Hatua 6 za kumzuzua Mwanamke

Hatua 6 za kumzuzua Mwanamke

Ethan Cruz

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2021
Posts
231
Reaction score
331
charming-a-woman.jpg

1. Pokea pongezi
Wanaume wengi wanatabia ya kukataa kupokea pongezi kutoka kwa mwanamke. Balada ya wewe kuguna ama kutojiskia huru wakati mwanamke anakupongeza, mbona usitumie nafasi hii kutumia maneno ya utamu kama ile 'asante, 'nashukuru' nk.

Kupokea pongezi kutoka kwa mwanamke ni kama vile kupokea zawadi kutoka kwake, hivyo kufanya hivi kutakuwa kukimfurahisha mwanamke kila wakati.

2. Kuwa na maoni chanya kujihusu
Kama hujiamini wewe mwenyewe ama unajiona huwezi kutimiza kumfurahisha mwanamke je unatarajia mwanamke akupende? Hivyo basi iwapo unataka kumzuzua mwanamke unafaa ujiamini wewe mwenyewe kama mwanaume.

Njia rahisi ya kutimiza hii ni kuhakikisha unavalia nguo za kupendeza, unavalia marashi yakunukia, na kuwa nadhifu. Wanawake wengi wanapenda mtizamo aina hii.

3. Jifundishe kudensi
Ok wengi wangeuliza kwa nini nijifunze kudensi? Kudensi ina uhusiano wowote upi na kumzuzua mwanamke? Jibu rahisi. Kwanza ni kuwa wanawake wanapenda sana wanaume ambao wanajua kudensi. Hivi ushajiuliza kwa nini dancers wengi wanapendwa na wanawake?

Pili ni kuwa wanawake wanaamini ya kuwa dancers wengi wanaujua mchezo ikija maswala ya chumbani.
Tatu ni kwa hautarajii mwanamke unayemzimia adensi na wanaume wengine wakati mumeenda kwa kilabu

So ni muhimu kujifunza kudensi, atleast style moja mbili za kumdanganya.

4. Tumia jina lake
Siri nyingine ya kumzuzua mwanamke ni kumtaja jina lake wakati wa maongezi. Kulingana na mwandishi maafuru wa kiingereza Dale Carnegie, anadai ya kuwa sauti tamu zaidi kwa sikio la mwanamke ni kusikia ukitaja jina lake.

Kama umekuwa ukifanya uchunguzi ni kuwa wengi wanahepa kutumia majina ya wapenzi wao nk. Hivyo wewe usikubali kuanguka ndani ya hio kategoria. Waonaje sasa uanze kutumia jina lake kila wakati unapomtext ama kuongea naye? Amini usiamini jambo hili linafanya kazi kama uchawi.

5. Muangazie yeye
Iwapo unataka mwanamke akuchukie kwa siku moja basi ongea na kujisifu wewe mara kwa mara wakati mnapoongea pamoja.

Iwapo unataka kumzuzua mwanamke basi kinachohitajika ni kuhakikisha unampa atenshen yako yote wakati mko pamoja mnaongea.

6. Kuwa mcheshi
Imethibitishwa ya kuwa hakuna mtu angependwa kujihusisha na mtu anayeboa. Hivyo kama unakipawa cha ucheshi ama unauwezo wa kumfanya mwanamke avutiwe nawe basi hio ni silaha kubwa ya kumfanya mwanamke azuzuike kwako.
 
Mwanzo nilimpata mke bora sana nikajitahidi kukidhi kila haja ya moyo wako,,ila fedha ilipoanza kuisha kutokana na matatizo ya hapa na pale ndipo nikajua tabia halisi ya mwanamke,,,sasa najiona nilichelewa sana kutafuta hela .....
ndo ile kosa pesa ujue tabia ya mkeo, mybe hulka yake tu kz alikuja kwako kipesa pesa na ndomana akaondoka baada ya pesa kukata koz wadhifa huna
 
Nilifanya hayo yote ila mwisho wa siku kaniacha solemba.
 
Kama mapenzi ni marahisi hivyo kusingekuwa na break up, unadensi mbele yake ukidhani kuwa unamfurahisha kumbe anakuona wewe ni mtu uliyekosa mwelekeo wa maisha.

Mapenzi ni magumu sana.
ss na ww udensi mbele yake iyo ni akili za usiku yan ndo kwanza una mmeet af uanze kujichezeshaa aaa boi sio kwly iyo ni next stage after party
 
Namba4 naiamini sana...nikimtumiaga demu wangu text nikaandika na jina lake anaReply fasta na kimaha kabisaaa
 
Mapenzi yanataka kuyarespct, insurence na matakataka mengine ya ziada
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom