NGAYANIMO
Member
- Feb 17, 2026
- 36
- 55
( TUKO NYUMA)
Chorus.
Tuko nyuma kimaendeleo
Sababu ya Rushwa , ubadhilifu na upendeleo
Tuko nyuma
Tuko nyuma Tu na kichocheo
Mambo ni ovyo hatuna Dira wala muelekeo...
Chorus.
Tuko nyuma kimaendeleo
Sababu ya Rushwa , ubadhilifu na upendeleo
Tuko nyuma
Tuko nyuma Tu na kichocheo
Mambo ni ovyo hatuna Dira wala muelekeo...
VERSE..1 ( FANANI )
Tuko nyuma tumechoka hohehae/
Wa Bongo wa leo tulipotoka natamani niwe kipepeo /
Maisha ya shoka ili kushinda yataka upeo/
Ni ma nyoka ma nyoka na twasubiri ni matokeo/
Sijui nchi imeuzwa hatuna dira wala muelekeo/
Tunapuuzwa wazalendo hatuna maendeleo/
Tuna nyanyaswa na wenye vyeo/ wanajifanya madondi malipo ya kodi wananywea vileo/
Lini tutafika usawa huu mwapiga kumeo/
Saa tatu taya mbili za koromeo /
Kweli tuko nyuma bila rushwa hakuna huduma/
Pesa mbele hakuna usawa wala huruma/
Yaani ubaya ubaya kama hauna sogea nyuma/
Kunja ndita kinoma noma rushwa ya chuma/
Kaa mwasibu aone Aibu kula cha Umma/
Haoni hatari kuwa na hekaluu la kifahari/
Yenye ana twaga ana pepeta hana habari/
Ni kazi kwetu walala hoi tusiokuwa na hali/
Kwani macho upima tangu kitambo watu ni chali/
Hatuna makali ya kufanya uzushi kulamba Asali/
Kumbuka wa Bongo pata maono ona kwa mbali/
Na hii ni Bongo nchi safi kwa wenye mali/
Bado na matongotongo mikono juu tumekubari/
Huu sio uongo hapa nchini ni kama Ajali/
Aah natia huruma wa tanganyika roho inauma/
Tuko nyuma kimaendeleo
Sababu ya Rushwa, ubadhilifu na upendeleo /
Tuko nyuma
Tuko nyuma..
Chorus.
Tuko nyuma kimaendeleo
Sababu ya Rushwa , ubadhilifu na upendeleo
Tuko nyuma
Tuko nyuma Tu na kichocheo
Mambo ni ovyo hatuna Dira wala muelekeo...
Chorus.
Tuko nyuma kimaendeleo
Sababu ya Rushwa , ubadhilifu na upendeleo
Tuko nyuma
Tuko nyuma Tu na kichocheo
Mambo ni ovyo hatuna Dira wala muelekeo...
LB GENIUS ' HARB BLASTERS CREW - TUKO NYUMA
Hapa tulipo wabongo tupo nyakanyaka/
Nyakanyaka...!!
Na bado tunapelekwa mchakamchaka/
Kila kona ni Rhumba kali wabongo hatuna hali/
" LB GENIUS" nawaza mbali kudada meli/
shika mtutu Vunja maduka night kali/
Night kali..!!
Tunapotoka ni mbali na bado tunasaga Lami/
Ndani ya jua kali/
Tulowapa madaraka sasa wanaponda mali/
Matatizo kibao na bado hawatujali/
Jali...!!
Kila mtu anapenda kuwa na mali/
Sisi kwa wadosi bado hatuna nafasi/
Ipo siku tutachoka tutapigana Risasi/
Risasi..!!
Madeiwaka hatuna pesa na bado mapolisi wanatutesa/
Kwenye mitaa ni zeke zeke na karaha/
Karaha..!!
Maajabu na machokoraha/
Watanganyika tupo ndani ya nyika/
Tunapokwenda ni lini tutafika sisi watanganyika/
Tuko nyuma toka siku za nyuma mpaka leo/
Mpaka leo..!!
Wabongo kwa wadosi bado ni vibaraka Hatuna vyeo/
Huu ni ukoloni mambo leo/
Tunapelekwa kama picha za video/
Maofisini hatuna Raha kila siku ridadasi/
Vyeo wanapeana wao kwa wao/
Na kabla ya kifo chako hupati mafao/
"LB " napandisha mzuka wa mizuba/
Wazawa tumechoka Bongo hatuna penzi la huba/
Kila siku ni dhuruba/
Kilichobaki tusari Sala za Toba/
Aaah..!!
Tupo nyuma kimaendeleo Sababu ya Rushwa ubadhilifu na upendeleo Tuko nyuma/
Aaah
Ukwaju wa kitambo
0767 542 202
( katika picha ni marehemu Lb genius)