Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Amani iwe kwenu.
Hata Chavda, Valambia na Rostam siku wakiamua kugombea uraisi kupitia CHADEMA watatetewa na washikilia ukuta!
Kuna msemo wa Kiswahili husema ‘’tabia haina dawa’’.Nahii ndio hasa inadhihirisha miongoni mwa viongozi na wanachama wa CHADEMA chini ya Mbowe.kwa wale wenye kumbukumbu ya siasa za Tanzania watawakumbuka Valambia,Chavda na Rostam katika harakati zao kibiashara ambazo kwa kiasi kikubwa zililiingiza taifa hasara kubwa. Kwa Tabia ya CHADEMA Chavda, Valambia na Rostam siku wakitoa fedha kwa dhumuni la kukodi chama ili kugombea Uraisi hakutakuwa na pingamizi. Nina sababu lukuki kuthibitisha hoja yangu;
Mbowe na wenzake ni waongo na huenda wanamiliki kiwanda cha uongo.
Mara kwa mara wamekuwa wakielezea wananchi kuwa wao wanachukia ufisadi na mafisadi kiasi cha kuwaorodhesha kwenye tovuti ya chama kinyume chake kumbe Mbowe huwa na mawasiliano ya karibu na mafisadi hao huku akiingia makubaliano nao kwa malipo kukiwa na ahadi ya kuwauzia nafasi za kugombea uongozi ndani ya chama. Kimsingi CHADEMA wanamchafua mtu ili awalipe pesa,ni walaghai kwa wananchi hawamaanishi wanalolisema.
Umasikini, udhaifu na ujinga wa Bavicha.
Mbowe na genge lake wanatumia umasikini, udhaifu na ujinga wa vijana wa CHADEMA kupitisha ajenda zao. BAVICHA wamegeuzwa’’ mbwa koko’’ leo wanaambiwa wamtukane Lowassa kasha wanaambiwa msifieni. Vijana wengi wanatumika sababu ya kutotaka kufanya kazi za kujitafutia kipato. Wamedanganywa kuwa nchi hii kuwa wezi hao wakishinda uraisi watawapa ajira na huduma bure za afya elimu nk. Kwa kuweka rehani vitalu vya gesi. Utasikia wakisema ‘’ Lowassa akishinda shule bure kwa watoto wetu chekechea hadi chuo kikuu’’, waliokuwa wakulima, biashara, kazi nk wameacha na kusuburi muujiza wa Lowassa na kundi lake ambalo kwa muda mrefu waliwatuhumu kuiba rasilimali na kuwatia umasikini. BAVICHA imejaza vijana waanoridhika kwa malipo ya kuwasifia viongozi na wabunge washikilia ukuta kwenye ‘’FB wall’’ zao na wanafurahia kwa hiyo siku Mbowe akiwapa malekezo ya kumsifia Chavda, Valambia au Rostam tutashuhudia ngonjera na mashairi matamu ya kuwasafisha. Ukitaka BAVICHA wakusafishe mlipe Mbowe na ukitaka wakutukane mnyime hela.
Itikadi ya CHADEMA chini ya Mbowe ni pesa na sio siasa safi.
Kwa sasa nafasi za uongozi CHADEMA zitagawiwa kwa wenye fedha, wanaoweza kulipa uongozi na sio wenye itikadi ya kutoa huduma kwa wananchi kupitia siasa. BAVICHA hawawezi kukemea uozo ambao unasababishwa na rushwa inayomea ndani ya chama ambayo kimsingi inaziba fursa ya wao kuwa viongozi baadaye sababu ya matumizi ya pesa kuwanzisha kampeni zisizo na kichwa wala miguu. Mbowe na wenzake walipongundua tu vijana watahoji kuhusu mpango wa maendeleo ya chama kaja na kampeneni ya kushikilia ukuta kwa nia ya kuwafumba wasione yanayotendeka nyuma yao. Kalagabaho!!! Wajinga ndio waliwao!
