Hatimaye Julius Malema atia neno kuhusu Magufuli

joto la jiwe

JF-Expert Member
Sep 4, 2017
26,117
46,613


Hii ni Mara ya kwanza kwa kiongozi machachari na kijana wa Afrika Kusini, Julius Malema kutia neno lolote kuhusu rais Magufuli.

Kwa muda mrefu amekuwa akifuatilia siasa za ukanda huu wa Afrika Mashariki na mara nyingi amekuwa akimkosoa sana rais wa Uganda, Yoweri Museveni na kumuunga mkono Bobi Wine, lakini hajawahi kushughulika sana na siasa za Tanzania.

Uvumilivu umemshinda baada ya kusikia mengi, hasa kitendo cha Magufuli kukataa masharti ya wachina katika mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo.

Katika "account" yake ya Twitter, amempongeza Magufuli kwa uamuzi wake huo. Hongera sana Magufuli.
 

Hii ni Mara ya kwanza kwa kiongozi machachari na kijana wa Afrika Kusini, Julius Malema kutia neno lolote kuhusu rais Magufuli.

Kwa muda mrefu amekua akifuatilia siasa za ukanda huu wa Afrika mashariki na Mara nyingi amekua akimkosoa sana rais wa Uganda, Yoweri M7 na kumuunga mkono Bobi Wine, lakini hajawahi kushughulika sana na siasa za Tanzania.

Uvumilivu umemshinda baada ya kusikia Mengi, hasa kitendo cha Magufuli kukataa masharti ya wachina katika mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo. Katika "account" yake ya tweeter, amempongeza Magufuli kwa uamuzi wake huo, Hongera sana Magufuli.

Hii yote ni kwa juhudi za JPM,Hongera sana Malema kwa kumpongeza JPM....Hii itatusaidia sana Uchumi wetu Kukua.
 
Kwa muda mrefu amekuwa akifuatilia siasa za ukanda huu wa Afrika Mashariki na mara nyingi amekuwa akimkosoa sana rais wa Uganda, Yoweri Museveni na kumuunga mkono Bobi Wine, lakini hajawahi kushughulika sana na siasa za Tanzania
Maana ya hiyo ni kwamba vyama vya upinzani, hasa CHADEMA na ACT-Wazalendo wameshindwa kutoa habari za kutosha huko nje, watu wajue upande wa pili wa huyo anayesifiwa. Nina hakika huyu kijana Malema asingetumia muda wake kusifia hayo aliyoyasifia.

Mh. Zitto kazi imewashinda?

Hata hivyo inaonyesha Malema hana taarifa sahihi hata juu ya hayo aliyoyasemea.
 


Hii ni Mara ya kwanza kwa kiongozi machachari na kijana wa Afrika Kusini, Julius Malema kutia neno lolote kuhusu rais Magufuli.

Kwa muda mrefu amekuwa akifuatilia siasa za ukanda huu wa Afrika Mashariki na mara nyingi amekuwa akimkosoa sana rais wa Uganda, Yoweri Museveni na kumuunga mkono Bobi Wine, lakini hajawahi kushughulika sana na siasa za Tanzania.

Uvumilivu umemshinda baada ya kusikia mengi, hasa kitendo cha Magufuli kukataa masharti ya wachina katika mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo.

Katika "account" yake ya Twitter, amempongeza Magufuli kwa uamuzi wake huo. Hongera sana Magufuli.
Kitu kimoja ninachoweza kukubaliana na Magufuli ni kukataa masharti ya mkataba wa Bandari ya Bagamoyo.
 
Tunaoishi Tanzania tunamfahamu na tunayafahamu anayoyafanya kuliko mtu mwingine yeyote. Ni aheri maneno hayo yangetoka kwa Balozi wa Afrika Kusini nchini Tanzania maana huyo anaona mema na mabaya yote yanayotokea nchini mwetu.
 
Tunapokea pongezi za Malema ambaye ni kiongozi wa chama maarufu cha upinzani cha Economic Freedom Fighters EFF. Malema ndiye Lissu w Afrika Kusini. Huku Lissu wetu tumemvua mpaka ubunge na kumtelekeza huko nje akihudumiwa na mabeberu.
wacha aendelee kuhudumiwa na mabeberu kwa sababu ndio anapenda..inamlipa zaidi kuliko kitumika Tanzania...ubunge kwani lazima yeye tu ndio anauweza..yani mtu akae kitandani hospitali miaka halafu mnasema.aendelee.kuwa mbunge..hampendi maendeleo ya wananchi wa jimboni kwake naona..nyinyi ni wabinafsi wa kiwango cha divisio eight
 
Tunaoishi Tanzania tunamfahamu na tunayafahamu anayoyafanya kuliko mtu mwingine yeyote. Ni aheri maneno hayo yangetoka kwa Balozi wa Afrika Kusini nchini Tanzania maana huyo anaona mema na mabaya yote yanayotokea nchini mwetu.
mabaya ni yapi mama..wananchi walio wengi asilimia zaidi ya 90 wako nyuma ya Magufuli msee. hawakuelewi unavyosema hili..wewe utakuwa muathirika wa makinikia..au vyeti feki..tafuta kazi ya kufanya mama utaaibika mjini
 
The young man is misinformed au na yeye yuko kazini kuhujumu mradi kwa kumsifia Jiwe ili asifanye mradi ambao ungezaa bandari kubwa kuliko bandari zote zilizoko ukanda wa bahari ya hindi ikiwemo ya Durban nchini mwao
pumbafff zao , eti bandari kubwa...khaaa...kwa faida ipi hasa...
 
Maana ya hiyo ni kwamba vyama vya upinzani, hasa CHADEMA na ACT-Wazalendo wameshindwa kutoa habari za kutosha huko nje, watu wajue upande wa pili wa huyo anayesifiwa. Nina hakika huyu kijana Malema asingetumia muda wake kusifia hayo aliyoyasifia.

Mh. Zitto kazi imewashinda?

Hata hivyo inaonyesha Malema hana taarifa sahihi hata juu ya hayo aliyoyasemea.
tueleze wewe labda unayoyajua kwa sana kuliko hao uliowataja..wenzano wanaona aibu kutamka uongo juu ya Magufuli..wanaogopa kusutwa na wananchi wakati wa kampeni..majimboni mwao..unafanya mchezo.nini..watu wapo strategically..hawakurupuki kama wewe jomba
 
Tunapokea pongezi za Malema ambaye ni kiongozi wa chama maarufu cha upinzani cha Economic Freedom Fighters EFF. Malema ndiye Lissu w Afrika Kusini. Huku Lissu wetu tumemvua mpaka ubunge na kumtelekeza huko nje akihudumiwa na mabeberu.
Kama Lisu alituambia issue ya Acacia tutapata aibu ya karne na hatujaipata . Tunawezaje kumuamini kama si kibaraka wa mabeberu?
 
Back
Top Bottom