Halima Mdee Unachemka

Watanzania wana tabu sana mkuu.

Wanataka Mdee akawajengee barabara.....Ukenge mwingine tabu tupu.
Huu sio Ukenge, Mbunge anawajibika kwa wananchi wake waliomchagua, yeye ndio sauti yetu kwa serikali. Tunajua kuna hela zipo za budget ya barabara na hata siku ile aliokuja alisema hela zilikuwepo so nikufuatilia tu. Ukiomba chakula kwa baba yako sio maana apike na akulishe, jukumu lake ni kuleta chakula then wapo watendaji watashughulika mpka kinapikwa na watu wanakula na wengine watalishwa. Understand hilo mkuu na jua haki zako. hii sio tabu, tunamuonyesha jinsi gani anavyokuwa mzembe na kazi yake, au unataka aje JK ajenge? kuwa serious bwana na topics serious kama wataka joke zipo uzi za jokes.
 
Anaetakiwa kujua mambo ya kauchochoro ka mtaani kwenu ni Mbunge au Diwani?

That is No brainer.
Kama nim kauchochoro why alikuja siku ya kwanza na kutoa ahadi hewa? Anajua hivyo vi uchochoro vina count kwenye KURA. Huu ni ukweli na ukweli huwa unauma. Kama alijua ni kazi ya DIWANI mbona hajampa diwani hilo jukumu? wote tunapenda mapinduzi ila kama kuna mtu anachelewesha mapinduzi tunamsema. kama huyu ni nduguyo basi ukamwambia haya alafu uone kama atakuambia hii kazi yake au ya diwani.
 
Una funza kwenye ubongo, mdee anakusanya kodi yako?
Angepewa jukumu la kukusanya KODI si ndio angehamia USA kuishi huko, maana saa hivi analipwa na kodi zetu haonekani kwenye maswala muhimu. Yeye ni sauti ya wananchi katika serikali. Cha msingi tunataka mgombea mwingine 2015 from CDM wakimuweka huyu sister do itameza kwao full. sisi tupo ground zero huku tunaona na tunasikia ya wananchi sasa wewe leta siasa za hapa mtandaoni umpotoshe mwenzio.
 
Siku hizi Mhe Mdee anakusanya kodi? Kwanini Hamuwadai mnawaowalipa kodi? Miaka 53 ya uhuru CCM imewafanyia nini wananchi wa kawe?.... I guess mleta mada ni kada wa CCM na anajua kuwa kazi ya ujenzi wa barabara, miundo mbinu ya maji na umeme ni kazi ya serikali iliyoko madarakani kwa kuwa wao ndio wanaokusanya kodi na kuingia mikataba ya kuuza rasilimali zetu... Mhe. Mdee tunamshukuru sana otherwise ardhi ya Watanzania ungekuta karibu yote imeshanyakuliwa na wazungu ...Kawe mnatakiwa mumsupport Halima Mdee kwa nguvu zaidi kwani baadhi ya mbinu chafu ya CCM ni kutokupeleka maendeleo kwenye majimbo ya wapinzani....
 
Halima mda mwingi hushinda Saloon akijitumbua Chunusi sugu,huku akiwaza atazaa lini maana bado ni Single

mazee kuwen na heshima kidogo na binadam wenzenu ndugu yangu.
 
Sasa mkuu mwenzio akijipaka kinyesi na wewe wajipaka zaidi au unamsafisha? Hao CCM kweli kabisa hawajafanya lolote lile ktk Taifa ili tokea Baba wa Taifa awachie nchi hii. Ndio maana tumempa Mh. Mdee na CDM support waichukue nchi, sasa kama yeye ndio msemaji wetu serikalini na unajua fika kuwa huko kuna mafungu ya kazi hizi za maendeleo why akae kimya while tuna haribikiwa, na sisi tumemtuma awawajibishe magamba?Point yangu sio kuwaleta CCM ktk jimbo la kawe,Mimi ni mwamna mageuzi mzuri tu so ninapo ona wana mageuzi wenzangu tulio wapa majukumu nao wana kuwa kama CCM nashangaa sana. Point hapa ni kumbusha mh. Mdee kuwa awe ana keep promise zake, hata kama amefanya mambo mengi na hili pia kama ni dogo pia ni jambo lazima alifanye kumbuka kuna usemi usemao " Unakula Ng'mbe mzima unashindwa mkia" so Ajipange amalizie mkia.
 
