Sijaelewa wamepata tuzo hiyo kwa kufikia vigezo gani lakini pamoja na mambo mengine nadhani inaweza kuwa ni kutokana na perfomance nzuri kwa mambo mengi ikiwemo kuongezeka kwa mapato isivyo kawaida kulinganisha na huko nyuma.
Kudos kwa madiwani na wabunge wa upinzani kusaidia kuziba mianya ya wizi na ubakaji mapato ya halmashauri kuliko kuwa kunafanywa na genge la viongozi wa CCM na mawakala wao.
Channel 10 TV - hapa naona Halmashauri ya Kinondoni inapokea zawadi ya kuwa Halmashauri bora Barani Afrika. Loh. Kumbe na sisi tupo! Mungu endelea kuibariki Tanzania!!
Halmashauri bora barani Afrika?! Kweli...!!!!? Mambo mengine ni dhihaka tupu, tena dhihaka hasa. Jana nilipoona kwenye taarifa ya habari nilibaki na mshangao... Hebu tujifikirishe kidogo
-mshindanishaji alikuwa ni nani?
-Alitumia vigezo gani muhimu!?
-Alitumia halmashauri za majiji mangapi yenye mfumo kama wetu?
Kwa miundombinu ile ya kuingilia na kutokea halafu kinondoni ikashika no 1, sijui aliyeshika mkia yukoje? Najua tunapenda mno maigizo lakini yasiachane mno na uhalisia
Root naipenda sana nchi yangu tena sana lakini siwezi kuwa mnafiki penye ukweli nyeusi nitaita nyeusiWatanzania wachawi, hawaipendi Tanzania. Jamani hii ni nchi yenu ulizaliwa hapa na utafia hapa. Ipende hata kinafiki
Watanzania wachawi, hawaipendi Tanzania. Jamani hii ni nchi yenu ulizaliwa hapa na utafia hapa. Ipende hata kinafiki