CHADEMA wanapenda sana siasa za ramli na miujiza.
Huu ni udhaifu ambao umewajaa viongozi na wanachama wa CHADEMA, ikitokea mtu akaleta propaganda ya uongo kama Lowassa alivyowadanganya kuwa yeye ni kila kitu wamwachie mipango yote ya kura za uraisi, kwa sababu akili zao zimegeukia ukuta hawakuangalia nyuma woote wakamwamini, na alivyoshindwa uchaguzi amewaamuru washike ukuta wasielewe linaloendelea anawadanganya kaibiwa kura angali alijitapa yeye ndiye nguli wa wizi wa kura za uraisi. Hivyo kwa mwanasiasa mwenye mbinu za kuajiri ‘’waganga’’ na ‘’manabii’’ maarufu watoe ujumbe kuwa miungu yao imesema wao ndio wameitwa kuwa raisi vijana walizungusha mikono kama ishara ya mabadiliko lakini kwa hili agizo walilopewa kushikilia ukuta viungo pekee watakavyoweza kuzungusha/kukatika ni kiuno na shingo…hivyo tutarajie BAVICHA wakiambiwa na kina Valambia….ukutaaaaa….wao wanaitikia wataitikia huku wamenyoosha mikono mbele mithili ya kibinda nkoi….huku wakizungusha kichwa/shingo na viuno…hizi ndio hathari za kushikilia ukuta.
Kibwagizo cha kufikirisha.
‘’Akili za Mbowe mshikiliaUKUTA zimegonga UKUTA, mwisho wa kufikiri….bila maono CHADEMA UKUTA wamegonga UKUTA hawajui pa kwenda wamebaki kushika UKUTA, Lowassa mshikilia UKUTA kawawekea UKUTA wasijue linaloendelea, wakati UKUTA!.Wabunge washikilia UKUTA wana njaa ya posho wameanza kubomoa UKUTA
‘Siasa ni sayansi’ Dr.Slaa (1.9.2015)
Nawasilisha.
Hata Chavda, Valambia na Rostam siku wakiamua kugombea uraisi kupitia CHADEMA watatetewa na washikilia ukuta!
Kuna msemo wa Kiswahili husema ‘’tabia haina dawa’’.Nahii ndio hasa inadhihirisha miongoni mwa viongozi na wanachama wa CHADEMA chini ya Mbowe.kwa wale wenye kumbukumbu ya siasa za Tanzania watawakumbuka Valambia,Chavda na Rostam katika harakati zao kibiashara ambazo kwa kiasi kikubwa zililiingiza taifa hasara kubwa. Kwa Tabia ya CHADEMA Chavda, Valambia na Rostam siku wakitoa fedha kwa dhumuni la kukodi chama ili kugombea Uraisi hakutakuwa na pingamizi. Nina sababu lukuki kuthibitisha hoja yangu;
Mbowe na wenzake ni waongo na huenda wanamiliki kiwanda cha uongo.
Mara kwa mara wamekuwa wakielezea wananchi kuwa wao wanachukia ufisadi na mafisadi kiasi cha kuwaorodhesha kwenye tovuti ya chama kinyume chake kumbe Mbowe huwa na mawasiliano ya karibu na mafisadi hao huku akiingia makubaliano nao kwa malipo kukiwa na ahadi ya kuwauzia nafasi za kugombea uongozi ndani ya chama. Kimsingi CHADEMA wanamchafua mtu ili awalipe pesa,ni walaghai kwa wananchi hawamaanishi wanalolisema.
Umasikini, udhaifu na ujinga wa Bavicha.