Kweli nimeamini member humu wanaongozwa na chuki.NITAJIENI MAJUKUMU YA MBUNGE..suala la barabara ni jukumu la council..kama ni hivyo hakuna mbunge ambaye atarudi coz barabara nyingi tanzania zina hali hii.

MFANO sasa ivi nipo jimbo la OLE SENDEKA hapa number tano hapafai na magari yamekwama kwa mafuriko na ubovu wa barabara so CCM NDO INA MFUMO MBOVU NA IMEFIKA TAMATI NA KODI INAYOTUMIA KTK KUWAPA UBUNGE WATOTO WA WAKUBWA.
 
inawezekana mdee ni mkurugenzi wa manispaa au tanroads na ana bajeti ya barabara huwezi jua ndugu. meya wa jiji na wa manispaa wanawekwa kipande ipi hapo.
Mdee ni Sauti ya wananchi kwa serikali, Sisi hatujawahi mchagua mkurugenzi wa Jiji wa Meya wa Jiji. Eleweni majukumu ya Mbunge.
 
Sasa kama sio Jukumu lao kuongea kero za wananchi kazi yao ni nini? Hapa hatusemi aje atengeneze yeye barabara anatakiwa komaa barabara itengenezwe, same kwa huyo Mbunge wako OLE Sendeka, Hapa wala hatuna chuki na mtu tunamkumbusha majukumu yake, Soma vizuri Mada nimeeleza vizuri sana kwamba alikuja mwaka jana na akaona hili tatizo na aka promise kushughulikia in a month time, tokea siku ile hajarudi tena wala hatujapata feedback yoyote kuhusu tuliongea nae na ahadi yake. So hapo kuna Kosa kwetu au kwake? Ila 2015 hiyooo sijui atapita wapi kuja kutuomba hizo Kura au atakuja na HELIKOPTA??
 

kwahiyo mbunge akamuwajibishe mhusika na aliyewateua amechukua hatua gani?.ok kwani hyo barabara ipo chini ya mamlaka ipi?.
 
kwahiyo mbunge akamuwajibishe mhusika na aliyewateua amechukua hatua gani?.ok kwani hyo barabara ipo chini ya mamlaka ipi?.
Yeye anajua ipo kwa mamlaka ipi ndio maana alikuja mwaka Jana na akahaidi kurudi kwetu ndani ya mwezi na solution ya tatizo letu, but ndio ikawa kimojaa, tunamuona kwa Luninga tu mjengoni.
 
duuuh itatuchukua miaka mingi kuelewa wajibu wa serkl inayokusanya mapato/kodi na kaz ya uwakilish wa mbunge......!!!

Kweli mkuu, na magamba wakiona hivi wanafurahia sana kwani wanajua watu bado hawajitambui.
 
Haki ya Mungu ningekuwa na namba ya simu au email yake ningemtumia hizi foto kwa simu yake! kama kuna mtu anavyo hivyo ani inbox au kama mtu ana facebook/Twitter yake share hapa niruke nae majoka.
 
Mdee ni Sauti ya wananchi kwa serikali, Sisi hatujawahi mchagua mkurugenzi wa Jiji wa Meya wa Jiji. Eleweni majukumu ya Mbunge.

sawa naomba uniambie hao majukumu yake kwa uchache,je na kama akafuatilia na kupuuzwa na wahusika ana mamlaka ipi kisheria dhidi yao?.
 
Kweli mkuu, na magamba wakiona hivi wanafurahia sana kwani wanajua watu bado hawajitambui.
Hebu tuambieni nyie mnaojua Majukumu ya Mbunge, kama hili sio lake mtuambie tulipeleke mahala husika. Ila I always wasikia waheshimiwa bungeni pale wakisema wananchi wangu hawana Maji, Barabara Mbovu n.k au?Na kwenye kampeni zao wanasema pia maneno haya mkinichagua ntahakikisha barabara zote zinapitika, maji yanapatikana n.k au hizo zinakuwa ni pwepwe za kampeni tu then tukiwachagua inabidi tuwasiliane na President?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…