Hasheem thabeet anatatizo gani kukaa bench (houston rokects)- nba

Hasheem ana muda mwingi wa kufanya vizuri, walipomchukua walijua kuwa ni long term project. Sasa hivi Rockets wanacheza vizuri so hawawezi kumpa Thabeet muda na kuvuruga timu ili dogo apate experience. Kwa kifupi unless aumie au awe na nidhamu mbaya sana (hakuna habari yoyote ya kukosa nidhamu) Thabeet atakuwa NBA kwa miaka mingi ijayo, kwasababu ya urefu tu.



Mkuu kumbuka huyu dogo wetu ana umri mdogo sana na anatakiwa kujituma katika hiyo age aliyo nayo wenzake waliingia wakiwa na age ndogo kuliko hiyo yeye anachopaswa ni kufanya workouts sana na sio mchezo sasa tatizo lake wakati wa mapumziko dogo anakuja Dar kula raha wakati wenzake wanajifua, check hao ma super star kama Lebron James ukiangalia jitu liko huko juu lakini workouts zake usipime sasa dogo wetu yeye ameridhika nini sasa hakuna wa kumshauriiiii watu wanajiuliza ni kulikoni au hana hama na hiyo game kajilazimisha au?



HT sasa ana miaka 25. Angalia Blake Griffin ana miaka 23; Kevin Durant ana miaka 24; Serge Ibaka ana miaka 23; Derrick Rose ana miaka 24; James Harden ana miaka 23; Brandon Jennings ana miaka 23; O.J Mayo ana miaka 25 (tena huyu alikua nae Grizzlies).
Hawa ni baadhi ya wachezaji vijana wanaotamba vibaya mno NBA.

Sasa kusema HT bado ni mdogo sana na muda mwingi, mnakua mnakosea. Lebron tayari ana miaka 28, na hao vijana hapo juu wanatishia utambaji wake; sasa kwa mtizamo huu, HT akiendelea kuwa katika kiwango alicho sasa, hakika hana muda mwingi ataondoka NBA.
 
Wajua ni wachezaji wangapi wa Africa wako NBA na wote wana piga kila Game wachezayo ni huyo Hasheem wako unae mtetea ana vigezo vyote vya kuwa 1st 5 line up ya timu yake ila dogo mzembe wewe NBA ni workouts zako mfano mzuri ni Serge Ibaka (Mtoto wa Congo-Kinshasa) anachezea Oklahoma City all stars ya mwaka jana alikuwepo kwa Dunk Competition na aliingia na bendela ya Congo, Luol Deng yuko Chicago Bulls katoka Sudan uliza kafanya mambo gani sudani ujue, mbali na hao kuna msenagal yuko High School USA, NBA wamesema anastahili kucheza NBA na sio huko High School leo hiii unadiliku msifu Hasheem kwa mauuvivu khaaa ivi unaujua huu mchezo kweli au unaongea penye ukweli tunasema tuuu dogo anapoteza muda wake huko tuuu ukiwa NBa ni kupambana na sio kwenda kuosha na ndio mawazo ya kwetu watanzania kupe kuishi pila kuhangaikia maisha , Na ndio maana nika toa mfano kwa Jeremy Lini ameanza last 2 week on Monday kwa 28pts na 8 asst na mpaka sasa ndani ya week mbili Jeremy Lin ana Points 109pst in First 4 start (Most In NBA since Merger) na Knicks won last 5 games toka Lin ameanza hebu jiulize Haseem toka ameingia kaweka record gani na he was the 2nd pick Overall in NBA 2009 ivi unajua maana ya 2nd Pick in NBA au unadhani ni mpira wa TFF,SIMBA ,YANGA,VODACOM huu???


Kweli Luol Deng ana asili ya Sudan, lakini sasa ni raia wa Uingereza. Hivyo ni muingereza; hata NBA anatambulika kama muingereza.
 
Kila binaadam ana kikomo chake, mlitaka kila mmoja awe kama Jordan au Kobe?

Alipofika Hasheem hakuna Mtanzania aliyewahi hata kunusa, kaweka historia kwa Tanzania anastahili kila pongezi. Kuwepo tu benchi la NBA si mchezo. Kuwepo NBA ni ndoto ya karibu kila mtoto wa kimerekani na Basket ni mmoja katika michezo inayopendwa sana US, seuse kuwa ni ndoto ya wengi duniani.

