Hali ya Watumishi wa Umma wilayani Maswa ni mbaya sana kwani Watumishi wa kada za elimu na afya wanalazimishwa kukopeshwa fedha nakwa kupitia Saccos bubu iliyopo ndani ya Halmashauri(Inayo milikiwa na Mkurugenzi pamoja na baadhi ya Maafisa utumishi) kwa riba ya asimilia 20 kwa mwezi.
Ndani ya Halmashauri ya Maswa Dc Viongozi wa Halmashauri husika wamekuwa na Tabia ya kujichukulia sheria mkononi kama vile wao ni mahakama.Hii imepelekea watumishi kuwa waoga hata kudai haki zao za msingi,kwa kuhofia mkono wa chuma wa viongozi wa Halmashauri Maswa Dc.
Ajabu ni kwamba watumishi wa umma waliopo ndani ya Halmashauri hii hasa kada ya Elimu na Afya hawana Furaha ya kutumika ndani ya Halmashauri hii,Walimu na wahudumu wa afya wamelazimishwa kuchangia Shilingi 5,000/=kila mmoja toka kwenye mshahara wake(makato ya Moja kwa moja?ili kuchangia shughuli za mbio za Mwenge.
Je,ni kwamba Serikali haina bajeti husika kuhusu mwenge?Kwanini tuwapokonye hata hiki kidogo walichonacho hawa watu ambacho wanajipatia kwa taabu.
Waziri wa Tamisemi na Mkuu wa mkoa wa Simiyu mnapaswa kujua hili na kama mnalijua basi mlichukulie hatua haraka iwezekanavyo,huu ni unyanyasaji wa kiwango cha hali ya juu zaidi kwa watumishi hawa ambao baada ya miaka mitano tunawaomba watuchague tena tukiwachukulia kama kundi muhimu sana.
Jambo lingine mpaka sasa tangu Waajiriwa wapya wa kada za afya na elimu waripoti kazini 28/07/2022 Mapaka leo hawajaingiziwa hata shilingi kumi kwenye akaunti zao hata pesa ya kujikimu,Je bado tutarajie uzalendo na huduma bora toka kwa Watumishi hawa?
Mtu aliyepelekwa eneo kama Ikungulyankhoma anaishije ilihali hana hata pa kuanzia na ni mwezi sasa umepita.
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Maswa mkoa wa Simiyu ameanzisha Saccos bubu ndani ya Halmashauri ambapo wanawakopesha Watumishi wapya fedha za kujikimu kwa riba ya Asilimia 20 kwa mwezi.
Je hii SIMIYU (Maswa) ni nje ya Tanzania?