Hatua saba muhimu za uponyaji wa CHADEMA!

LENGEJU BOB

Member
Nov 1, 2010
53
29
Na. Robert Victor Lengeju.


DONDOO
1. Busara ya Ukimya: kufikiri kabla ya kusema na kuchagua cha kusema
2. Toba, Msamaha, Upatanisho na Maridhiano
3. Kamati ya wazee wenye hekima, wasio na upande wala ushabiki na upande
4. Wasivuliwe uwanachama, lakini wasijereshwe kwenye vyeo vya awali.
5. Makundi yakemewe, yavunjwe
6. Zitto na Mbowe wakatazwe kugombea uwenyekiti.
7. Nyufa zizibwe haraka !

 
Hivi yule mheshimiwa anaye shikishwa ukuta mbona haja toa tamko lolote toka sakata la uasi lianze .... manake yeye ndiomuanzilishi wa hoja ya unafiki
 
Mimi pia nimeguswa sana na kinachoendelea CDM, kusema ukweli kufa kwa chadema hata mwana CCM makini hawezi kufurahia.
CDM ni chama cha watanzania ,niliwahi kufanya kazi na watu kutoka USA, hata kama mtu ni Republican/Democrats hawezi kuota wala kuwaza eti chama kimojawapo kife kwa maanufaa ya chama chake,mmoja alinitolea mfano wa kutupa T shirt kwa sababu umepata shart,kwa maana yeye anaamini kila nguo itafaa kwa wakati na majira furani.
Nimefarijika sana na makala yako bwana Lengeju,ni makala iliyojaa kila chembe ya Utanzania na upeo wa kuionea huruma hii nchi,maana anaye ionea huruma nchi hii ni sharti awe na maono ya kukomaza Demokrasia.

Ni kweli usio pingia kuwa binadamu tumeumbwa kwa kutofautia mmoja na mwingine,ili maisha yaende ni sharti tukabali usemi usemaosema (give and take).

Haiwezekani tukubaliane kwa kila jambo,na ukikuta watu wanakubaliana kila jambo,fuatilia huenda watakuwa na matatizo ya kufikiri,nadiriki kusema huenda ni majuha.Maana haiwezekani watu wote watano mfano mukubaliane kwa kila kitu,haiwezekani,ila watu wenye busara hukubali pia mawazo pinzani/kinzani na wao.

Mfano mimi ni Dr wa magojwa ya binadamu,nawaza namna gani mgonjwa anaye umwa ugonjwa fulani nitamtibuje,mwingine ni engineer anawaza hivi atapitisha umeme kwenye maji ufike Zanzibar. Laiti hawa wote wangewaza kitu kimoja hakika maisha yangekuwa majanga,dunia ingekuwa sehemu mbaya kabisa kuishi,lakini kwa kuwa binadamu tunatofautiana kuna vitu anuwai vinaendelea kwa wakati mmoja.

Hivyo mimi ni muumini mkuu wa kuamini kila fikira/wazo au mtizamo furahi unahiji kuangaliwa kwa umakini mkubwa pengine unaweza kuwa ndo mwanzo wa kitu kimoja bora kabisa,ili mradi umepewa nafasi ,umepata tafakuri ya kina na kuja na ufafanuzi wenye kuonesha mlengo hasi na chana na watu ambao hawana mlengo fulani ili kutendea haki wazo/mtizamo fulani.Ikidhihirika kuwa si bora kwa wakati wowote au kwa wakati huu au wakati fulani,pia mwenye wazo akubali au aende ajipange upya kwa maana ya kuboresha zaidi,au atafute namna nyingine ya kuwasirsha mawazo yake apate kueleweka maana pingine hakueleweka vizuri,ila asitumie nguvu au jadhiba kuladhimisha anachoamini.

Mh ZZK na wenzie pamoja na Viongozi wa chadema walioko madarakani hasa Mwenyekiti wetu mpendwa Freemani Mbowe kama kweli wanapenda maendeleao na uhai wa demokrasia changa ya nchi yetu ,niwaombe tu wasome makala ya huyu bwana hasa hatua ya kwanza,ya sita na ya saba.

Kijana amejitahidi sana kuchambua bila kuegemea upande wowote,binafsi nakubaliana naye mia kwa mia.Tofauti zetu sizizime doto ya vijana wa kitanzania.

Pia naomba niwaonye wana chama wa chama pinzani na CDM kama kweli wako nyuma ya mipango hii ovu,hawako salama maana dhambi hii ni kubwa kuliko ufisadi,hela zinatafutwa ila demokrasia hainunuliwi kwa pesa wala thamani yake haipo.

Litakuwa jambo la ajabu sana eti mtu kuwa CCM anafanya mipango ya kuua chama kingine tena kwa kodi zetu,ni dhambi ambayo huwezi kutubu ukapata msamaha.