Mbowe na genge lake wanatumia umasikini, udhaifu na ujinga wa vijana wa CHADEMA kupitisha ajenda zao. BAVICHA wamegeuzwa’’ mbwa koko’’ leo wanaambiwa wamtukane Lowassa kasha wanaambiwa msifieni. Vijana wengi wanatumika sababu ya kutotaka kufanya kazi za kujitafutia kipato. Wamedanganywa kuwa nchi hii kuwa wezi hao wakishinda uraisi watawapa ajira na huduma bure za afya elimu nk. Kwa kuweka rehani vitalu vya gesi. Utasikia wakisema ‘’ Lowassa akishinda shule bure kwa watoto wetu chekechea hadi chuo kikuu’’, waliokuwa wakulima, biashara, kazi nk wameacha na kusuburi muujiza wa Lowassa na kundi lake ambalo kwa muda mrefu waliwatuhumu kuiba rasilimali na kuwatia umasikini. BAVICHA imejaza vijana waanoridhika kwa malipo ya kuwasifia viongozi na wabunge washikilia ukuta kwenye ‘’FB wall’’ zao na wanafurahia kwa hiyo siku Mbowe akiwapa malekezo ya kumsifia Chavda, Valambia au Rostam tutashuhudia ngonjera na mashairi matamu ya kuwasafisha. Ukitaka BAVICHA wakusafishe mlipe Mbowe na ukitaka wakutukane mnyime hela.
Itikadi ya CHADEMA chini ya Mbowe ni pesa na sio siasa safi.
Kwa sasa nafasi za uongozi CHADEMA zitagawiwa kwa wenye fedha, wanaoweza kulipa uongozi na sio wenye itikadi ya kutoa huduma kwa wananchi kupitia siasa. BAVICHA hawawezi kukemea uozo ambao unasababishwa na rushwa inayomea ndani ya chama ambayo kimsingi inaziba fursa ya wao kuwa viongozi baadaye sababu ya matumizi ya pesa kuwanzisha kampeni zisizo na kichwa wala miguu. Mbowe na wenzake walipongundua tu vijana watahoji kuhusu mpango wa maendeleo ya chama kaja na kampeneni ya kushikilia ukuta kwa nia ya kuwafumba wasione yanayotendeka nyuma yao. Kalagabaho!!! Wajinga ndio waliwao!
CHADEMA wanapenda sana siasa za ramli na miujiza.
Huu ni udhaifu ambao umewajaa viongozi na wanachama wa CHADEMA, ikitokea mtu akaleta propaganda ya uongo kama Lowassa alivyowadanganya kuwa yeye ni kila kitu wamwachie mipango yote ya kura za uraisi, kwa sababu akili zao zimegeukia ukuta hawakuangalia nyuma woote wakamwamini, na alivyoshindwa uchaguzi amewaamuru washike ukuta wasielewe linaloendelea anawadanganya kaibiwa kura angali alijitapa yeye ndiye nguli wa wizi wa kura za uraisi. Hivyo kwa mwanasiasa mwenye mbinu za kuajiri ‘’waganga’’ na ‘’manabii’’ maarufu watoe ujumbe kuwa miungu yao imesema wao ndio wameitwa kuwa raisi vijana walizungusha mikono kama ishara ya mabadiliko lakini kwa hili agizo walilopewa kushikilia ukuta viungo pekee watakavyoweza kuzungusha/kukatika ni kiuno na shingo…hivyo tutarajie BAVICHA wakiambiwa na kina Valambia….ukutaaaaa….wao wanaitikia wataitikia huku wamenyoosha mikono mbele mithili ya kibinda nkoi….huku wakizungusha kichwa/shingo na viuno…hizi ndio hathari za kushikilia ukuta.
Kibwagizo cha kufikirisha.
‘’Akili za Mbowe mshikiliaUKUTA zimegonga UKUTA, mwisho wa kufikiri….bila maono CHADEMA UKUTA wamegonga UKUTA hawajui pa kwenda wamebaki kushika UKUTA, Lowassa mshikilia UKUTA kawawekea UKUTA wasijue linaloendelea, wakati UKUTA!.Wabunge washikilia UKUTA wana njaa ya posho wameanza kubomoa UKUTA
‘Siasa ni sayansi’ Dr.Slaa (1.9.2015)
Nawasilisha.