Hatimaye Mheshimiwa Rais Magufuli kutembelea Kagera, Wapinzani mtakuja na ngonjera ipi tena?

Don san tan

JF-Expert Member
May 23, 2015
562
433
KAGERA

Leo Rais wa Jamhuri wa Muungano Mh. John Pombe Magufuli anategemewa kuwasili mkoani
humo kwa ziara ya siku mbili yenye lengo la kuwatembelea wananchi walioathirika na tetemeko la Ardhi lakini pia kuzindua na kuweka mawe ya msingi katika miradi kadhaa ya maendeleo ambayo yaliathiriwa kutokana na
tetemeko hilo mkoani humo.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Mstapha jana alisema Rais ataingia asubuhi ya leo akitokea Geita na baadaye atahudhuria ibada ya misa na kesho yake ndiyo atawatembelea baadhi ya wananchi waliotumia nguvu zao kujenga nyumba
zao na makazi baada ya kuharibiwa na tetemeko la Ardhi kisha atatembelea miradi ya ujenzi wa shule ya Sekondari ya Ihungo na kuweka jiwe la msingi na kuzungumza na wananchi.
 
Mmmmh mwaka mpya huu labda atakua anasoma hotuba
 
wataanza kusema, Oooh!! amechelewa kwenda.
kweli kabisa They have no new. Tuwakalie kimya tu maana hawana Effect yoyote kwetu Watanzania.
 
Hapo atakuwa amefanya very good wale ambao hawajatumia nguvu zao kujenga nyumba zao asiwatembelee inawezekana ni wakimbizi si wa TZ

Kweli mtaisoma namba na wale madiwani kule Arusha sijui wamepata dhamana
 
Watu wameteseka weee na wengine wamepoteza maisha eti sasa ndiyo anaenda kuwapa pole, kafungua mwaka vibaya
 
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli.
Akufaaye kwa raha tu sio rafiki wa kweli
Akutembeleaye ukiwa gerezani huyo anakujali.
Akutembeleaye wakati wa sikukuu wakati hakuja kukuona gerezani huyo si rafiki wa kweli
 
Hayo ni majukumu ya rais na si kusubiri wapinzani wakorome au kufanya jambo kuonyesha wapinzani hayo ni mawazo mfu
 
Naona raisi JPM atawatolea uvivu wazushi wote hukohuko Kagera, stay tuned.
 
Amechelewa Sizonje
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…