Henry Kilewo
JF-Expert Member
- Feb 9, 2010
- 899
- 1,108
Ndugu zangu Watanzania wenzangu kwa kipindi hiki ambacho chama chetu CHADEMA tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu wa kitaifa na mimi nikiwa ni mmoja wa wagombea kwenye Nafasi ya Ujumbe wa Kamati Kuu napenda kuongea na nyie leo maneno machache sana ila yenye uzito wake.
Kipindi changu chote cha mapambano yangu kwaajili ya uhuru wa nchi yangu, sijawahi kuwa na shaka hata mara moja kuhusu ushindi wa mwisho wa mapigano matakatifu ambayo mimi na nyie tumejitolea maisha yetu.
Kwaajili ya kile tunachoitakia nchi yetu ya kuwa na maisha ya kuheshimika yaliyo na utu yenye uhuru bila vikwazo kutoka kwenye ukoloni wa ccm na washirika wake wa kukandamiza haki na usawa kwa watakamabadiliko, Ambao wamepata msaada wa moja kwa moja ama usiyo wa moja kwa moja,kwa makusudi ama bila makusudi Maafisa Fulani wa juu wa jeshi la polisi wasiyokuwa waaminifu wameendelea kuwa upande wa ccm bila kutambua kuwa ipo siku ccm itaondoka madarakani na wao wataendelea kuwa na wajibu wakulitumika Taifa.
Wananchi wengi wanapewa rushwa kwaajili ya kufanikisha kupotosha ukweli wa uhitaji wa serikali ya ccm kuondoka madarakani,ndio Wanatuchelewesha, wanatuhuzunisha lakini ninauhakika hakuna jambo baya linaloweza kuishi milele bali jambo OVU huishi kwa muda na kupotea milele, Nenda Kenya,Malawi, Zambia nk, Kama jeshi liliwahi kushindana na Umma likashinda.
Ila Chadema hatupo peke yetu Walimu,Wakulima,Wavuvi,Madaktari,Wafanyakazi, waendesha boda boda,wasukuma mikokoteni,mama lishe,wanafunzi na wataka mabadiliko kote duniani na watu waliyohuru kutoka kila pembe ya Tanzania siku zote watakuwepo upande wa Chadema hawata utelekeza mwanga huu wa Chadema mpaka siku zitakapo kuja ambazo hakutakuwa na wakoloni tena pamoja na wanajeshi wa kununuliwa katika nchi yetu.
Kwa wenetu ambao tutawaacha na wengine ambao hatutawaona tena, Natamani waje kuambiwa kuwa mustakabali wa Tanzania ni mzuri na unatarajiwa kuwa kila Mtanzania atafanikisha kazi takatifu ya kuujenga upya uhuru wetu na utaifa wetu.
Kwakuwa bila utu hakuna uhuru,Bila haki hakuna utu na bila uhuru hakuna watu waliyo huru.
Hakuna ukatili kutendewa sivyo ama mateso yaliyonifanya niombe -kuhurumiwa kwakuwa napendelea kufa kishujaa, Imani ikiwajuu na kujiamini kwangu kukiwa na umuhimu katika kujua mwisho wa nchi yangu.
Historia itazungumza siku moja japokuwa haitakuwa historia ya kuifurahisha CCM na washirika wake kwani huwo utakuwa ndiyo mwisho wake.
Lakini ni ile itakayofundishwa kutoka mikononi mwa ccm na wapambe wake,Chadema itaandika historia yake Mwisho na itakakuwepo Kaskazini,kusini,mashariki na magharibi mwa Tanzania Historia ya utukufu na utu.
Tafadhali msisononeke makamanda wenzangu, najua mnajua nchi yetu inateseka kwakiasi kikubwa na itajua namna ya kuulinda uhuru wake....
Mgombea ujumbe kamati kuu Chadema 2014
-
Mungu ibariki Chadema
Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki Afrika
Henry Kilewo
05.09.2014
Kipindi changu chote cha mapambano yangu kwaajili ya uhuru wa nchi yangu, sijawahi kuwa na shaka hata mara moja kuhusu ushindi wa mwisho wa mapigano matakatifu ambayo mimi na nyie tumejitolea maisha yetu.
Kwaajili ya kile tunachoitakia nchi yetu ya kuwa na maisha ya kuheshimika yaliyo na utu yenye uhuru bila vikwazo kutoka kwenye ukoloni wa ccm na washirika wake wa kukandamiza haki na usawa kwa watakamabadiliko, Ambao wamepata msaada wa moja kwa moja ama usiyo wa moja kwa moja,kwa makusudi ama bila makusudi Maafisa Fulani wa juu wa jeshi la polisi wasiyokuwa waaminifu wameendelea kuwa upande wa ccm bila kutambua kuwa ipo siku ccm itaondoka madarakani na wao wataendelea kuwa na wajibu wakulitumika Taifa.
Wananchi wengi wanapewa rushwa kwaajili ya kufanikisha kupotosha ukweli wa uhitaji wa serikali ya ccm kuondoka madarakani,ndio Wanatuchelewesha, wanatuhuzunisha lakini ninauhakika hakuna jambo baya linaloweza kuishi milele bali jambo OVU huishi kwa muda na kupotea milele, Nenda Kenya,Malawi, Zambia nk, Kama jeshi liliwahi kushindana na Umma likashinda.
Ila Chadema hatupo peke yetu Walimu,Wakulima,Wavuvi,Madaktari,Wafanyakazi, waendesha boda boda,wasukuma mikokoteni,mama lishe,wanafunzi na wataka mabadiliko kote duniani na watu waliyohuru kutoka kila pembe ya Tanzania siku zote watakuwepo upande wa Chadema hawata utelekeza mwanga huu wa Chadema mpaka siku zitakapo kuja ambazo hakutakuwa na wakoloni tena pamoja na wanajeshi wa kununuliwa katika nchi yetu.
Kwa wenetu ambao tutawaacha na wengine ambao hatutawaona tena, Natamani waje kuambiwa kuwa mustakabali wa Tanzania ni mzuri na unatarajiwa kuwa kila Mtanzania atafanikisha kazi takatifu ya kuujenga upya uhuru wetu na utaifa wetu.
Kwakuwa bila utu hakuna uhuru,Bila haki hakuna utu na bila uhuru hakuna watu waliyo huru.
Hakuna ukatili kutendewa sivyo ama mateso yaliyonifanya niombe -kuhurumiwa kwakuwa napendelea kufa kishujaa, Imani ikiwajuu na kujiamini kwangu kukiwa na umuhimu katika kujua mwisho wa nchi yangu.
Historia itazungumza siku moja japokuwa haitakuwa historia ya kuifurahisha CCM na washirika wake kwani huwo utakuwa ndiyo mwisho wake.
Lakini ni ile itakayofundishwa kutoka mikononi mwa ccm na wapambe wake,Chadema itaandika historia yake Mwisho na itakakuwepo Kaskazini,kusini,mashariki na magharibi mwa Tanzania Historia ya utukufu na utu.
Tafadhali msisononeke makamanda wenzangu, najua mnajua nchi yetu inateseka kwakiasi kikubwa na itajua namna ya kuulinda uhuru wake....
Mgombea ujumbe kamati kuu Chadema 2014
-
Mungu ibariki Chadema
Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki Afrika
Henry Kilewo
05.09.2014