"Hapa Kusoma Tu" Hongereni sana Uongozi wa Mawenzi Sekondari

SHIEKA

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,244
4,258
Tarehe 3/3/2016 binti yangu anayesoma mawenzi sekondari moshi alirudishwa nyumbani akiwa na barua ya uongozi wa shule iliyonihitaji niende shuleni hapo kujadiliana na waalimu juu ya maendeleo na nidhamu ya mwanangu. Sikuielewa kabisa hiyo barua, ikabidi nimuulize kijana kuna nini.Alinijibu kwamba shuleni kulikuwa na operesheni kali ya kukamata simu za wanafunzi.
Nikamwuliza na wewe ulikamatwa na simu? Nilimwuliza kwa sababu mie sijawahi kumnunulia hata kinokia tochi. Jibu alilotoa ni kwamba eti katika ile patashika ya kamatakamata mwanafunzi mmoja kwa kujihami alitupa simu kwenye kitanda chake hivyo simu ikaonekana ni yake (ya binti yangu)
Mazungumzo kati ya wazazi na uongozi wa shule yalifanyika 10/3/2016.Uongozi wa shule ulituonesha simu na vifaa vya mawasiliano walivyovikamata.Si ma-iphones, ma-ipads ma-samsung galaxy, na masimu ya ajabuajabu ambayo hata majina yake sijui.
Ilitushangaza sana jinsi watoto walivyokazania simu kuliko kitabu.
Iliamuliwa kwamba vikochokocho vyote viharibiwe na uongozi wa shule ukasema utachukua jukumu hilo.
Ni kweli simu ni chombo muhimu kwa mawasiliano lakini kwa upande wangu si chombo cha manufaa kwa mwanafunzi aliye shuleni.

Pongezi nyingi uongozi wa mawenzi sekondari moshi kwa kuwaweka watoto kwenye mstari mzuri wa maadili.

friend wangu Amavubi, vipi, ulikuwepo?
 
Tarehe 3/3/2016 binti yangu anayesoma mawenzi sekondari moshi alirudishwa nyumbani akiwa na barua ya uongozi wa shule iliyonihitaji niende shuleni hapo kujadiliana na waalimu juu ya maendeleo na nidhamu ya mwanangu. Sikuielewa kabisa hiyo barua, ikabidi nimuulize kijana kuna nini.Alinijibu kwamba shuleni kulikuwa na operesheni kali ya kukamata simu za wanafunzi.
Nikamwuliza na wewe ulikamatwa na simu? Nilimwuliza kwa sababu mie sijawahi kumnunulia hata kinokia tochi. Jibu alilotoa ni kwamba eti katika ile patashika ya kamatakamata mwanafunzi mmoja kwa kujihami alitupa simu kwenye kitanda chake hivyo simu ikaonekana ni yake (ya binti yangu)
Mazungumzo kati ya wazazi na uongozi wa shule yalifanyika 10/3/2016.Uongozi wa shule ulituonesha simu na vifaa vya mawasiliano walivyovikamata.Si ma-iphones, ma-ipads ma-samsung galaxy, na masimu ya ajabuajabu ambayo hata majina yake sijui.
Ilitushangaza sana jinsi watoto walivyokazania simu kuliko kitabu.
Iliamuliwa kwamba vikochokocho vyote viharibiwe na uongozi wa shule ukasema utachukua jukumu hilo.
Ni kweli simu ni chombo muhimu kwa mawasiliano lakini kwa upande wangu si chombo cha manufaa kwa mwanafunzi aliye shuleni.

Pongezi nyingi uongozi wa mawenzi sekondari moshi kwa kuwaweka watoto kwenye mstari mzuri wa maadili.

friend wangu Amavubi, vipi, ulikuwepo?
Mkuu kwa vile umeenda mpaka pale, hebu niambie kuhusu high school yao. Jee wanafunzi wanapata taaluma iliyo bora? Maana kwa hilo la simu nimeshajua kuwa nidhamu inazingatiwa.
Nina sababu za kutaka kujua
 
Mkuu kwa vile umeenda mpaka pale, hebu niambie kuhusu high school yao. Jee wanafunzi wanapata taaluma iliyo bora? Maana kwa hilo la simu nimeshajua kuwa nidhamu inazingatiwa.
Nina sababu za kutaka kujua
Taaluma bora ni uwepo wa vifaa na walimu.high school mawenzi ni ngumu kuisemea harakaharaka maana ziko combi mbalimbali. Kuna hgl, hge, pcb.Hgl imekaa vizuri, waalimu wa kutosha na wenye bidii. combi nyingine sijui vizuri samahani.
 
Dah Mi nimekuta kisanji anamalizia na mkiramweni ndio akaingia nikiwa o level. Sema wakati huo kulikuwa na kifaa Mama Matee na pia Mr Nyange.

Kipindi cha Mama Mkiramweni,kipindi hicho ilikua kusoma tu kulikua hakuna namna nyingine,mawasiliano ilikua ni kwa posta barua zinasomwa mida ya kutoka,natamani age irudi nyuma!!
 
Dah Mi nimekuta kisanji anamalizia na mkiramweni ndio akaingia nikiwa o level. Sema wakati huo kulikuwa na kifaa Mama Matee na pia Mr Nyange.
Itakua wa class moja mkuu,Mr Nyange ndo alikua wanamwita Bwiru,mkali wa hesabu siku hizo.
Mama Matee alikua mnoko aibu.
Mkuu unaikumbuka mi cake ya mzee Shayo??
 
Itakua wa class moja mkuu,Mr Nyange ndo alikua wanamwita Bwiru,mkali wa hesabu siku hizo.
Mama Matee alikua mnoko aibu.
Mkuu unaikumbuka mi cake ya mzee Shayo??

Naikumbuka sana wakati tunaingia from one alikuwepo dada mmoja anauza wali maharage kwa bei chee sana lkn wakamfukuza sijui alikuwa anaitwa teddy? Alevel ilikuwa vizuri sana enzi hizo.
 
Naikumbuka sana wakati tunaingia from one alikuwepo dada mmoja anauza wali maharage kwa bei chee sana lkn wakamfukuza sijui alikuwa anaitwa teddy? Alevel ilikuwa vizuri sana enzi hizo.
Kweli mdau,baadae sana wakaja kufungua canteen yao.
 
Mimi nilisoma mwika pale advance...yani ukikutwa na simu utafurahi na roho yako
 
Back
Top Bottom