
6. Mwisho wa matumizi, kifo kuoza na kuanza mchachato mwingine wa uumbaji...kwamba ipende unavyoipenda gari yako au nyumba yako au nguo nk..kila siku inayopita ndio inaelekea kaburi la uchakavu, au chuma chakavu uzee na hatimaye kifo na kuwa recycled tayari kwa matumizi mengine mapya aidha kwa mtindo ule ule au(reborn) au kwa matumizi mengine (reincarnation)
Kwahiyo uumbaji hauna mwisho vitu vinaundwa vinatumika vinazeeka kuharibika na kutumiwa kwa matumizi mengine
Upende mwili wako uupendavyo lakini kamwe hutakuwa wewe wa jana na wa sasa hutakuwa wewe wa kesho
Tunakuwa na mapenzi yaliyopitiliza kwenye vitu...vile tuvipendavyo sana hatutaki vituondoke, na hutumia hata nguvu za ziada kuvihodhi, vile tusivyovipenda tunataka vituondoke haraka...ni kanuni ya kiasili ya binadamu
Hakuna kidumucho milele, hatua sita za uumbaji huzunguka kwenye gurudumu lisilo na mwisho...
KUMBUKA: ZIJAPOPITA SIKU ZA FURAHA USIHUZUNIKE BALI UFURAHI KWAKUWA ZILIKUWEPO
Ishi kwa tafakuri kuu...Alamsiki...!!!
Kwamba alimaliza kazi ya uumbaji siku ya sita... tunafuata kuitii hii siku na kuienzi kwakuwa yeye alipumzika, lakini leo hii hata sasa kuna watu wana majukumu ambayo hawapaswi kupumzika, kumbuka Yesu Kristo aliponya siku ya Sabato na hii hatuwezi kusema kuwa kaitangua toratiMshana jr.naomba unifafanulie kidogo hapo mwanzo wa andiko lako kuwa siku ya saba Mungu ndiye aliyepumzika na sio aliewaumba,je tunakosea kupumzika siku ya saba?i mean siku moja ktk wiki?kama jibu ni ndio,vipi kuhusu IKUMBUKE SIKU YA BWANA NA UITAKASE?
Uumbaji wa Kimungu ni tofauti na uumbaji wa mwanadamu, yeye alitamka na ikawaSisi binaadamu tunahisabu siku kutokana na usiku na mchana na nilazima kuwepo jua na dunia,wakati mungu anaumba hivyo vitu havikuwepo je ni siku gn Mungu alizo tumia kuumba hivyo vitu?