Hati ya Kumkamata Rais Omar Al Bashir wa Sudan!

Buchanan

JF-Expert Member
May 19, 2009
13,199
1,969
Wapendwa wanaJF,
Nimeona ni vema nikaweka hii hati ya kumkamata Rais wa Sudan, Omar Al Bashir kujua ni mashtaka gani anayotuhumiwa nayo na Mahakama ya Jinai ya Kimataifa (The International Criminal Court) iliyoko The Hague kwa mujibu wa Sheria za Kimataifa na kama kuna justification yoyote yenye ushawishi ya kutolewa kwa hati hiyo. Fungua attachment hiyo hapo chini. Then tujadili.
 

Attachments

  • Warrant of Arrest of Omar Al Bashir.pdf
    358.2 KB · Views: 52
Mmm, hakuna mchangiaji? Learned bros and sisters!
 
Mheshimiwa, nashindwa hata nianzie wapi kwasababu rais wetu mpendwa ndiye rafiki yake mmoja wapo wa huyu al bashir na kikwete kwa mdomo wake alilaumu mataifa mengine kutokuwachukulia marais wa africa kihivyo....ni kitu cha ajabu dunia nzima inashangaaa. Turkey ambao ni islamic nation ilimwambia kuwa akitembelea uturuki watamkamata, lakini tz alikuja siku ile kwenye sulivan akakalishwa kwenye kiti pamoja na marais kama kawaida, hakukamatwa.

kwa kufupi, hii warrant ya arrest ni halali kabisa kwasababu al bashir amekuwa indirect perpetrator wa mauaji ya watu weusi kule sudan....na makosa ambayo sina wasiwasi nayo kuwa akikamatwa lazima ataswekwa ndani nayo ni CRIMES AGAINST HUMANITY AND WAR CRIMES....mwanzoni waliweka hadi GENOCIDE kwasababu ilionekana kama wale watu wanaouawa ni wa rangi moja na wengi wao ni kabila moja na kwasababu khartoum ni waarabu waliowengi, prosecutor alitazama kama kutakuwa na genocide..ikashindikana hivyo waka drop charge ya genocide zikabaki izo mbili ya war crimes and crimes against humanity.

kwanini ameshutumiwa na makosa hayo? ni kwasababu al bashir amekuwa akiwatumia kwa mlango wa nyuma (indirectly) janjaweed militias kuua watu halaiki, choma nyumba zao, baka na fanya vitendo vyote vya kiovu,...kuna ushaidi wa kutosha kuthibitisha hilo na yeye amekuwa akiwatumia janjaweek kama silaha ya kuwashambulia adversary wake....

sina uhakika, inawezekana genocide ilisharudishwa mwaka jana au mwaka huu kama sikosei, nitajaribu kusoma iyo doc uliyoweka na material zingine nione...na inawezakana kabisa kuna genocide pale..you know ili kuwe na genocide kunatakiwa kuwe ne proof kuwa the perpetrator intended to terminate/destroy in whole or in part an ethnic,racial, national...etc utasoma hii kwenye ICC STATUTE...ila kinachoangaliwa sana ni "intent to destroy a group" yaani ndo mens rea yake...na kuna ushaidi kuwa al bashir huwa anataka kuteketeza kizazi cha hawa watu weusi sana ili wabaki race ya waarab na machotara kama ilivyo kaskazini mwa sudan.....just kama Turkey walivyofanya kwa armenians, hitler alivyofanya kwa wayahudi, kule cambodia etc....nitakuja na argument za kisheria baadaye...kwasasa nilikuwa naongea kama layman...
 
ii mahakama ya kimataifa ni for africa au? mbona viongozi wanaokamatwa na case nyingi ni za africa tu! sisemi kua wahalifu wasishtakiwe lakini suala zima la double standard lazima liangaliwe! mbona viongozi wa nchi kama za amerika, ufilipino, mexico, colombia etc wanaongoza mauaji ya watu wasio na hatia well kama hawana hatia si wakathibitishe hilo mahakamani!
 
ii mahakama ya kimataifa ni for africa au? mbona viongozi wanaokamatwa na case nyingi ni za africa tu! sisemi kua wahalifu wasishtakiwe lakini suala zima la double standard lazima liangaliwe! mbona viongozi wa nchi kama za amerika, ufilipino, mexico, colombia etc wanaongoza mauaji ya watu wasio na hatia well kama hawana hatia si wakathibitishe hilo mahakamani!

