Hata CHADEMA ni porojo tu...

Hata CHADEMA ni porojo tu...

hamna pesa? Mmh hayo mabakuli ya jerojero za watz anakula nani mkuu? Mleta mada kasema kama mna uwezo wa kushawishi watu wakaandamana na kufanya vurugu.. Mtashindwaje kuwashawishi wachangie mjenge hata kadarasa kamoja.
nani kasema hii nchi haina madarasa,madarasa kajenga lowasa kibao lakini hayana faida tunataka tupate fursa ya moja kwa moja kuwaonesha watu kwamba tunaweza basi.tunataka tuwaoneshe jinsi ya kuwajaza walimu kwenye hayo madarasa.all in all ccm inanuka mavi.ila sisemi kama cdm ni chama kizuri sana maana hakijawahi kutawala bado lakini kwa hali ilivyo sasa tuwape nafasi ili tujijengee utaratibu wa kuondoa uozo na sio kulalama tu.tukishajijengea uwezo wa kubadili hata cdm au chama chochote kikiharibu tunatupa kule tunaweka kingine tofauti na ilivyo sasa.kife chama cha mapinduzi."wanaoipenda tanzania itikieni kwa sauti kuu kifeeeeeee"mnaonufaika na sembe kaa kimya
 
Hii nchi haitakombolewa kutoka kwa hawa wakoloni kama tutaendelea kuwa na watu wenyemawazo kama haya!
 
In fact hata kama hujahama wewe ni mamluki na unajadili watu/chama badala ya hoja. tunaelewa kuwa kadi sio kigezo kwani wengi wenye hizo ni wanachama wafu. Bora uwe mfu ubaki kimya kuliko kutokota na kubwabwaja. tafuta ajira ujipatie kipato cha kukusitiri badala ya kutumiwa kaama hivi. Porojo unazo wewe kwani unashindwa kuangalia upande wa pili. Tatizo tunalolipata humu jf ni kuchanganyika na wachangiaji wenye upeo mdogo mno. Nadhani ndio maana agenda ya nchi yoyote inakuwa kutoa elimu bora iuli tuepukane na vishoka hata kwa mambo yanahitaji uelewa mdogo. Elimu ya shule za kata ndio tatizo kubwa sasa hivi. Unaweza kumlinganisha mtu ambaye hajashika dola kwa kubwabwaja tu. Kachuke buku zako mbili au tatu uwahi kongoro ili uweze kuripoti kwa waajiriwa wako kesho. Baragumu limepigwa watu wanahitaji mabadiliko ya kweli. Rekodi ndogo tu mmeiona: Wabunge 48 wa CDM wanawatoa jasho mkusanyiko wa wabunge mia3 na ushee kwenye hoja. Hatima yenu iko kwa wananchi, mwenye macho haambiwi tazama.
 
Alafu serikali ifanye kazi gani CHADEMA kama chama cha upinzani kazi yake ni kuisukuma serikali kutekeleza ilani yake,CHADEMA hawakusanyi kodi,kama CCM wameshindwa ku-deliver wakae pembeni alafu tuone kama CHADEMA hawatatekeleza hayo yote unayoyasema

Yaani CHADEMA wajenge hospital kwa hizi mia mbili wakati CCM wanakula kodi yetu na hawafanyi chochote!!

Tujadili vitu vya maana tuache masikhara


Hawafanyi chochote! sio kweli
Na magari yanayotumia 400,000 per day kuliendesha?
Na marupurupu yote hayo!
Na semina hewa katika halmashauri!
Na safari hewa za wakuu wa serikali!
Hayo yote ni kodi ya wananchi!

Labda usemi hawanufaiki wachonge!
Na tangu lini mwenye shibe akamjua mwenye njaa?
 
Nataka kumsaidia huyu mtoa mada nafikiri ana matatizo ambayo wengi wanayo walioko nje ya hivi vyama ila ni wapiga kura kwa kutumia mantiki na siyo upofu na upenzi wa vyama...

CDM inasema mengi kuhusu maendeleo ya taifa hili, lakini haya yote yanahitaji kukuza wigo la kodi achana tu na ufanisi wa kukusanya hii iliyopo. CDM wenyewe wataongezaje Pato la taifa ukitoa kupuguza ufisadi na other inefficiencies za CCM (ambazo sawa zitaokoa upotevu lakini hazitaongeza hilo pato kwa kiasi hiko wanachofikiri CDM kuweza kuleta hayo mageuzi ya kiuchumi)...

je CDM watabinafsisha sekta ya madini huku mikataba ikilindwa na sheria za kimtaifa?
je CDM watapunguza kodi ya PAYE ili kustimulate spending tuwe kama marekani consumer driven economy?
je CDM watawekeza kwenye viwanda au kilimo na pesa za uwekezaji huu zitatoka ndani (kwa source gani kama kodi haitotosha) au mikopo (kama deni letu la nje halitalipuka na kutoa faida yeyote ya uwekezaji huu)
je tufuate indiginazation policies kama za mugabe kuweka uchumi ndani ya mikono ya watz na kuokoa capital flight?

Kwa kifupi propaganda majukwaani hazijibu haya maswali na ukiangalia safu ya uongozi CDM uzalendo peke yake bila uzoefu na maarifa binafsi(achana na washauri wa ndani na nje watakaopewa ajira CDM ikiingia madarakani) inaleta mashaka zaidi na maswali zaidi...tutaendeleaje kiuchumi na njia ipi tutumie CDM hawawi specific kwenye haya
 
Utangulizi.
Bado nina kadi ya CHADEMA,

Maada
Naipenda hii nchi kuliko Vyama na siasa zake, Kabla ya mifumo ya vyama Tanzania ilikua na wakazi na waliishi kwa taratibu na misingi yaliyojipangia wakati huo.

