Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,794
Ni model ya gari ya Toyota Harrier kizazi cha vvt-i (umeme mwingi mafuta kidogo).
Huku kwetu tunaita new model lakini kimsingi sio new model kwa huko Japan.
Kwa kawaida Harrier ni gari zinazosifika kwa ulaji mbaya wa mafuta lakini model hii TAKO LA NYANI ni tofauti na model nyingine
Uundwaji wake umezingatia starehe zaidi, kasi, nguvu na ulaji mdogo wa mafuta. Hivi vigezo vimewavutia wa bongo wengi mpaka kuifanya ndio gari ya kuuzia sura kwa sasa yani ndio gari inayouza.
Huwezi kukaa dakika kumi mahali yanapopita magari bila kuiona hii gari mpaka sasa inaelekea kuwa kama sare ya taifa
Neno TAKO LA NYANI limetokana na hii gari taa zake za nyuma zilivyo.Yani zimekaa kama makalio ya nyani gendaeka yule mwenye makalio mekundu.
Lakini ni wangapi wanajua hatari za hii gari gumzo la jiji? Kwa taarifa yako ndio gari zinazoongoza kwa ajali zikifuatiwa na Alphard.
Unaweza kudhani zina tatizo lakini shida ni sisi wenyewe. Hatujazoea gari zenye take over kubwa na mwendokasi wa fasta.
Hivyo ndugu zangu kama kuna mwenye mpango wa kununua hii gari azingatie haya wepesi, mwendokasi na nguvu ya hii gari
Jr