Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,362
- 4,816
1. Amani pasipo haki, Ni wapi umeiona?,
Kwa hadithi sikumbuki, Ajabu'li kuliona,
Walo juu mishikaki, wa chini hakuna dona,
Haki Ikikosekana, Amani I Mashakani
2. Wanahubiri Usawa, wanaiba wakigawa,
Mifumo imepagawa, Dhoofu yataka dawa,
Wamewajaza machawa, waimbe nchi I Sawa,
Haki Ikikosekana, Amani I Mashakani
3. Amani wanayosema, ya wasiojulikana
Imegeuka kiama, kuna hofu kila kona
Nani alie salama, wote tunaulizana
Haki ikikosekana, amani i mashakani
5. Twatakiwa kuongea? Au tubakie kimya?
Ni swali nawatengea, mwapaswa kulimumunya
Maana tukitembea, watuo wanatuminya
Haki ikikosekana, amani i mashakani
6. Wanakuja na mitutu, kuitangaza amani
Unatekewa Kisutu, haupo magerezani
Hauwaambii kitu, wanakana asilani
Haki ikikosekana, Amani I mashakani
7. Wanatupwa mashambani, huku wengine mitoni
Wanatekwa mabasini, wauawa maporini
Wanavamiwa makanisani, I wapi hiyo amani?
Haki ikikosekana, Amani i mashakani
8. Na Mtuambie leo, Kipi mwataka tunene
Mnatunyima upeo, kuwasifu tufanane
Wakoloni mamboleo, yu wapi Beni sanane
Haki ikikosekana, Amani i mashakani.
9. Kuongea yetu haki, yaturuhusu Katiba,
Hatutaki unafiki, maovu kimya kubeba,
Msitupige fataki, maoni yakiwakaba,
Haki ikikosekana, Amani i mashakani.
10. Haki huzaa amani, muimbayo jukwaani,
Katu hazitengamani, vinginevyo maafani,
Haraka Badilikeni, ubinafsi uacheni
Haki Ikikosekana, Amani I Mashakani
11. Utaifa hushamiri, Haki ikisimamiwa,
Nchi hali huwa shwari, chaguzi zenye usawa,
Furaha iso mithiri, hakuna wa kutugawa,
Haki ikikosekana, amani i mashakani,
Kwa hadithi sikumbuki, Ajabu'li kuliona,
Walo juu mishikaki, wa chini hakuna dona,
Haki Ikikosekana, Amani I Mashakani
2. Wanahubiri Usawa, wanaiba wakigawa,
Mifumo imepagawa, Dhoofu yataka dawa,
Wamewajaza machawa, waimbe nchi I Sawa,
Haki Ikikosekana, Amani I Mashakani
3. Amani wanayosema, ya wasiojulikana
Imegeuka kiama, kuna hofu kila kona
Nani alie salama, wote tunaulizana
Haki ikikosekana, amani i mashakani
5. Twatakiwa kuongea? Au tubakie kimya?
Ni swali nawatengea, mwapaswa kulimumunya
Maana tukitembea, watuo wanatuminya
Haki ikikosekana, amani i mashakani
6. Wanakuja na mitutu, kuitangaza amani
Unatekewa Kisutu, haupo magerezani
Hauwaambii kitu, wanakana asilani
Haki ikikosekana, Amani I mashakani
7. Wanatupwa mashambani, huku wengine mitoni
Wanatekwa mabasini, wauawa maporini
Wanavamiwa makanisani, I wapi hiyo amani?
Haki ikikosekana, Amani i mashakani
8. Na Mtuambie leo, Kipi mwataka tunene
Mnatunyima upeo, kuwasifu tufanane
Wakoloni mamboleo, yu wapi Beni sanane
Haki ikikosekana, Amani i mashakani.
9. Kuongea yetu haki, yaturuhusu Katiba,
Hatutaki unafiki, maovu kimya kubeba,
Msitupige fataki, maoni yakiwakaba,
Haki ikikosekana, Amani i mashakani.
10. Haki huzaa amani, muimbayo jukwaani,
Katu hazitengamani, vinginevyo maafani,
Haraka Badilikeni, ubinafsi uacheni
Haki Ikikosekana, Amani I Mashakani
11. Utaifa hushamiri, Haki ikisimamiwa,
Nchi hali huwa shwari, chaguzi zenye usawa,
Furaha iso mithiri, hakuna wa kutugawa,
Haki ikikosekana, amani i mashakani,