Hatimaye Kamati ya Mwakyembe yaanika ufisadi TRL

Hatimaye Kamati ya Mwakyembe yaanika ufisadi TRL

Unataka ushahidi gani? Si nenda Yono Auction Mart ukachunguze? Umekuwa toto jinga utafuniwe kila kitu?

Ukitaka taarifa zaidi kiwanja chenyewe ni plot numbers 160&161 kinatazamana na hoteli ya Bahari beach. Ikulu wanajua na ndio maana walimtoa hiyo wizara. Angelikuwa mtu mwingine angefukuzwa kabisa. Ila walijua Mwakiembe angeanza propaganda zake kwamba kaonewa. Wakamtuma rafiki yake Sitta ashuhudie ufisadi wake.

Kiwanja hicho alitaka kukifanya eneo la ku park magari kwa abiria watakaokuwa wanatumia hiyo meli kutoka Bagamoyo kwenda kule mjini. Ila wamemtoa kabla na dili imelala.

Tunajua mengi sana ya Mwakiembe. Karma ya Pasco imeanza kumrudia baada ya kumwonea Lowassa.

Wewe Jenifa si umeleta tuhuma humu. Sasa mbona unalilia. Futa machozi Nenda kwa huyo Michael Jackson wako Yono akupe ushahidi Acha blaa blaa hapa. Nchi haiongozwi kwa maneno ya mtaani. Nenda Kariakoo kapike ushahidi wako ulete hapa Tukushuhulikie.Sijui hata shule umesoma wapi, manake unashindwa kuelewa kuwa ukimtuhumu mtu unapaswa kuleta ushahidi usio na chembe ya shaka.
 
Nadhani hawa wataitwa pembeni waulizwe: Mlichukua bei gani? Haya lete ya kampeni hapa, alfu mjifanye kama mmesimamishwa?
 
Nadhani imefiia mahali sasa inabidi Serikali iangalie kwa makini sana maamuzi ya kufanya biashara ya manunuzi India. Hawa watu wana asili ya rushwa sana, sitaki kuwa mbaguzi lakini tufuatilie sana kwa umakini na kwa kipindi kirefu utaona kwamba hakuna manunuzi yoyote ya fedha nyingi yaliyowahi kufanyika ikahusisha hawa wenzetu ikawa na manufaa kwa Taifa letu.
Inasikitisha kwamba bado tunakumbatia mambo haya kijinga jinga mpaka leo. Nikikumbuka EPA......... siandiki zaidi. naachia hapo.
 
Taarifa za uwakika pasipo shaka yoyote kutoka kwa mmoja wa wajumbe wa tume ya uchunguzi wa ununuzi wa mabehewa ya TRL iliyoundwa na aliyekuwa Waziri wa uchukuzi ambao wamekabidhi ripoti yake kwa Mhe. Sita Waziri wa sasa wa uchukuzi imeweka wazi jinsi wataalam wa TRL walivyofisadi

Nchi kwenye ununuzi wa haya mabehewa.

Mojawapo ya maajabu ya Musa kama siyo ya firahuni ni pale hawa wataalam walipobadilisha specification s na baadhi ya vipengele vya mkataba baada ya ukaguzi nchini India ili mkataba ukidhi walichokuta huko na siyo mtengenezaji atengeneze kwa mahitaji
yetu... Bila huruma wala weledi wakaweka matumbo yao Mbeleeee.

Tumwombe Mhe. Waziri awachukulie hatua stahili na wapelekwe Kmahakamani kwa kuhujumu uchumi na siyo kuwahamishaa.

Tegemea report kamili hapa.

Kuna mambo mawili ambayo hatujajua body ya Zabuni iliegemea huko ama la, haijajulikana!

PPRA inamtaka mtu ambaye ni Lowest EVALUATED Bidder apewe tenda. Lowest EVALUATED Bidder ni tofauti na LOWEST BIDDER!

Kigezo kingine labda yaweza kuwa ni ile Sentensi inayosema Mwajiri halazimishwi kukupa ushindi wa Zabuni kwa namna yoyote ile ima kwa kuwa gharama zako ni ndogo haiwezi kuwa ni sababu ya mzabuni kushinda. Case fulani fulani husababisha tender kuwa Re-advertised!
 
hivi bosi wa katibu mkuu wa wizara ni waziri au katibu mkuu kiongozi,swali tu nauliza maana kama katibu ni mhusika wa mikataba maana copy lazima awenayo katibu mkuu wa wizara sasa katibu mkuu kiongozi na wewe unacopy na taarifa nzima ya mchakato msaide babu Sitta kumaliza huu utata mtafukuza watu weeeeee waliopiga wametulia kimya
 
Hapo najua Manji-Quality Group)hajakosekana,hiyo pesa ni ya ccm wamepiga hapo
 
Back
Top Bottom