CCM wameshindwa kuwawezesha watanzania kupata hata yale mahitaji muhimu (food, cloth, and shalter), ni masikitiko makubwa sana.Wameiba kila kinachoibika na kutuachia MAPANKI. Miaka Hamsini ya utawala wao (huku wakibadili majina ya CHAMA kama ile hoteli maarufu ya jijini DAR "SERENA") Imekua ya machozi jasho na damu.ANYWAY Mungu yupo na sote tunaamini hivyo.

Tatizo langu ni CHADEMA, huu ukombozi tunaohubiri tena tukimuingiza muumba "TUMEANZA NA MUNGU, TUTAMALIZA NA MUNGU" unamashaka makubwa sana.Leo kama IKIRUHUSIWA TAASISI ZA DINI KUSIMAMISHA WAGOMBEA kisiasa Kanisa Katoliki litaibuka mshindi bila shaka. Wamejenga MASHULE, HOSPITALI, VYUO VIKUU, VYUO VYA UFUNDI, HOSTELI, tena vijijini kwa wale waliosahaulika na kadhalika. Simaanishi taasisi nyingine hazijatoa huduma hizi la! ila kanisa hili linaongoza toka enzi hizo.

Kinachonitoa JASHO ni jinsi gani niitofautishe CHADEMA na CCM, Kwani maneno wanayoyatumia sasa hata MAFISADI wa CCM huyatumia wanapoomba kura.Je hizi lugha tamu tamu za ukombozi ntajuaje kua hazitageuka kuwa shubili kama sioni mifano thabiti sasa. Kila kukicha Chadema tunachangishana eti kughalimia uendeshaji wa chama (KWELI!!!!). Kama nia ni ukombozi kwa nini tusianze sasa kutumia michango na ruzuku kujenga hata dispensary vijijini, kununua madawati, kulipia karo watoto wa maskini, kuamasisha watu kujitolea kujenga miundombinu vijijini na nk..

Hatuwezi kujitofautisha na CCM kwa sela za midomoni na kwenye vitabu tu..Tuanze utekelezaji kwa kile kidogo tulichonacho KAMA TAASISI ZA KIDINI ZIFANYAVYO VILE...Kama tunaweza kuhamasisha watu kuunga mkono maandamano yetu (ambayo yana tija pia) tuhamasishe pia wakusanyike na kufyatua matofali ili kujenga dispensary vijijini..Mambo ya HELKOPTA ni anasa kubwa sana kwa mkurya wa kibhancha bhancha, au msukuma wa SAYUSAYU. tunahubili ukombozi wa maskini kwa display ya anasa..Kuna ulazima gani kutumia helkopta katika mikutano ya kawaida kabisa??

Ni muda wa kujitofautisha na CCM kwa Vitendo na si maneno na sela, la sivyo itakuwa ni POROJO tu za kutaka madaraka then BUSINESS AS USUAL. (Mungu kakupa akili na maarifa bure, kuvitumia ni hiari yako)

Hitimisho

Sijahama chama.

Kama ambavyo wewe umestuka mimi pia nilistuka pale wabunge wa CDM waliposhindwa kusamehe posho ya kukaa na wakaanza kushindana wenyewe kwa wenyewe "tuchukue ama tusichuke" aidha Mwenyekiti wa Kamabi ya upinzania bungeni akarejesha Shsngingi la Serikali alilopatiwa kwa matumizi yake lakini nasikia akaende kulichukua kimya kimya
 
unaweza kutuambia mpaka shule moja ya sekondari inakamilika waumini wa eneohusika wanakuwa wamechangishana mara ngapi? Na kwa maana hiyo hiyo cdm kwa mchango wa mara moja wanaweza kujenga shule kwa kila eneo wanalopita?

Takribani wagombea wote wa CDM walipokuwa wakiomba kura waliahidi kuwa karibu na wananchi na kuwahamassha wachangie maendeleo, ni wangapi wapo karibu na wananchi? kama sio kila siku kuzua sababu yza kutumbua ruzuku kwa maandamnao na mikutano isiyoisha badala ya kuwa karibu na waliowapigia kura 2010. Hilo nalo linahitaji kuwa madarakani/
 
Takribani wagombea wote wa CDM walipokuwa wakiomba kura waliahidi kuwa karibu na wananchi na kuwahamassha wachangie maendeleo, ni wangapi wapo karibu na wananchi? kama sio kila siku kuzua sababu yza kutumbua ruzuku kwa maandamnao na mikutano isiyoisha badala ya kuwa karibu na waliowapigia kura 2010. Hilo nalo linahitaji kuwa madarakani/

kwahiyo mkuu, hayo maelezo ndiyo yamejibu nichohoji hapa chini? ndiyo maana wengi hufeli mitihani hebu soma tena hapa chini ulinganishe na ulichojibu hapo juu....

quote_icon.png
By adolay
unaweza kutuambia mpaka shule moja ya sekondari inakamilika waumini wa eneohusika wanakuwa wamechangishana mara ngapi? Na kwa maana hiyo hiyo cdm kwa mchango wa mara moja wanaweza kujenga shule kwa kila eneo wanalopita?
 
Back
Top Bottom