Hatimaye Edward Snowden apata ajira Russia

Hatimaye Edward Snowden apata ajira Russia

EMT

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
14,477
Reaction score
15,347
650089_orig.jpg

650089_orig.jpg

Aliyekuwa mwajiriwa wa NSA nchini Marekani Edward Snowden amepata kazi ya kusimamia tovuti huko Russia, ambayo kama ilivyo usiri wa sehemu anayoishi, vile vile jina la tovuti hiyo nalo halijawekwa bayana. Picha inayoonekana hapo juu inamwonesha Snowden akiwa na mmoja wa watunga sheria wa Ujerumani, na mwanakamati wa Kamati ya Bunge inayohusika na uangalizi wa shughuli za Mashirika ya Kiusalama ya nchi Ujerumani, Hans-Christian Sroebele ambaye walionana hivi karibuni kwa lengo la kuzungumzia zaidi kuhusu sughulli za udukuzi za NSA.

Barua aliyoiandika kwa anwani ya Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel akiielekeza kwa Serikali ya Ujerumani, alimkabidhi mmoja wa watunga sheria wa Ujerumani, Hans-Christian Sroebele, ambaye naye aliiwasilisha kwa wanahabari Ijumaa ya leo, amesema kusema ukweli kamwe si kosa na hivyo anaamini uungwaji mkono anaoupata baada ya kufichua siri na shughuli za NSA, zitasaidia kuishinikiza Serikali ya Marekani kupunguza 'tabia haribifu' ambayo inamzuia pia kutoa siri zaidi za udukuzi unaofanywa na Serikali hiyo. Snowden amekaririwa pia akisema kuwa yupo tayari kwenda nchini Ujerumani kusaidia uchunguzi kuhusia na na udukuzi unaodaiwa kufanywa na Marekani dhidi ya Kansela Merkel.

Wakati huo huo, kitengo cha Haki na Sheria cha Serikali ya Marekani kimejiunga kwenye kesi iliyofunguliwa dhidi ya 'mpiga filimbi' aliyeishitaki shirika la USIS (United States Investigations Services) iliyopewa dhamana na mkataba tangu mwaka 1996 kwa ajili ya usalii na usajili wa watu wanaoomba kuajiriwa na Serikali, kuwa haikufanya kazi yake kwa makini katika kuchunguza nyendo za nyuma za Snowden (quality control reviews in background check) na hivyo kushindwa kumshauri vyema mwajiriwa wake. Mashitaka hayo yalifunguliwa katika mahakama ya Alabama zaidi ya miaka miwili iliyopita.

USIS ndiyo iliyohusika pia na kuajiriwa kwa Aaron Alexis, askari mtaalamu wa teknolojia, aliyefyatua risasi katika ofisi za kituo cha jeshi la maji na kuua watu 12 huko Washington mwezi uliopita. Tayari msemaji wa USIS amekiri kuwa wanashirikiana na Serikali katika uchunguzi na tayari wameshafanya marakebisho ya kiuongozi ikiwa ni pamoja na kuongeza ufanisi katika kazi zake tangu mwaka jana zilipoanza kutoka kashifa dhidi yake. USIS inashutumiwa kuzembea na kufanya kazi yake kwa kulipua kuanzia mwaka 2008 ili kufikia malengo ya Serikali.


Source: Snowden apata ajira, akutana na Kiongozi wa Ujerumani - wavuti.com
 
Marekani wataiweza wapi... huyu Dogo kichwani hazimo.... nadhani walifanya kosa kutomchunguza kwenye kazi nyeti kama hizo alizowahi fanya..... na isije kuwa ni janja ya Nyani waache na wao wamuweke kwenye matovuti yao ndio watakuja mfahamu vizuri siku za Usoni... Msaliti haachi kusaliti
 
Du hii ishu hii ni noma aisee

Kwa Mmarekani litatulizwa tu... ni sawa na Wanafunzi wagome kufanya mtihani... wanajua watakachopata..... ni kuishi bila cheti.... hii kitu ya kumvimbishia Mmarekani haina Mashiko.... Huwezi msemea baba yako polisi afungwe wakati yeye ndie anayekutunza na kukulisha
 
Marekani wataiweza wapi... huyu Dogo kichwani hazimo.... nadhani walifanya kosa kutomchunguza kwenye kazi nyeti kama hizo alizowahi fanya..... na isije kuwa ni janja ya Nyani waache na wao wamuweke kwenye matovuti yao ndio watakuja mfahamu vizuri siku za Usoni... Msaliti haachi kusaliti

Who knows... maybe Marekani wanamtumia kiaina dhidi ya Russia?
 
Ndiyo madhara ya kuwa na mashoga kwenye taasisi nyeti kwa kujifanya haki za binadamu matokeo yake ndiyo hayo.
 
....and that's why Mr. Putin is now the most powerful person on earth.
 
Kama anacheza michezo kwa warusi watamnyonga!manaa ukute kuna kitu ambacho kiko mbali sana kinatengenezwa hapo!!
 
Kwa Mmarekani litatulizwa tu... ni sawa na Wanafunzi wagome kufanya mtihani... wanajua watakachopata..... ni kuishi bila cheti.... hii kitu ya kumvimbishia Mmarekani haina Mashiko.... Huwezi msemea baba yako polisi afungwe wakati yeye ndie anayekutunza na kukulisha

he he he he he he he he
 
I dont trust him,sidhani kama kweli aliisaliti marekani.
 
Back
Top Bottom