Moderator, najua hii mada inaangukia jukwa la elimu, lakini naomba msihamishe hii, angalia kwa muda wa siku chache.
Juzi nimemsikia Mwigulu Nchemba akitamba sana kuhusu maendeleo ya elimu nchini na hasa kwenye Jimbo lake. Hii ni pale alipohojiwa na VoA.
Sasa Tarehe 01 Septemba 2013 Dk Kitila Mkumbo alialikwa na umoja wa wanafunzi wa vyuo vikuu wanaotoka Iramba kushiriki mjadala wa namna ya kuboresha elimu Iramba na alipewa nafasi ya kuwa mgeni rasmi. Katika hotuba yake, pamoja na mambo mengine alieleza hali ya elimu katika Jimbo hilo na akatoa mapendekezo yake ya namna ya kutoka hapo. Alionyesha kwamba hali ni mbaya sana. Nawaletea dondoo za yale yaliyokuwemo kwenye hotuba yake ambaye aliigawa kwa wajumbe. Of course hotuba yake ilileta kasheshe na manusura Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Lulumba afukuzwe na afisa elimu sekondari kwa kumkaribisha Dk Mkumbo kwa maelekezo ya mkuu wa Jimbo, Mwigulu. Bahati nzuri hotuba yake aliigawa kwa Afisa Elimu na watumishi wa halmashauri ya wilaya na watu waliifurahia. Mwigulu alikasirika sana kwa nini yeye hakupewa nafasi ya kuwa mgeni rasmi. Anyway, hii hapa ndiyo hali halisi ya elimu huko Iramba.
____________________________________________________________________________________________
· Jumla ya Wanafunzi waliofanya mtihani mwaka 2012: 1804
o Waliofaulu: 376, sawa na asilimia 20.8
o Jumla ya waliofeli na waliofaulu kwa ngazi ya Daraja la Nne: 1393, sawa na asilimia 77.2
o Waliofaulu somo la hesabu: 83, sawa na asilimia 4.6.
o Kati ya shule tano zilizofanya vibaya zaidi kimkoa (Singida), tatu zipo katika Wilaya ya Iramba (Jimbo la Iramba Magharibi) ambazo ni: Mgongo 94/94, Kyengege 91/94 na New Kiomboi 92/94. Kyengege ndiyo Kata anayotoka mbunge wa Iramba Magharibi.
o Shule ya mwisho kimkoa ipo katika Wilaya ya Iramba (Jimbo la Iramba Magharibi), nayo ni Shule ya Sekondari Mgongo.
Kwa matokeo haya ni vijana 35 pekee wenye uwezekano wa kujinga na kidato cha tano mwaka 2013 kutoka Wilaya ya Iramba, na ni hawa pekee wenye uwezekano wa kujiunga na Vyuo Vikuu na Elimu ya Juu mwaka 2015.
Sasa hiyo elimu bora ambayo Mwigulu alikuwa anatamba nayo huko VoA ni ipi?
Juzi nimemsikia Mwigulu Nchemba akitamba sana kuhusu maendeleo ya elimu nchini na hasa kwenye Jimbo lake. Hii ni pale alipohojiwa na VoA.
Sasa Tarehe 01 Septemba 2013 Dk Kitila Mkumbo alialikwa na umoja wa wanafunzi wa vyuo vikuu wanaotoka Iramba kushiriki mjadala wa namna ya kuboresha elimu Iramba na alipewa nafasi ya kuwa mgeni rasmi. Katika hotuba yake, pamoja na mambo mengine alieleza hali ya elimu katika Jimbo hilo na akatoa mapendekezo yake ya namna ya kutoka hapo. Alionyesha kwamba hali ni mbaya sana. Nawaletea dondoo za yale yaliyokuwemo kwenye hotuba yake ambaye aliigawa kwa wajumbe. Of course hotuba yake ilileta kasheshe na manusura Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Lulumba afukuzwe na afisa elimu sekondari kwa kumkaribisha Dk Mkumbo kwa maelekezo ya mkuu wa Jimbo, Mwigulu. Bahati nzuri hotuba yake aliigawa kwa Afisa Elimu na watumishi wa halmashauri ya wilaya na watu waliifurahia. Mwigulu alikasirika sana kwa nini yeye hakupewa nafasi ya kuwa mgeni rasmi. Anyway, hii hapa ndiyo hali halisi ya elimu huko Iramba.
____________________________________________________________________________________________
· Jumla ya Wanafunzi waliofanya mtihani mwaka 2012: 1804
o Waliofaulu: 376, sawa na asilimia 20.8
o Jumla ya waliofeli na waliofaulu kwa ngazi ya Daraja la Nne: 1393, sawa na asilimia 77.2
o Waliofaulu somo la hesabu: 83, sawa na asilimia 4.6.
o Kati ya shule tano zilizofanya vibaya zaidi kimkoa (Singida), tatu zipo katika Wilaya ya Iramba (Jimbo la Iramba Magharibi) ambazo ni: Mgongo 94/94, Kyengege 91/94 na New Kiomboi 92/94. Kyengege ndiyo Kata anayotoka mbunge wa Iramba Magharibi.
o Shule ya mwisho kimkoa ipo katika Wilaya ya Iramba (Jimbo la Iramba Magharibi), nayo ni Shule ya Sekondari Mgongo.
Kwa matokeo haya ni vijana 35 pekee wenye uwezekano wa kujinga na kidato cha tano mwaka 2013 kutoka Wilaya ya Iramba, na ni hawa pekee wenye uwezekano wa kujiunga na Vyuo Vikuu na Elimu ya Juu mwaka 2015.
Sasa hiyo elimu bora ambayo Mwigulu alikuwa anatamba nayo huko VoA ni ipi?