sijutii kumpa kura yangu Hashim rungwe, kwanza hana njaa kama wajinga wengi wasiomjua wanavyomzania, pili ni msomi na tajiri pia anajua kabisa nini anafanya, ila ninachosikitika tunaishi katika jamii ya hovyo kabisa, mahaba niuwe ya vyama na wagombea ndio yanatugarimu mpaka sasa.......
rungwe kaongea facts na reasoning yake ipo juu sana kaongea ukweli uliotukuka na si masikhara...
swala la reli bado ni utata mtupu, hadi zuma anaombwa akatusaidie kupata mkopo? kumbe kelele nyingi na mashauzi ya hapa na pale halafu hela zenyewe hazipo, watu wanashindwa kuelewa kua Zuma hana nguvu na ushawishi mkubwa kiasi hicho kama viongozi wanavyojiaminisha tayari huko kwao yupo kwenye matatizo makubwa ndani ya chama chake.......
tujiongeze hapa kuna uwezekano mkubwa hizi ndoto za alinacha zisitimie.... tuombe uhai tutashuhudia mengi.
viawanda bila malighafi? utaendelezaje viwanda bila kua na big plantations? kilimo cha kutegemea mvua? ndoto zingine bana daaah, ngoja niishie hapa nisijeitwa mchochezi maana milion 7 parefu usawa huu.