Hayawi Hayawi Yamekuwa!
Akina Karl Marx huko nyuma waliyasema - na sio kwa kutabiri bali kwa kutafakari michakato na mwelekeo wa mabadiliko ya kiuchumi na Kijamii - Kwamba utafika wakati mfumo fulani utajichokea wenyewe kwa sababu za michakato inayopitwa na wakati, misuguano, mivurugano ya ndani ambayo itawafanya wadau wake kuchokana wenyewe kwa wenyewe, na wanaosubiri kupata riziki kupitia mfumo huo uliopo kukata tamaa.
Hayati Nyerere alianza na falsafa ya kugawana riziki kupitia sera za udhibiti wa rasilimali za taifa ili kuondoa tofauti za kipato miongoni mwa wananchi na wote tuwe sawa.
Ustaadhi Mwinyi akaja na sera za soko huria ili kuwainua wananchi katika kutafuta riziki na kuupiga vita ukabwela usio wa lazima.
Mkapa akaja na sera za ubinafsishaji na juhudi za kubana mianya ya ukwepaji ukusanyaji wa mapato ili serikali iwe na nguvu ya kiuchumi kwa maslahi ya wananachi wake.
Bwana Kikiwete amefanya kazi kubwa sana ya uendelezaji wa miundo mbinu ya kitaifa ili kufungua milango ya kifursa za kibiashara na uzalishaji, na uwekezaji wa nguvu sekta zote.
Yote haya yaliyofanikiwa na yasiyofanikiwa yamefanyika chini ya uongozi wa Chama Tawala, ambacho sasa kinaelekea kuishiwa sera na hatimaye kubakiwa na dhana ya kutafuta "mtu ama watu" wa kuwatwisha mzigo wa udereva wa nchi hii, badala ya sera na mikakati inayoonekana itawahakikishia WaTz nafuu na maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii.
Na ndio sababu tunaona kina Membe, Makufuli, Sita, Ngoyayi, na wengine wakihamasishwa kujitokeza, na kupigiwa debe huku na huko, ili watafute fursa ya uongozi, bila kujali mustakabali wala muktadha wa sera za Chama hiki na ahadi zake kwa Wananchi.
Ni wazi kabisa hiki Chama kikongwe kimefikia hatua ya uzee, kuchoka, na hatimaye kuchokwa na Watz walio wengi.
Mivutano iliyomo ndani ya chama endapo itafikia hatua ya kuteuliwa mtu kugombea uongozi ati kwa kuwa kuna dhana ya "anapendwa na Wengi" ambayo haina mashiko zaidi ya hisia na sababu za kimaslahi za wapiga debe wake, ndipo maneno ya kina Marx yatakapo dhihirika kwa kuwa siku zote JAMII SIO MGANDO, BALI HUBADILIKA KWA KUWA NDIO MAUMBILE YAKE.
Na hiki Chama kikongwe kitajikuta kikihifadhiwa kwenye dampo la taka taka za historia.
Ni suala la muda tu......Just a matter of Time.
Akina Karl Marx huko nyuma waliyasema - na sio kwa kutabiri bali kwa kutafakari michakato na mwelekeo wa mabadiliko ya kiuchumi na Kijamii - Kwamba utafika wakati mfumo fulani utajichokea wenyewe kwa sababu za michakato inayopitwa na wakati, misuguano, mivurugano ya ndani ambayo itawafanya wadau wake kuchokana wenyewe kwa wenyewe, na wanaosubiri kupata riziki kupitia mfumo huo uliopo kukata tamaa.
Hayati Nyerere alianza na falsafa ya kugawana riziki kupitia sera za udhibiti wa rasilimali za taifa ili kuondoa tofauti za kipato miongoni mwa wananchi na wote tuwe sawa.
Ustaadhi Mwinyi akaja na sera za soko huria ili kuwainua wananchi katika kutafuta riziki na kuupiga vita ukabwela usio wa lazima.
Mkapa akaja na sera za ubinafsishaji na juhudi za kubana mianya ya ukwepaji ukusanyaji wa mapato ili serikali iwe na nguvu ya kiuchumi kwa maslahi ya wananachi wake.
Bwana Kikiwete amefanya kazi kubwa sana ya uendelezaji wa miundo mbinu ya kitaifa ili kufungua milango ya kifursa za kibiashara na uzalishaji, na uwekezaji wa nguvu sekta zote.
Yote haya yaliyofanikiwa na yasiyofanikiwa yamefanyika chini ya uongozi wa Chama Tawala, ambacho sasa kinaelekea kuishiwa sera na hatimaye kubakiwa na dhana ya kutafuta "mtu ama watu" wa kuwatwisha mzigo wa udereva wa nchi hii, badala ya sera na mikakati inayoonekana itawahakikishia WaTz nafuu na maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii.
Na ndio sababu tunaona kina Membe, Makufuli, Sita, Ngoyayi, na wengine wakihamasishwa kujitokeza, na kupigiwa debe huku na huko, ili watafute fursa ya uongozi, bila kujali mustakabali wala muktadha wa sera za Chama hiki na ahadi zake kwa Wananchi.
Ni wazi kabisa hiki Chama kikongwe kimefikia hatua ya uzee, kuchoka, na hatimaye kuchokwa na Watz walio wengi.
Mivutano iliyomo ndani ya chama endapo itafikia hatua ya kuteuliwa mtu kugombea uongozi ati kwa kuwa kuna dhana ya "anapendwa na Wengi" ambayo haina mashiko zaidi ya hisia na sababu za kimaslahi za wapiga debe wake, ndipo maneno ya kina Marx yatakapo dhihirika kwa kuwa siku zote JAMII SIO MGANDO, BALI HUBADILIKA KWA KUWA NDIO MAUMBILE YAKE.
Na hiki Chama kikongwe kitajikuta kikihifadhiwa kwenye dampo la taka taka za historia.
Ni suala la muda tu......Just a matter of Time.