Rugby Union
JF-Expert Member
- Nov 21, 2012
- 402
- 257
Ripoti zinasema kuwa hali si shwari ndani ya Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa, licha ya sintofahamu kufuatia kusitishwa kwa zoezi la ugawaji wa vitambulisho katika baadhi ya maeneo, utendaji ndani ya taasisi hiyo hauko vizuri.
Madudu mengine ndani ya NIDA ikiwemo kupeana kazi kindugu (karibu watu wote wanaofanya kazi data centre, iliyopo jengo la BMTL, Victoria wameajiriwa bila utaratibu rasmi na wanajuana na wakubwa wa NIDA). Jambo lingine ni ndugu na vimada wa mabosi wa NIDA kutaka kupewa huduma za vitambulisho bila kufuata utaratibu rasmi kwenye vituo vya ugawaji vitambulisho, jambo ambalo limekuwa kero kubwa kwa wafanyakazi hao.
Malipo ya wafanyakazi wanaoenda kufanya kazi za nje ya kituo huwa hayapo, au ni ya kuzungushwa, huku wakiambiwa na baadhi ya watu walio karibu na wakuu wa idara kuwa hela ipo, lakini wasipofuatilia wataambulia patupu.
Tuhuma zingine ni pamoja na mamlaka kutuhumiwa kuajiri watu ambao aidha hawana elimu stahiki ama ambao utendaji wao ni dhaifu kwa kuwa tu wana mahusiano ya kindugu/mapenzi na hao wanaoitwa vigogo wa taasisi hiyo (wakuu wa idara na mameneja).
Kinachotarajiwa: Kutokana na matatizo hayo ambayo ni ya muda mrefu na hayana dalili ya kutatuliwa kuna uwezekano wafanyakazi wa NIDA wakashusha utandaji wao kwa makusudi, hii ni kwa mujibu wa mtu aliye karibu.
Madudu mengine ndani ya NIDA ikiwemo kupeana kazi kindugu (karibu watu wote wanaofanya kazi data centre, iliyopo jengo la BMTL, Victoria wameajiriwa bila utaratibu rasmi na wanajuana na wakubwa wa NIDA). Jambo lingine ni ndugu na vimada wa mabosi wa NIDA kutaka kupewa huduma za vitambulisho bila kufuata utaratibu rasmi kwenye vituo vya ugawaji vitambulisho, jambo ambalo limekuwa kero kubwa kwa wafanyakazi hao.
Malipo ya wafanyakazi wanaoenda kufanya kazi za nje ya kituo huwa hayapo, au ni ya kuzungushwa, huku wakiambiwa na baadhi ya watu walio karibu na wakuu wa idara kuwa hela ipo, lakini wasipofuatilia wataambulia patupu.
Tuhuma zingine ni pamoja na mamlaka kutuhumiwa kuajiri watu ambao aidha hawana elimu stahiki ama ambao utendaji wao ni dhaifu kwa kuwa tu wana mahusiano ya kindugu/mapenzi na hao wanaoitwa vigogo wa taasisi hiyo (wakuu wa idara na mameneja).
Kinachotarajiwa: Kutokana na matatizo hayo ambayo ni ya muda mrefu na hayana dalili ya kutatuliwa kuna uwezekano wafanyakazi wa NIDA wakashusha utandaji wao kwa makusudi, hii ni kwa mujibu wa mtu aliye karibu.