Kwa hili naomba Rais Kikwete aingilie kati,pamoja na mambo mengi anayozushiwa Mkuu wa nchi yetu sijaona akiwa msitari wa mbele kuhanisi demokrasia ya nchi yetu.
Naamini anayo nia thabiti ya kuona emokrasia ya nchi yetu inakua kuliko wakati wowote wa uhai wa Taifa hili changa,hivyo sidhani wala siamini kama anaweza kuruhusu hela za kodi zitumike kunajisi demokrasi kiasi hiki.

Mungu ibariki Afrika,Mungu ibariki Tanzania
 
Mungu baba muweza wa yote hebu wafunulie hawa wana wako walau waweze kung'amua hiki kilichofafanuliwa na huyu ndugu. Personally naikubali makala hii.
 
naomba ufafanuzi juu ya kitila mkumbo.
_ ali kiri makosa gani?
_ali kubali kuratibu na kuandika waraka?
_alikiri kutengeneza mparaganyiko wa chama?
Embu naomba upembuzi yakinifu juu ya kile kinachosemwa kuwa mkumbo ali kiri.
Na kwa kuongezea maadam wewe umeruka kesi ya uhaini wa zitto na mkumbo basi tukubali kuwa alicho kifanya zitto na mkumbo ni kukubali yaishe kwa wakati ule ili kuepusha malumbano
labda niseme bila uwoga kwamba zitto na mkumbo hawana hatia yoyote, na kama wataendelea kuwatuhumu kuwa niwahalifu wa chama. ni kwamba hii vita ya maneno majukwaani haito isha na mwisho wa siku itabaki tukose wote.
 

Hakuna cha kukosa wote wala nini, wao waende huko kwa wenye mahaba nao, wote tumeshuhudia wanao kuja kuwatetea na kulia lia kwamba hawajatendewa haki ni kinanani? Hivi hata kama una ubongo mdogo kama wa kuku huwezi kujiuliza kulikoni jirani kulia hadi kuzimia kwa ajili ya msiba wa mchumba wako?
 
Hillarious indeed....!

Yaani Mbowe anyimwe haki yake ya kikanuni,kikatiba na kidemokrasia kwa sababu ameongoza kikao kilichowaadhibu wasaliti?

Yes,CHADEMA ina watu wengi.Wapo akina Lissu na wengine wenye misimamo isiyotiliwa shaka lakini haiwezi kuwa hoja ya kumnyima Mbowe nafasi ya kugombea
 
Uchambuzi ni mzuri ila hapa penye kifungu kuwa mbowe na zitto wasigombee wengi utawatanza ingawa pana ukweli
 
yan Mungu katuumba tofauti sana yan kunabaadhi ya wa2 akili zao cjui zkovp, anapotokea m2 anaeandika mambo mazur na muhimu kwa ustawi wa demokrasia ya nchi na chama(cdm) wao huwa mstari wa mbele kucreticize,bila hata hoja ya msingi, tubadilike jamani, sio kila wakati lazima uchangie mada kama ur pointless
 
Sijapata kusoma andiko lililosheheni busara kama hili tokea kuanza kwa sakata hili tete na nyeti kwa ukuaji wa demokrasia nchini mwetu. Hakika mwandishi huyu anastahili heshima. Ameweka mizania sawa katika kila kipengele alichokijadili, na ametoa mapendekezo mujarab kwa tatizo hili tete.
 
With due respect you are PRO ZITTO! Baregu pia ni PRO ZITTO! Dr Lweitama ni Neutral, Prof Safari ni PRO ZITTO pia! All in All CCM hawamtaki MBOWE kwenye Chair kwa sababu chini ya uongozi wake CHADEMA wamefanikiwa sana! Ni rahisi tu CHADEMA imejengwa na watu ambao katika biashara zao wamefanikiwa hivyo misingi ya uongozi wanaijua maana wanaitumia kila siku kwenye biashara zao ambazo zimefanikiwa!!
 

Umenigusa, umenitia Moyo...Asante
 
Kaka, heshima yako. Binafsi si Mwana Chadema ila ni mfuasi wao mkubwa. Kama alivyosema mchangiaji mmoja hapo nakiri sijawahi kuiona makala iliyochambua mgogoro huu na kujaribu kutoa suluhu kama ulivyofanya wewe. Niseme tu Zitto na Kitila wana makosa makubwa lakini yaliyoandikwa kwenye huo waraka yapo yenye ukweli ndani yake.

Nashauri makala yako hii isambazwe kwenye magazeti hasa ya Jumapili na Jumatano ili Watanzania walau sasa baada ya kusikia malumbano ya pande mbili kwa muda mrefu sasa wasome mawazo ya watu wanaotafuta suluhu katika mgogoro huu.

Hili la Mbowe na Zitto kuzuiwa kugombea lilipaswa kuwa la kwanza kwa sababu inaelekea ndio kiini ch mgogoro huu. Wanaosema Mbowe ana hakiya kugombea wajiulize kwanini Zitto alishauriwa ajiondoe mwaka 2009 na akakubali? Kama nia ni kujenga chadema imara kuelekea 2015 ni vizuri watu wakajifunza ku sacrifice baadhi ya mambo.
 
Sultan mbowe na mtakatifu mchukua wake za watu na ww mbeba sumu naliona anguko lenu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…