Hali ya Usalama Jijini Dar inazidi kuzorota, Vyombo vya Usalama vinafanya kazi gani?

falcon mombasa

JF-Expert Member
Mar 5, 2015
9,159
9,241
Saa saba na nusu usiku huu nilipokua natoka masaki naenda sinza kupitia kinondoni nimekutana na tukio la kuhuzunisha sana,

Nilipoanza kushuka bonde la mkwajuni kuelekea moroco hotel takribani njia nzima nilikua peke yangu naendesha gari ndipo kwa mbaali nikaona vijana watatu wanakimbia kuelekea moroco hotel huku mmoja kati yao akiwa yuko mbele na begi mgongoni huku wawili wakiwa nyuma wanamkimbiza

Nilipofika karibu niligundua wale vibaka walikua wanataka kumkaba yule wa mbele huku wakiwa na vitu mfano nondo zenye ncha kali,basi nikakimbiza gari hadi kuwa usawa sawa na yule wa mbele ndipo nilimsikia vizuri akiomba msaada huku bado wale vijana wakiendelea kuja,nilipofanya maamuzi ya kujaribu kusimama ili kumpa lift yule anaekimbizwa gafla nikaona vijana wengine wanne wanatokea kwenye bonde hilohilo la mkwajuni wakikimbilia gari yangu ndipo nilipoamua kukimbiza gari haraka huku nikimuacha yule jamaa amezingirwa.

Sasa kilichopolekea hadi kuandika uzi huu nimesikitishwa sana nilipofika kituo cha polis magomeni ili kutoa taarifa haraka nikakuta kumezungushiwa utepe unaonikataza kuingia kituoni hadi kesho asubuhi, basi sikuwa na la kufanya zaidi ya kuondoka huku nikiwa nimesikitika nikimfikiria yule mshkaji.

Sasa hapa nauliza jeshi la polis la tanzania lipo kwaajili ya kumlinda nani jamani mbona sielewi?
 
pole yake lakini hivi ni kwa nini vituo vya polisi wanavifunga usiku......nafikiri haya ni mabadiliko toka lile tukio la kituo cha stakishari naona wakaja na fomula ya kuvifunga.......ila kwa muda huu hata hapa mtaani kwetu chooni huendi ni mwendo wa kwenye kopo ndio maana tuko macho mpaka muda huu
 
Kuna siku kama saa sita usiku nilitokea magomeni kuja kinondoni kwa mguu, kuna jamaa pale hotel morocco hotel nikamwuliza vp hakuna vibaka hapo bondeni? Akaniambia wapo ila dawa yake pita kwenye barabara ya mwendo kasi halafu uwe unakimbia kama unafanya mazoezi hivi, mara unainama, mara unainuka hawakukabi.

Nikaanza kukimbia bwana, ile kufika usawa wa ilipokuwa ile nyumba nzuri iliyobomolewa aisee walitokea vijana wawili wana mapanga marefu kama ya akina Jack Chen walinikimbiza hadi kituo cha mkwajuni wakaniacha pale baada ya kuona kuna dalili za watu.

Lile bonde la mkwajuni halifai na ukizingatia yale maeneo ndio makao makuu ya sembe na bange.
 
Juzi hapo kuna jamaa yangu niliongea nae anadai huko kwao ofisi ya premier betting ilivunjwa usiku na flat tv karibuni tano,pc mbili na pesa zimeibwa,na hapo mahali ni karibu na kituo cha polisi.

Yaani watu wanabeba 40" flat tv tano na computer na kuondoka salama kabisa bila kushtukiwa mapema.

Dar hapako sawa kipindi hiki.
 
pole yake lakini hivi ni kwa nini vituo vya polisi wanavifunga usiku......nafikiri haya ni mabadiliko toka lile tukio la kituo cha stakishari naona wakaja na fomula ya kuvifunga.......ila kwa muda huu hata hapa mtaani kwetu chooni huendi ni mwendo wa kwenye kopo ndio maana tuko macho mpaka muda huu
Pale Stakishari kuna geti usiku na utepe mchana. Maajabu haya
 
Hata maeneo ya goba-mbezi pale njia panda ya kinzudi ukija mpaka kwa mwaikambo mpaka kunguru hali ni tete uhalifu umeongezeka sana ,polisi tunaomba msaada wenu ,mbwa wanawekewa sumu magari wanaiba power windows ili mradi amani haipo uck
 
Mkuu kuna uwezekano mkubwa ikawa wewe ndio ulikuwa mlengwa wa tukio hilo. Hao jamaa ni team moja ungesama ingekula kwako.
Si rahisi raia kukatiza saa saba usiku katika bonde hilo labda mgeni.
Hata mgeni si rahisi kukatiza labda teja
 
Mleta mada... imeshasemwa sana humu kuhusu warning za kupita bonde la mkwajuni usiku

Sielewi kwanini umepita hiyo njia
 
Saa saba na nusu usiku huu nilipokua natoka masaki naenda sinza kupitia kinondoni nimekutana na tukio la kuhuzunisha sana,

Nilipoanza kushuka bonde la mkwajuni kuelekea moroco hotel takribani njia nzima nilikua peke yangu naendesha gari ndipo kwa mbaali nikaona vijana watatu wanakimbia kuelekea moroco hotel huku mmoja kati yao akiwa yuko mbele na begi mgongoni huku wawili wakiwa nyuma wanamkimbiza

Nilipofika karibu niligundua wale vibaka walikua wanataka kumkaba yule wa mbele huku wakiwa na vitu mfano nondo zenye ncha kali,basi nikakimbiza gari hadi kuwa usawa sawa na yule wa mbele ndipo nilimsikia vizuri akiomba msaada huku bado wale vijana wakiendelea kuja,nilipofanya maamuzi ya kujaribu kusimama ili kumpa lift yule anaekimbizwa gafla nikaona vijana wengine wanne wanatokea kwenye bonde hilohilo la mkwajuni wakikimbilia gari yangu ndipo nilipoamua kukimbiza gari haraka huku nikimuacha yule jamaa amezingirwa.

Sasa kilichopolekea hadi kuandika uzi huu nimesikitishwa sana nilipofika kituo cha polis magomeni ili kutoa taarifa haraka nikakuta kumezungushiwa utepe unaonikataza kuingia kituoni hadi kesho asubuhi, basi sikuwa na la kufanya zaidi ya kuondoka huku nikiwa nimesikitika nikimfikiria yule mshkaji.

Sasa hapa nauliza jeshi la polis la tanzania lipo kwaajili ya kumlinda nani jamani mbona sielewi?

Kuwalinda ccm ili chadema wasifanye mikutano yao. Masna wataiumbua serikali yetu tukufu. Maana wao ni maigizo tu.
 
Back
Top Bottom