MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,171
- 23,996
Nilikuwa ni mmoja wa Watanzania wakati wa kampeni ambao tulipenda wapiga kura wawachague wabunge wengi wa wapinzani ili wakaisimamie kikamilifu serikali ya Rais Magufuli kwa kujadili hoja kwa umakini wake, uzito wake na umuhimu wake kwa nchi.
Ni kweli wabunge wa kambi ya upinzani wameongeza mpaka kufikia zaidi ya 117 kwenye bunge lenye wabunge almost 380. Hata hivyo nimeanza kupatwa na wasiwasi kama idadi hii itakuwa imeongeza fikra mpya, pana na mbadala katika bunge la Tanzania.
Ninachokiona kwa sasa ni uwingi wa kambi ya upinzani kimwili badala ya uwingi wa fikra mpya na pana. Kwa mtu asiyeangalia masuala kwa makini anaweza akadhani kambi ya upinzani kwa sasa imeongeza nguvu kifikra lakini kiuhalisia imeongeza tu idadi ya wabunge kimwili ambao kuongezeka kwake hakuwezi kuzuia hoja na miswaada ya serikali kupitishwa na wabunge wa tiketi ya CCM.
Mikutano saba ya bunge imedhihirisha na kuonyesha kambi ya upinzani haiwezi kusimama kwa nguvu za hoja kamaTundu Lissu na Zitto Kabwe watakosekana bungeni!
Ni aibu kwa kambi ya upinzani kutegemea wabunge wawili katika kuisimamia serikali kwa makini hasa ikichukuliwa katika siasa za demokrasia ya vyama vingi ni wajibu wa kila mbunge wa chama kilichoko madarakani kuiwezesha Serikali ya chama chake kutekeleza majukumu yaliyoahidiwa katika ilani ya uchaguzi ikiwa ni pamoja na kutumia uwingi wao kuidhinisha maombi ya bajeti na kubadilisha sheria yanayoletwa bungeni na Serikali ili kuiwezesha nayo itimize ahadi zilizotolewa kwa wananchi kupitia Ilani ya Uchaguzi ya chama.
Inaeleweka kazi ya wabunge wa upinzani siyo kuisimamia serikali pekee bali pia kuidhoofisha katika macho ya wananchi ili wapate uwanja chanya wa kisiasa(political gain).
Kwa sasa wabunge wa upinzani zaidi ya 117 wanabebwa kihoja na wabunge wawili ambao wameonekana kuisimamia serikali kikamilifu. Mpaka sasa ni hoja za Tundu Lissu na Zitto Kabwe zinazoifanya serikali kurudi kwenye msingi wa utendaji kama zilivyo taratibu, kanuni na sheria za bunge/nchi.
Wabunge wengine wakisimama kutoa hoja wanachofanya ni kutoa viroja na vichekesho. Tumewaona wabunge wenye elimu za hapa na pale kama Saed Kubenea, hawezi hata kusoma kanuni mpaka apate msaada wa Tundu Lissu. Joseph Mbilinyi, anadai uwingi wa kura alizopata zaidi ya wabunge wote anatakiwa awe Waziri Mkuu. Jesca Kishoa akidhani bunge ni kijiwe cha kisiasa ambacho hakina kanuni na sheria, to name but a few.
Kwa ujumla, wabunge wengi wa upinzani wanatimiza namba na siyo fikra pana. Utegemezi wa wabunge wawili ni udhaifu mkubwa katika kambi ya upinzani na hatari kwa mapambano ya kutumia nguvu za hoja bungeni.
Kambi ya upinzani ijitathmini upya katika majukumu yake bungeni!
Nadhani hata Mbowe atakuwa ameliona hili tatizo ndio maana kwa sasa anafanya kila linalowezekana ili Zitto awe sehemu ya UKAWA!
Ni kweli wabunge wa kambi ya upinzani wameongeza mpaka kufikia zaidi ya 117 kwenye bunge lenye wabunge almost 380. Hata hivyo nimeanza kupatwa na wasiwasi kama idadi hii itakuwa imeongeza fikra mpya, pana na mbadala katika bunge la Tanzania.
Ninachokiona kwa sasa ni uwingi wa kambi ya upinzani kimwili badala ya uwingi wa fikra mpya na pana. Kwa mtu asiyeangalia masuala kwa makini anaweza akadhani kambi ya upinzani kwa sasa imeongeza nguvu kifikra lakini kiuhalisia imeongeza tu idadi ya wabunge kimwili ambao kuongezeka kwake hakuwezi kuzuia hoja na miswaada ya serikali kupitishwa na wabunge wa tiketi ya CCM.
Mikutano saba ya bunge imedhihirisha na kuonyesha kambi ya upinzani haiwezi kusimama kwa nguvu za hoja kamaTundu Lissu na Zitto Kabwe watakosekana bungeni!
Ni aibu kwa kambi ya upinzani kutegemea wabunge wawili katika kuisimamia serikali kwa makini hasa ikichukuliwa katika siasa za demokrasia ya vyama vingi ni wajibu wa kila mbunge wa chama kilichoko madarakani kuiwezesha Serikali ya chama chake kutekeleza majukumu yaliyoahidiwa katika ilani ya uchaguzi ikiwa ni pamoja na kutumia uwingi wao kuidhinisha maombi ya bajeti na kubadilisha sheria yanayoletwa bungeni na Serikali ili kuiwezesha nayo itimize ahadi zilizotolewa kwa wananchi kupitia Ilani ya Uchaguzi ya chama.
Inaeleweka kazi ya wabunge wa upinzani siyo kuisimamia serikali pekee bali pia kuidhoofisha katika macho ya wananchi ili wapate uwanja chanya wa kisiasa(political gain).
Kwa sasa wabunge wa upinzani zaidi ya 117 wanabebwa kihoja na wabunge wawili ambao wameonekana kuisimamia serikali kikamilifu. Mpaka sasa ni hoja za Tundu Lissu na Zitto Kabwe zinazoifanya serikali kurudi kwenye msingi wa utendaji kama zilivyo taratibu, kanuni na sheria za bunge/nchi.
Wabunge wengine wakisimama kutoa hoja wanachofanya ni kutoa viroja na vichekesho. Tumewaona wabunge wenye elimu za hapa na pale kama Saed Kubenea, hawezi hata kusoma kanuni mpaka apate msaada wa Tundu Lissu. Joseph Mbilinyi, anadai uwingi wa kura alizopata zaidi ya wabunge wote anatakiwa awe Waziri Mkuu. Jesca Kishoa akidhani bunge ni kijiwe cha kisiasa ambacho hakina kanuni na sheria, to name but a few.
Kwa ujumla, wabunge wengi wa upinzani wanatimiza namba na siyo fikra pana. Utegemezi wa wabunge wawili ni udhaifu mkubwa katika kambi ya upinzani na hatari kwa mapambano ya kutumia nguvu za hoja bungeni.
Kambi ya upinzani ijitathmini upya katika majukumu yake bungeni!
Nadhani hata Mbowe atakuwa ameliona hili tatizo ndio maana kwa sasa anafanya kila linalowezekana ili Zitto awe sehemu ya UKAWA!