Unafikiri Rais Omar Al Bashir amefanya uhalifu wowote wa kimataifa unaostahili yeye akamatwe? Na je, double standard inaondoa kosa la Omar Al Bashir kama lipo?
 
ii mahakama ya kimataifa ni for africa au? mbona viongozi wanaokamatwa na case nyingi ni za africa tu! sisemi kua wahalifu wasishtakiwe lakini suala zima la double standard lazima liangaliwe! mbona viongozi wa nchi kama za amerika, ufilipino, mexico, colombia etc wanaongoza mauaji ya watu wasio na hatia well kama hawana hatia si wakathibitishe hilo mahakamani!

ndugu yangu, cambodia kuna mahakama ya kimataifa hadi sasa hivi....ufilipino kuna mauaji gani yamefanyika?...elezea mauaji yaliyofanyika the philipines, nchi gani ya america imefanya mauaji elezea makosa yao kisheria hapa ndo utaeleweka ...kwasababu sometimes kitu unachofikiri wewe ni cha kisheria inawezekana sio kweli kama unavyofikiri,...mexico kuna mauaji gani...una uhakika wanaongoza kwa mauaji? ya namna gani?..hapa umeongea bila vithibitisho, anza upya,...jipange lete hapa makosa waliyofanya hao wengine halafu utaelezwa nini ICC statute inavyosema kisheria...usiongee kwa hisia, ongea kwa point.

pia...tushukuru Mungu kama ICC waafrica wengi wanakamatwa kwenda the hague, ni kwasababu hakuna sehemu zingine zenye uovu wa ajabu kama hapa...ukianza kuangalia congo kwa kina Lubanga, katanga na Ngudjoro walioko kule the hague, utaona kuwa walikuwa na makosa ya wazi kabisa ya kivita na crimes against humanity....ukiangalia Joseph kony wa Uganda anayekata watu midomo na mikono/miguu halafu anawaachia waende...choma nyumba zao na kuua etc..amefanya makosa mengi ya kivita na crimes against humanity, ukiangalia sudan kwa huyu janjaweed anayesaport janjaweed wenzie kuua watu weusi na hasa ambao ni wakristo...utaona international community haina sehemu nyingine mbaya kuliko Darfur...more than two million people dissplaced kwenye lile jangwa..na ndo maana nilisema genocide inaweza kurudishwa kwasababu hata kama hautauwa...ile kuwafanya watu waishi kwenye mazingira magumu jangwani ili wafe kwa starvation pia inahesabika kuwa genocide kama itagundulika kuwa ulikuwa na intention ya kutumia hiyo kama njia ya kuterminate that group of people...watu wanapata shida sana darfur kule..

ukiangalia nchi za ulaya magharibi...waliuana sana kule former Yugoslavia...lakini wanayo mahakama ya kwao ICTY iliyoko kule the hague inadili na mambo yao...na ICC imeanza tu hapa juzi miaka ya 2002 na hakujapatikana nchi zingine/bara lingine duniani linalokuwa na makosa yanayodondoka kwenye mahakama hii ila africa, ndio maana waafrica wengi wanajaa huko.

usiongelee ugaidi wa waarabu, huo haupo kwenye jurisdiction ya ICC.
 
ii mahakama ya kimataifa ni for africa au? mbona viongozi wanaokamatwa na case nyingi ni za africa tu! sisemi kua wahalifu wasishtakiwe lakini suala zima la double standard lazima liangaliwe! mbona viongozi wa nchi kama za amerika, ufilipino, mexico, colombia etc wanaongoza mauaji ya watu wasio na hatia well kama hawana hatia si wakathibitishe hilo mahakamani!
Mahakama hii imewahi kushughulikia kesi za nchi nyingi tu, hata Marekani ikiwemo. Hili limekuzwa sana kwamba Afrika inaonewa kwa sababu Mkuu wa Nchi anatakiwa akamatwe! Fungua link hii ili kuangalia kesi zilizowahi kupelekwa katika Mahakama ya Kimataifa tangu mwaka 1947!
 
Mahakama hii imewahi kushughulikia kesi za nchi nyingi tu, hata Marekani ikiwemo. Hili limekuzwa sana kwamba Afrika inaonewa kwa sababu Mkuu wa Nchi anatakiwa akamatwe! Fungua link hii ili kuangalia kesi zilizowahi kupelekwa katika Mahakama ya Kimataifa tangu mwaka 1947!

mkuu, tofautisha kati ya international court of Justice ambayo iko chini ya United Nations, na International Criminal court ambayo independent of the UN....International court of Justice deals with cases between nations, while international criminal court deals with individuals and not nations/states...the ICC started working in 2002 though the Rome agreement was entered in 1998, not all states signed this treaty, including sudan, that is why the prosecutor under the principle of complementarity was not capable of commencing investigation of the sudanese president until when the Security council sent the matter to him....under this Rome statute (ICC statute), if you are not signatory, the prosecutor needs to be referred a case by the Security council or any other nation signatory to it...the same happens in arrest, no country which is not signatory to the statute of the ICC can arrest al bashir unless they are parties to it...

under the ICC, you don't need consent of the perpetrator to be prosecuted by the court, while under the ICJ, you must obtain consent of the state to be prosecuted (the allerged state has to consent that Yes, i wanna be party to the case...kama nchi ikikataa kuwa party...the praintiff and accused thing...., then the icc haitaihukumu)...they are totally two different things....the ICJ ilianza muda mrefu na imehukumu kesi nyingi, wakati icj imeanza juzi tu..
 
Nashukuru Mwana wa Mungu kwa marekebisho hayo. Tuendelee kujadili!
 
Back
Top Bottom