Kwa kipindi cha wiki mbili sasa watumiaji wa halotel wamekuwa wakilalamika kuhusu internet kuwa slow kupita kiasi huku bundle likimalizika kwa kasi ya BRT! Mtakumbuka pia kwamba ni hivi karibuni wameongeza bei ya internet bundles kimya kimya huku ikisemekana ni kwa ajili ya kulipa deni lililotokana na kupigwa faini na TCRA. Cha kushangaza kampuni husika imekuwa kimya kana kwamba haina mtu wa mahusiano ya jamii (Public relations officer) kutoa ufafanuzi/taarifa. Kama mmeridhika na kifo chenu basi naaga kwa kuiambia Halotel "lala mahali pema". Laini yenu nimeiharibu sina hamu nayo isije nitia umasikini.