Hakiki kama umesajiri simu yako sasa

Hakiki kama umesajiri simu yako sasa

Mlendamboga

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2011
Posts
670
Reaction score
347
TCRA imeanza kampeni za kuelimisha wananchi kuhakiki usajili wa simu card zao ili kujiweka salama kutokana na utekelezaji wa sheria ya Epoca ya 2010 inayotaka kila simu ya mkononi iwe imesajiliwa na kuwa na utambulisho wa mmiliki.Ili popote pale ulipo uweze kuhakiki kama umesajiliwa bonyeza kwenye simu yako ya mkononi *106# ok italeta taarifa za usajili wako, kama utabaini kasoro ni muhimu uende kwa wakala aliyekaribu akurekebishie taarifa zako ikiwa ni pamoja na kasoro za Majina.
Vitambulisho vinavyoruhusiwa kwa sasa kutumika kusajili simu ni
1. Kitambulisho cha uraia(NIDA)
2.Kitambulisho cha mpiga kura
3.Leseni ya kuendeshea gari
4.Hati ya kusafiria
5.Kitambulisho cha mkazi Mzanzibar
Kulingana na sheria ya Epoca kosa kubwa ni kusajili simu kwa taarifa za uongo (zisizo za kwako) ambapo adhabu yake ni kifungo cha miezi 12 na faini ya Tshs 3milioni
 
Jombaa unachanganya usajili wa sim card na handset rudia kuandika tena
 
Sim card tumeshazisajili mda mrefu sana. Ila wazo la kusajili simu kama tunavyosajili magari nalo ni wazo zuri sana!, IMEI number ndio namba za usajili wa simu.
 
nina siku ya pili voda wanashindwa kukamilisha usajiri kisa eti macho hayaendani na kitambulisho mara wakala mwingine anasema kitambulisho hakisomi basi full vurugu nimesusa kwa muda
 
Sim card tumeshazisajili mda mrefu sana. Ila wazo la kusajili simu kama tunavyosajili magari nalo ni wazo zuri sana!, EMEI ndio namba za usajili wa simu.
Kikubwa majina yaliyopo yafanane na vitambulisho vyako, vendors ama freelencers wakati fulani walikuwa wanasajiri mtu hata kwa taarifa zisizo zake ndiyo sababu ya kuhakiki kwanza ndipo uende ikiwa kuna kasoro
 
nina siku ya pili voda wanashindwa kukamilisha usajiri kisa eti macho hayaendani na kitambulisho mara wakala mwingine anasema kitambulisho hakisomi basi full vurugu nimesusa kwa muda
Lazima kuna tatizo manake mfumo wa usajili wa voda ni kweli unamtambua mtu kwenye uso wake!!
 
nina siku ya pili voda wanashindwa kukamilisha usajiri kisa eti macho hayaendani na kitambulisho mara wakala mwingine anasema kitambulisho hakisomi basi full vurugu nimesusa kwa muda
mi niliangaika sana na kitambulisho changu cha kupiga kura kusajili voda ikazingua mpaka nikamwomba mtu anisajilie kwa kitambulisho chake ndo naitumia kama yangu!
 
mi niliangaika sana na kitambulisho changu cha kupiga kura kusajili voda ikazingua mpaka nikamwomba mtu anisajilie kwa kitambulisho chake ndo naitumia kama yangu!
do! kazi kwelikweli nafikiri tume ya mawasiliano inapaswa kulitazama upya swala hili hata kwa mwenye jicho moja limekuwa tatizo
 
do! kazi kwelikweli nafikiri tume ya mawasiliano inapaswa kulitazama upya swala hili hata kwa mwenye jicho moja limekuwa tatizo
ni kweli na shida kubwa ipo kwenye line ya voda kuliko line za mitandao mingne
 
Back
Top Bottom