kibaravumba
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 6,635
- 7,005
Nimesikitishwa sana na maneno ya matusi dhidi ya BSS yaliyotolewa na kijana aliyeonekana yuko humble sana na kumbe hayuko hivyo.
Hamis bado una safari ndefu ambayo ndio kwanza ulikuwa unaianza.Unatakiwa ujifunze kuwa positive kila Siku ili ufanikiwe.
Pamoja na kwamba unaamini ungepaswa kuwa mshindi kwa kura za wananchi, unapaswa kujua pia waandaaji wa shindano hilo nao wana vigezo na masharti yao.Binafsi nilikuwa navutiwa sana na uimbaji wako,lakini bado sikuwa tayari wewe ndio uwe mshindi na kubeba brand ya BSS.Nilochoona mimi,ungekuwa mvumilivu,huenda ungejaribu kushiriki tena,ungefanikiwa.
Una bahati sana pia kuonekana kupitia BSS.Hiyo ilitosha kukufanya ushukuru sana kuliko kutupa maneno makali na kuwaita akina madam Ritta "washenzi!"
Huenda kuna changamoto wanazopitia BSS ambazo hawajaamua kuziweka wazi, hadi wakashindwa kuwalipa ninyi.
Ni bora ungekuwa mvumilivu na mwenye busara katika kutoa maoni yako. Maana najua, hata kama kuna mtu mwingine alikuwa na shauku ya kukusaidia, lazima atasita kwa utovu wa nidhamu uliouonesha. Ingekuwa bora ukatumia njia halali kama alivyofanya Meshack kudai haki yako, kuliko kuongea kashfa na matusi katika media.
Nimeongea tu kukushauri sina uhusiano wowote na Madame Rita. Ila ni mpenzi wa BSS.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hamis bado una safari ndefu ambayo ndio kwanza ulikuwa unaianza.Unatakiwa ujifunze kuwa positive kila Siku ili ufanikiwe.
Pamoja na kwamba unaamini ungepaswa kuwa mshindi kwa kura za wananchi, unapaswa kujua pia waandaaji wa shindano hilo nao wana vigezo na masharti yao.Binafsi nilikuwa navutiwa sana na uimbaji wako,lakini bado sikuwa tayari wewe ndio uwe mshindi na kubeba brand ya BSS.Nilochoona mimi,ungekuwa mvumilivu,huenda ungejaribu kushiriki tena,ungefanikiwa.
Una bahati sana pia kuonekana kupitia BSS.Hiyo ilitosha kukufanya ushukuru sana kuliko kutupa maneno makali na kuwaita akina madam Ritta "washenzi!"
Huenda kuna changamoto wanazopitia BSS ambazo hawajaamua kuziweka wazi, hadi wakashindwa kuwalipa ninyi.
Ni bora ungekuwa mvumilivu na mwenye busara katika kutoa maoni yako. Maana najua, hata kama kuna mtu mwingine alikuwa na shauku ya kukusaidia, lazima atasita kwa utovu wa nidhamu uliouonesha. Ingekuwa bora ukatumia njia halali kama alivyofanya Meshack kudai haki yako, kuliko kuongea kashfa na matusi katika media.
Nimeongea tu kukushauri sina uhusiano wowote na Madame Rita. Ila ni mpenzi wa BSS.
Sent using Jamii Forums mobile app