Harmonize kweli anawanyima usingizi, sasa nao wanakimbilia singeli

Harmonize kweli anawanyima usingizi, sasa nao wanakimbilia singeli

Mtuflani Official

JF-Expert Member
Joined
Dec 31, 2019
Posts
1,949
Reaction score
4,425
Yaani tokea Harmonize ameachana nao wanajaribu njia zote kumzima kwa sababu wanajua akipenya tu ndiyo utakua mwisho wao. Harmonize alitoa nyimbo ya singeli wakaona umepenya sana. Wakamchukua Lavalava nae atengeneze singeli na yule dogo.

Wakaenda mbali na kumlipa producer maarufu Marekani (Swizz Beats) ili awapigie promo waonekane wao ndiyo wakwanza kufanya kitu kama kile🤣🤣🤣. Sasa hivi naona wamemtuma Rayvanny nae afanye singeli.

Yaani hawa jamaa bhana wanatia sana huruma. Wanatumia sana pesa nyingi kulipia matangazo ya nyimbo zao mpya ilimradi tu waTrend YouTube.🤣

Kuna kipindi boss wao alipost ratiba ya show zake sijui anaenda Ulaya sijui wapi. Nimefatilia ile ratiba lakini hamna lolote. Kaishia kweda Nigeria kwenye tuzo na kupiga show kama “curtain raiser” wale complementary artists.

Ujumbe: Achaneni na yule mmakonde. Mnataka azame kumbe nyinyi ndo mnazama🤣🤣🤣
 
Hivi kumbe Harmonize anatoa nyimbo kwa ajili ya WCB? Au WCB wanatoa nyimbo kwa ajili ya Harmonize? Na sio fans tena?
 
Mnamzamisha Harmonize saizi amekuwa kama sabuni ya POA sijui kama unaijua. Kila mtu apambane kwa urefu wa kamba yake. Unataka mziki wa singeli aimbe Harmo peke ake? Kwa ulivyomjinga unadhani harmonize amekuwa msanii wa kwanza kuimba singeli?Singeli ipo wakati Harmo yuko kwenye zipu ya baba ake. Wewe wakati bado hata kiunoni mwa baba yako haupo.

Acha singeli ipae juu. Ni wakati wake sasa.Wasafi washaimba nyimbo za kila dizaini duniani hadi vikota vya kihindi.Labda Harmo ajabu Rege nadhani hiyo Wasafi Hawajaimba. Kuna jipya chini ya jua? Lipi hilo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo Rayvan atulize akili, juzi katoa nyimbo 5 leo anatuletea ujinga wake wa singeli, yaani kama anatapatapa hivi.
Ila pengine na yeye hapendi ila atafanyeje sasa na boss kasema.

Sent using Jamii Forums mobile app

Rayvanny anapigana proxy war! Huu mwaka kabla haujaisha boss ndo atatokezea mwenyewe. Sema wabongo wengi bado wamezibwa macho🤣
 
Back
Top Bottom