Hakuna nchi duniani kila mtu anahutubia taifa, ni Tanzania peke yake

Hopeless comment ever! Haya tuambie na wale wazee wa Machame waliomkataa Mwenyekiti wako wa maisha Mbowe Mugabe siyo wachaga au unafikiri wachaga wote wanakubali usani wa Mbowe?
View attachment 1450635
Acheni kuwatesa wazee kwa kuwafungia vilabu vyao vya mbege
Mnawafungia into submission halafu halafu mnakwenda kuwarikodi

Shame kwa huyo mmasai mkuu wa wilaya
 
Ujio wa teknolojia mpya ya kupashana habari na kuchipuka siasa taka nchini Tanzania kumeibua jambo ambalo lisipotafutiwa dawa linaweza kuja kutuletea majanga nchini. Kuanzia 2015 kumezuka tabia ya watu kujifanya wanahutubia Taifa. Na katika hali ya kushangaza mwaka 2019 mtu mmoja alijifanya anahutubia taifa kwa kutanguliza wimbo wa Taifa!

Akamalizia tena kwa wimbo wa Taifa. Maana yake halisi watu hawa wanafanya "impersonation"! Wanajifanya wao ni wakuu wa nchi! Sheria ya habari ipo na inatamka wazi nani ndiye anaweza kuwahutubia raia wa Jamhuri inayoitwa JMT.

Mtu mwingine yoyote anahitaji kibali. Ndio maana mfano Dar Es Salaam pakawekwa sehemu maalum kwa yeyote mwenye tangazo. Unatakiwa uombe muda na upeleke script yako pale Maelezo ihakikiwe.

Ujio wa teknolojia umerahisisha watu kuhutubia lakini haujabadili sheria! NI vyema sasa kila anayetaka kufanya press conference kupitia tools mbalimbali awekewe utaratibu. Ama sivyo iko siku atajiamkia mtu atangaze nchi imepinduliwa au mkuu wa nchi amekufa!

Si Idara ya Maelezo bado ipo tena kila mkoa? Si TCRA ipo?

Unaweza kudai je mtu akiwa nje ya nchi? Itakuwa hufahamu Internet inafanyaje kazi! Hawa kina YouTube na wenzao wana miiko. Serikali inaweza kuwataarifu kuwa ikitokea mtu anahutubia wasimruhusu mpake wapate clearance TCRA.

Sisi hatutakuwa wa kwanza kufanya hivyo. Mifano mzuri ni China, Morocco, Japan. Kina Google na YouTube hawawezi kufanya mchezo na wao. Watafungiwa kabisa. Na hawa hawajali kelele za haki za binadamu. Kwao ustawi wa nchi zao ni muhimu kuliko Uhuru wa jitu moja kutukana nchi!

Serikali chukueni nafasi yenu katika hili. Haiwezekani raia wahutubiwe na kila mtu! Tena wahutubiwe kujengeana chuki!
Kama Sheria husika ilishafutwa basi haraka rudisheni utaratibu wa kuhakiki hawa "maraisi" feki!

Watakuja sababisha balaa!

Hakuna nchi duniani mtu yoyote anahutubia Taifa! Mmewahi kusikia Kenya, Uganda, Marekani, UK?? Kwa nini Tanzania iwe holela hivi? Kwani YouTube, Google, Twitter na Facebook ziko Tanzania peke yake?

Mchelea mwana kulia hulia mwenyewe!!!!!
Da mkuu yani watu kufanya press zao nayo inakupa tabu,ebu tujikite kwenye mambo ya msingi ,mfano mtu akifanya press akaongea anachotaka na wakati huo wewe umekamata dora unapata shida gani?
Je vipi Laila Odinga aliejiapisha huko kenya mbele ya kandamnasi na huku kinyata akiwa tiyari ni rais mbona aliachwa na sasa yuko wapi? Kwisha.
Kuna vitu ukifanya unampa kiki adui yako bila kujua na kuna vitu ukipuuza una mpunguzia credit adui yako.miaka nenda rudi watu wamekua wakifanya press leo uje uzipige stop ghafla nini unaogopa?
 
Acheni kuwatesa wazee kwa kuwafungia vilabu vyao vya mbege
Mnawafungia into submission halafu halafu mnakwenda kuwarikodi

Shame kwa huyo mmasai mkuu wa wilaya
Endelea kusugua vidole vyako kwenye keyboard!
 
A leader of official opposition has that right. Usiandike vitu ambavyo hauna uelewa navyo. Umetoa mfano wa Kenya wakati haujui kwamba Raila Amolo Odinga siyo tu kwamba ame address the nation lakini pia akisema kesho watu wasiende kazini, basi hawaendi. Ufinyu wako wa maarifa usiuanike. ' Do not air your dirty laundry in public"
Jamaa alijiapisha kabisaa
 
Sisi ni Tanzania, nchi huru yenye mamlaka zake zinazojitegemea.

Sisi siasa yetu ili mpaka tuitwe tz sio lazima tufanane na marekani, China au Japan katika kuendesha mambo yetu.

Kadhalika upinzani wetu wa siasa za nchi pia una taratibu zake za kuendesha mambo yake.

We unaetaka tufanane na mataifa ya nje, si CCM haohao ndo wanapinga mitazamo ya kimagharibi.

Kwanini mnayakubali baadhi na kuyakataa baadhi.
 
Taifa letu bia yetu nchi yetu hata wewe ukitaka kuhutubia hujakatazwa mkuu😶
 
Leo asubuhi nilikuwa nikangalia Tv za kenya zikisema kundi kubwa kabisa la Nzige linakuja Nchini Tanzania kutoka kenya hizi ni habari mbaya sana
downloadfile-3.jpg
Locusts.jpg

Huu sio muda wa kiongozi kujificha
 
ID ya kichagga halafu wanamponda Mbowe ili Mbowe aonekane hakubaliki Kilimanjaro. Si mulete uchagusi wa haki muone..........
Unajua Ccm bado wanafikra za kikomunisti hizo ni propaganda za miaka ya sitini
 
Back
Top Bottom