Hasheem, apongezwe alipofikia na kwa huu mchezo ulivyo, it takes only 5 minutes za kucheza na move moja tu ya maana kubadili muonekano. Tumuombee kila la kheri.
haumtakii mema.....hata yeye akihojiwa anasema anataka siku moja awe kama KB24.......hiyo ya ku aim low anayo raisi wako kikwete tu......labda uniambie kafata kwake.......

alipohojiwa na bongo celebrity
BC: When you hear success stories of African born athletes like Dikembe Mutombo,Hakeem Olajuwan, Ashton Youboty, Luol Deng and many more others making it to the highest level of competition in North America from very humble beginning, what does that mean to you?

HT: It actually means a lot to me. These guys have opened a way for us. All we have to do is follow their footsteps. I am actually a good friend to most of them. For example I work out a lot with Emeka Okafor. He mentors and gives me a lot of good advices something which I believe is important for any aspiring professional athlete like myself. As you must have heard, he just signed a $72 Million contract with BobCats. So its just a great example to me.

Sasa wewe unasem anini hapa???? dogo aache uvivu na kulewa sifa za watu kama wewe ambao kila akina anawapa ofa ya viingilio bilicanas.......
 
Kila binaadam ana kikomo chake, mlitaka kila mmoja awe kama Jordan au Kobe?

Alipofika Hasheem hakuna Mtanzania aliyewahi hata kunusa, kaweka historia kwa Tanzania anastahili kila pongezi. Kuwepo tu benchi la NBA si mchezo. Kuwepo NBA ni ndoto ya karibu kila mtoto wa kimerekani na Basket ni mmoja katika michezo inayopendwa sana US, seuse kuwa ni ndoto ya wengi duniani.

Hasheem, apongezwe alipofikia na kwa huu mchezo ulivyo, it takes only 5 minutes za kucheza na move moja tu ya maana kubadili muonekano. Tumuombee kila la kheri.

kwahiyo ye kafikia kikomo bila kuanza?! hebu mcheki m-taiwan Lin,angalia akina Hayden.................hili toto linajua kuhonga machangu wa Bills tu...mbav!aibu sana kupata nafasi kama ile then you throw it away..potential ipo/iloikuwepo ar else asingechaguliwa as a second overall pick.shame!
 
Kipaji ni kitu huwezi lazimisha na kina ukomo wake pia ingawa pia uzembe unaweza ukaathiri kipaji.
Kwa HT sina hakika kama ukomo wake umefikia pale au anafanya uzembe kama wengi wetu tunavyo amini
Kimsingi NBA inawachezaji wengi sana na ushindani ni mkubwa kuliko maelezo na wanofanikiwa kung'ara ni wachache kuliko ambao wapo wapo NBA wakitegemewa kuonyesha kile wanachoaminiwa kuwa wanacho
SItaki wala sipendi kumuhuku HT kwa kutofikia kiwango cha juu kabisa cha kuweza kucheza games za kutosha wala si haki sana kumlinganisha na fulani sababu tunatofautiana uwezo
Cha msingi dogo akomae na nina. amini HT hajaridhika kama tunavyo dhani amepigana hadi kuingia NBA na sasa anapigana kupata namba, kama kuna Kobe alifanikiwa wiki moja its ok lakini wapo waliofanikiwa baada ya miaka hata 10 wakiwa bench NBA
Changamoto tumpeni lakini kejeli hazijengi, kudhani tu kuchaguliwa NBA ndio umemaliza kazi ni kujidanganya kuna ushindani pale jamani acheni utani, tumuombeeni kila la kheri dogo avuke mtihani huu maana kuna wengi sana wanaishi hapo pia

mkuu,sitaraji HT afanane kiwango na KD au Tyson Chandler wa nafasi kama yake.anachosikitisha wengi ni wkamba dogo anashindwa kufikia hata robo ya ile potential aliyonayo kaka,halafu ni kwa uzembe as akijituma kidogo tu,hawezi kuwa kama niliowataja but angalau atakuwepo kwenye league kwa muda mrefu.............anasahau wanaomsifia na kumapamba leo(kwasababu ya njaa zao tu) ndo watakaomcheka kesho,wakati anauza kibanda cha oysterbay na kagari kake(amuulize Mr. Nice).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom