Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na pia Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Dodoma, Ndugu Halima White Zuberi, amesema kuwa kwa mshikamano wa wakazi wa Dodoma na wanachama wa CCM, watahakikisha chama hicho kinapata ushindi mkubwa katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Zuberi ameyasema hayo leo, Jumatano Julai 2, 2025, jijini Dodoma aliporejesha fomu ya kuwania Ubunge wa Viti Maalum kupitia Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Mkoa wa Dodoma.
Amesema kuwa wanachama wa CCM watafanya kila jitihada kuhakikisha wanazipata kura zote za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na wagombea wote wa CCM wanaotegemea kuteuliwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi, ikiwemo Madiwani na Wabunge.
"Chama chetu kitaendelea kuwa ngome imara katika Mkoa wa Dodoma, na sisi kama wanachama tutahakikisha hilo linafanikiwa, iwe inanyesha mvua ama jua linawaka," amesema Zuberi kwa msisitizo.