Hata Nyie wanaume?

Hata Nyie wanaume?

vivian

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2009
Posts
1,749
Reaction score
1,002
[h=3][/h]
[h=3]KIJUE CHAMA CHA KUTETEA HAKI ZA WANAUME TANZANIA(TAMRA)[/h]





KATIBU WA UHAMASISHAJI WA TAMRA TAIFA BWANA HATIBU MGEJA AKIWA NA MWEKA HAZINA WA TAMRA TAIFA BWANA JUMA KOMBO

TANZANIA MEN’S RIGHTS ASSOCIATION
CHAMA CHA KUTETEA HAKI ZA WANAUME TANZANIA
”TAMRA”
Equal treatments for all
UTANGULIZI

TAMRA ni Asasi ya kiraia iliyoanzishwa na wanaume wa Tanzania kwa lengo la kutoa msaada wa Kisheria pamoja na Elimu ya Haki na Wajibu katika mahusiano ya kindoa kati ya mwanamke na mwanaume.

Kuanzishwa kwa asasi hii kumekuja katika kipindi hiki baada ya tafiti mbalimbali kuonyesha kuwa wapo wanaume wengi wanaofanyiwa vitendo vya ukatili katika masuala ya ndoa kwa kunyimwa haki zao za kindoa kutupiwa virago pindi mwanamke anapoamua kumchoka mwanamme kufuatana na kukosa kipato, kupungukiwa nguvu za kiume na mambo kama hayo , jambo ambalo limeonekana kuwa ni chanzo cha migogoro katika ndoa inayosababisha ongezeko la watoto wanaoishi bila wazazi wa pande zote mbili yaani [ Baba na Mama] huku hali hii ikiigharimu jamii na wanandoa kupigana na kusababisha majeraha na mauaji katika jamii.

Si hivyo tu Mwanamme wa Tanzania amekuwa ni mvumilivu kwa vile amekuwa akitendewa mambo yote haya bila kuwa na chombo cha kukemea vitendo hivi jambo lililotoa ushawishi kwa waanzilishi wa chama hiki kupata uchungu na hatimaye kuamua kuanzisha Asasi hii.

Muda mrefu mwanaume wa Tanzania hakupata wapi pa kwenda kupata msaada wa kisheria, imefika wakati wanaume kuwa na chama cha kuwatetea dhidi ya unyanyasaji kutoka kwa wake zao katika nyanja mbali mbali ikiwemo mambo ya ndoa,urithi wa mali kwa wagane, pamoja na ulezi wa watoto.

TAMRA kinaenda mbali katika kuelimisha wanaume juu ya haki zao za msingi pamoja na kuwaelimisha juu ya wajibu wao kama baba katika kuitunza familia yake,kuondoa mfumo dume na mfumo jike, kupiga vita unyanyasaji kwa mke na watoto,urithi wa mali kwa wajane na wagane pamoja na kulea watoto kabla na baada ya kufariki kwa wanandoa.

Jina la asasi: Asasi hii itajulikana kuwa ni Chama cha kutetea haki za wanaume Tanzania/Tanzania Men’s Rights Association kwa kifupi TAMRA
<>(1)<>(2)<>(3)TAFSIRI
“TAMRA” itamaanisha ni TANZANIA MEN’S RIGHTS ASSOCIATION.
KUTAKUWA NA VIONGOZI WAFUATAO WA TAMRA
<>·<>·<>·<>·<>·
KAZI ZA TAMRA.

TAMRA itakuwa na kazi zifuafuatazo:
<>(1)(2)(3)(4)(5)(6)(7)(8)(9)
MALENGO YA TAMRA.
TAMRA itakuwa na malengo kama ifuatavyo:-
<>(1)(2)(3)(4)(5)(6)(7)(8)(9)<>10<>11<>12Kutoa misaada kwa makundi ya wasiojiweza yatima, wazee,wagonjwa ,wakimbizi majeruhi wa ajari, majanga kama njaa,mafuriko, shule au kujenga majengo ya kutoa huduma za afya na elimu kulinda na kutunza mazingira kuangalia chaguzi ndani na nje ya Tanzania.

USIKOSE KUSIKILIZA KIPINDI MAALUM KATIKA RADIO NURU FM SIKU YA JUMAMOSI TAREHE 9 KITAKACHORUSHWA KUANZIA MIDA YA SAA 3.20 -4.00 USIKU TUTAKUWA NA MWANASHERIA WA TAMRA BW.BENY SHABAKAKI
WAWEZA SIKILIZA LIVE HAPA WWW.FRANCISGODWIN.BLOGSPOT.COM
 
Mh!
Huyo Katibu na Mweka Hazina wake mbona ni kama Wagane wote.
 
Waaoohh!
Hatimae saa ya ukombozi imefika! Tumepata chama! Washatunyanyasa kisana tu hawa binadamu!
Their days are numbered
 
kuna wanaume wananyanyasika sana we acha tu hasa walio oa makabila ya kaskazini huko
 
Hata wao wanamatatizo hayo, wapo wanaopigwa na wake zao....
sema ukubwa wa tatizo haujajulikana kwa sababu hawasemi, bila shaka sahivi tutajua kwakuwa wamepata chama....!!!
 
vivian
fathers4justice.jpg


fathers4life_1368438c.jpg


r-FATHERS-FOR-JUSTICE-DAVID-CAMERON-large570.jpg


20060926-manchester1.jpg


fathers-4-justice.jpg



 
kwi kwiiii kwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii .... mie ndukiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.

kama nawaona vile wanavyodai haki zao lol
 
hayaaa wale waliooa mabausa mwokozi huyooo na wale walioa askari sasa kuwekwa korokoroni bila sababu baaassiii

asante vivian
 
wanajihami na vipondo kutoka kwa wake zao,wanawake wamechoka naw days.hahaaaaa!raha kweli kweli,sasa hivi mwanamke ukimpiga ngumi anakupa teke la mbavu na ngumi za kutosha,acha wajihami,wanawake na maendeleo,maji yamewafika shingoni huhuhuuuuu!
 
Haa! Jamani!
Taasisi ya ndoa karibu itakuwa janga la kitaifa!
 
Hata mashoga si wanamme?
Wananyimwa haki yao ya kuolewa.

DUnia imevaa bukta inatrot, kazi ipo
 
Hata mashoga si wanamme?
Wananyimwa haki yao ya kuolewa.

DUnia imevaa bukta inatrot, kazi ipo
Kongosho Mpenzi acha kabisa hadithi za mashoga.

Hebu niambie tu. kwa maoni yako binafsi what is the motive behind this Organization formation?

Ninachojua Kenya wanaume ndio wananyanyaswa na wake zao. Lakini hapa Tanzania uniambie mwanaume wa kikuria anadai haki yake kijinsia utakua umenidanganya.

Hivi wakati wakuanzisha hivi vyama wahusika hauwaulizwi sababu ya kuvianzisha na mifano hai ya msukumo uliowafanya waanzishe vyama hivi?

I miss Bebii
 
Last edited by a moderator:
Walichelewa kwani kama kunyanyaswa ilianza zamani. Ushauri hakikisha unapooa unaangalia size na strengh na sio uzuri, wengine kama dume vile.
 
vivian@nimeshindwa hata kuchangia kwa uzuri ulionao natamani uwe kama unavyoonekana kwenye avatar yako.
 
Haya tumekiona chama cha kututetea ngoja tukachukue kadi
 
Back
Top Bottom