Hatari - Tanzania listed among high risk countries for Ebola outbreak

Kwanza kabisa sijabagua, nimesema kuna watu humu hujiita Watz ilihali ni Wakongo, kwa mfano huyu mulisaaa aliwahi kudai kwamba yeye ni Mkongo nusu na Mtanzania nusu, nijuavyo sheria zenu haziruhusu uraia pacha, na kwa jinsi Kiswahili chake huwa majanga, hivyo atakua Mkongo.

Pili, nyie ndio wabaguzi mliojawa chuki mlizorithi kutoka kwenye mfumo wa ujamaa, muna hulka za kuwafukuza watu ambao mababu zao walizaliwa kwenu huko, kisa wana asili ya nchi zingine. Kuna yule jamaa mjaluo niliwahi kuleta habari zake humu, mumemtesa sana ilhali wazazi wake ni wazawa wa nchi yenu.

Anyways sijajua SANA suala la huyu jamaa.
Lkn mbona na NYIE mnamkana miguna miguna kisa eti anapingana na uhuru Kenyatta.
 
Anyways sijajua SANA suala la huyu jamaa.
Lkn mbona na NYIE mnamkana miguna miguna kisa eti anapingana na uhuru Kenyatta.

Sijui kwanini huwa mnajitoa ufahamu likija suala la Miguna na kulitumia kama kisingizio cha unyanyasaji wa hao raia wenu.
Miguna aliomba uraia wa Kanada wakati ambao hatukua tunaruhusu uraia pacha, hivyo moja kwa moja aliupoteza uraia wa Kenya.
Kwa njia rahisi labda utaelewa nikitumia mfano wa Tanzania, leo hii kuna yule mdada husababisha nchi yenu yote inataharuki, mapolisi wanajazana kwenye barabara zote wakikimbia kimbia, viongozi wenu wa CCM wanaongea na kutokwa mipovu balaa, anaitwa Mangi Kimambi na nina uhakika unamfahamu vizuri maana wewe ni mmoja waliokesha humu wakimfuatilia kwa povu.
Leo hii ikitokea huyo Mambi ameomba uraia wa Marekani, na kwa sababu nchi yenu hairuhusu uraia pacha, hivyo atapoteza uraia wa Tanzania, na siku akija mtamtolea nje. Hususan kama kipindi hiki amechokonoa uongozi wenu wote.

Ndivyo ilivyo kwa Miguna, alirudi Kenya na kupata stakabadhi kwa njia za mkato, lakini kwa vile hakua na vurugu dhidi ya serikali, wakaichukulia poa, lakini alipojifanya Mangi Kimambi wa Kenya, hapo ilibidi maafisa wa usalama na makachero kumfuata hatua kwa hatua, stakabadhi kwa stakabadhi.

Ni kawaida, ukitaka kupambana na dola au serikali yoyote ile, hakikisha mambo yako yote yamekaa ipasavyo maana watafukua makaburi. Kwenu huko niliona mahoteli ya Mbowe mnayayfuata. Pia Marekani ipo siku walimzushia uraia aliyekua rais wao bwana Obama.
 
Back
Top Bottom