HALI YA USALAMA NCHINI-JK words

mmakonde

JF-Expert Member
Dec 26, 2009
965
66

Hali ya Usalama Nchini

Ndugu Wananchi;
Hivi karibuni wananchi wengi wameingiwa na hofu kubwa kuhusu usalama wa nchi yetu. Ni mara ya kwanza Watanzania wamekuwa hivyo. Hofu hiyo inatokana na kauli na vitendo vya wenzetu wa CHADEMA vyenye dhamira ya kutaka kuleta machafuko makubwa na uvunjifu wa amani nchini. Kufanya maandamano na mikutano ni haki ya msingi ya vyama vya siasa na raia. Lakini, kuigeuza fursa hiyo kuwa ni jukwaa la kuchochea ghasia na kwa nia ya kuiondoa Serikali iliyoko madarakani kwa mabavu ni matumizi mabaya ya fursa hiyo.

Nchi yetu ni ya kidemokrasia na kila miaka mitano tunafanya uchaguzi wa kuchagua viongozi wetu. Uchaguzi wa mwisho tumefanya tarehe 31 Oktoba, 2010. Kabla ya hapo tulikuwa na kampeni zilizochukua karibu miezi mwili na nusu. Kila chama kilielezea jinsi kitakavyokabiliana na matatizo yanayowakabili wananchi wa nchi yetu ikiwa ni pamoja na haya wanayoyazungumza sasa. Hatimaye siku ya uchaguzi wananchi walifanya uamuzi wa kuchagua chama walichokiamini, nacho ni Chama cha Mapinduzi. Iweje leo, miezi mitatu baadae kwa mtu au chama cha siasa kufanya maandamano kwa masuala yale yale waliyoyasema kwenye kampeni. Siyo sawa hata kidogo. Kuchochea ghasia ati kwa nia ya kuiondoa Serikali madarakani ni kinyume cha Katiba na ni kuiingiza nchi katika mgogoro usiokuwa wa lazima. Tutasababisha umwagaji wa damu, watu kupoteza maisha na mali zao kuharibiwa bila sababu yoyote ya msingi.

 
Hali ya Usalama Nchini







Ndugu Wananchi;




Hivi karibuni wananchi wengi wameingiwa na hofu kubwa kuhusu usalama wa nchi yetu. Ni mara ya kwanza Watanzania wamekuwa hivyo. Hofu hiyo inatokana na kauli na vitendo vya wenzetu wa CHADEMA vyenye dhamira ya kutaka kuleta machafuko makubwa na uvunjifu wa amani nchini. Kufanya maandamano na mikutano ni haki ya msingi ya vyama vya siasa na raia. Lakini, kuigeuza fursa hiyo kuwa ni jukwaa la kuchochea ghasia na kwa nia ya kuiondoa Serikali iliyoko madarakani kwa mabavu ni matumizi mabaya ya fursa hiyo.

Nchi yetu ni ya kidemokrasia na kila miaka mitano tunafanya uchaguzi wa kuchagua viongozi wetu. Uchaguzi wa mwisho tumefanya tarehe 31 Oktoba, 2010. Kabla ya hapo tulikuwa na kampeni zilizochukua karibu miezi mwili na nusu. Kila chama kilielezea jinsi kitakavyokabiliana na matatizo yanayowakabili wananchi wa nchi yetu ikiwa ni pamoja na haya wanayoyazungumza sasa. Hatimaye siku ya uchaguzi wananchi walifanya uamuzi wa kuchagua chama walichokiamini, nacho ni Chama cha Mapinduzi. Iweje leo, miezi mitatu baadae kwa mtu au chama cha siasa kufanya maandamano kwa masuala yale yale waliyoyasema kwenye kampeni. Siyo sawa hata kidogo. Kuchochea ghasia ati kwa nia ya kuiondoa Serikali madarakani ni kinyume cha Katiba na ni kuiingiza nchi katika mgogoro usiokuwa wa lazima. Tutasababisha umwagaji wa damu, watu kupoteza maisha na mali zao kuharibiwa bila sababu yoyote ya msingi.


yaani anadhani watu wanaihofu chadema? watu wanahofu milipuko ya mabomu, ufisadi, hali ngumu ya maisha inayoweza kuibua wimbi la wizi na ujambazi. Ndiyo mambo ambayo mtu mwenye dhamana ya Urais angepaswa kuyatolea mikakati ya kukabiliana nayo.
This guy is highly disconnected from reality!
 
Nimesikiliza hotuba ya JK,hasa kuhusu usalama wa taifa,nikashangaa sana
Kuwalaumu CDM kwa hili it is unbeliavable.

Nafikiri Rais bado anafikiri watu tuko miaka ya 70 au 80!
Watu tunaelea mambo mengi ya nchi kuliko hata watu wa UWT.

Watu wamechoka na bla bla bla.Miaka 50 ya uhuru,bado watu wanahangaika na
1.Umeme wa uhakika
2.Njaa
3.Maji
4.Inflation
5.Poor education for majority

YET kuna watu wachache wameamua kuihujumu nchi ,without any shame.Hata balozi wetu huko USA anafaidi na hii ring ya corruption through these mediocre law firms!Really it is beyond comprehension
Angalia Dowans,tunaoneka kama sisi Wananchi we are so stupid!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!JAMANI yule Mwarabu eti asipigwe picha imenifanya
mimi niamini there is idiocy among many people in Tanzania

I tell you nchi imekuwa so corrupt kuliko hata jirani zetu wa KENYA.
Mbaya zaidi ,nchi yetu imekuwa top recipient wa foreign aid,kwa about 50 years now,pamoja na "AMANI NA UTULIVU",lakini pace ya maendeleo ni ndogo sana.

NANI ni custodian wa taifa hili?
I doubt,we are going to the wire.
Ukiangalia 2 past presidents they are all the same.To be fair to JK,haya madudu yalianza chini ya Mmakonde mwenzangu,MKAPA.kufanya biashara IKULU na other dubious deals.

Tungekuwa na Judiciary huru,Mkapa,Lowassa,Mkono,Chenge,Karamagi,Mramba na other gangsters wangekuwa KEKO gerezani.
Lakini kwa sababu ya UTULIVU NA AMANI wako nje,bado wanaplot uozo .F*******************. i am angry.
 
Back
Top Bottom