Hatimae leo nimempeleka Polisi

Hatimae leo nimempeleka Polisi

Kuna mshkaji ameniblock sababu aliniomba nimkopeshe laki 3,ile kumuambia sina hiyo pesa kaniblock whatsapp ,halafu ajabu dec last year alikata tiketi za atcl 4 go & return mwanza kula x mass,leo ananiblock kwa kutokua na laki 3 ya kumkopesha!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mm huwa sikopeshi mtu, labda nikupe tu tu.

Na wala huwa sikopi pesa.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Habarini za mdahuu,..ngoja niende moja kwa moja kwenye mada..kuna kijana nilimkopesha kiasi Cha pesa Kama laki mbili..kwa matarajio ya kurudisha baada ya miez miwili. Matokeo yake mwaka Sasa unakaribia kukata,..tangu mwezi wa 3 jana Hadi hivi leo 2020..

Leo nimeona isiwe kesi nikampeleka kituoni ili tuandikishiane,.hela yangu ataileta lini..nimeshukuru amekubali kuwa namdai..na ameandika tarehr ya kuleta pesa yangu..

akikiuka agizo inabidi alale ndani hata siku tatu tu ilia ashike adabu..

N:B ukitaka ubaya dai chako

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna kesi ya jinai/ polisi hapo.Hayo ni madai tupu....
hao askari waliokusaidia inabidi na wenyewe wawajibishwe kuingilia kesi ya madai. kwa kutumia mabavu...
ni askari wa kituo gani hao!!!
 
Unajua ukimkopesha mtu usimdai kwa ukali na ubabe nenda nae taratibu mpaka atalipa hyo naifanya mm sana taratibu kvp fanya hv;
1.kama uliyemkopesha anafanya biashara basi ni rahisi kukulipa,nenda kwenye biashara yake aidha duka au chochote nenda kwa upole na unyenyekevu wa hali ya juu usitake akulipe hela yote mfano unamdai 200,000 mwambie akupe hata 10000 ndani ya mwez hela yako itakuwa imeisha
2.kama anafanya biashara ya bidhaa au chakula au chochote...nenda ukachukua bidhaa au chakula chenye 5%ya pesa unayomdai lengo ni kupunguza deni..ukijifanya mjuaj hata hyo 5%hutopata
Mfano mm nilikuwa namdai muuza chips ana banda lake akasema anataka hela afanyie mtaj lkn amekwama nikampatia laki 2 ila kulipa ikawa mtihan nikaona isiwe tabu nikawa naenda kila ck kuchukua 5000 asiponipa nakula chips mayai na kuku nusu, ivo mpaka deni likaisha
Kwenda police sio sukuhisho maana akienda kule akikubali kuwa ni kwel unamdai basi jua umekwisha maana hata kama unamdai 1m atasema yeye uwezo wake kulipa ni 50k so ni bora uende nae taratibu ili angalau akulipe kidogo kidogo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi mambo ya kukopesha niliacha zamani sana kwa sababu ya watu kutokuwa waaminifu
Akija mtu namwambia sina za mkopo
Na kama ni wa karibu sana kwa mfano akitaka laki na shida ni yake nampa 20 bure zingine akajalize mbele
Ujinga huo sitaki kabisa
Yaani mtu anakuja kwa unyenyekevu sana ila mpe sasa kila siku ni ahadi tu



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Back
Top Bottom