Kapepo
JF-Expert Member
- Aug 14, 2015
- 1,063
- 1,188
Kuna binti nilikuwa na mazoea nae ya kawaida tu hapa kazini napofanyia kazi kama marafiki nikimtumia messages anajibu tu vizuri bila shida, sasa tabu imeanzia hapa nilipomtongoza kwa mara ya kwanza pale nilipomuambia nampenda nimemuelewa alinijibu kwa kuuliza "serious " nikamjibu ndio yeye alinijibu hivi "mhhhh" ndio ukawa mwisho wayeye kupokea simu zangu tena wala kujibu messages hajibu tena, namimi nkaamua kumpotezea sikumtokea tena wala kumsumbua kwa simu ila tukionana kazini tunaongea tu kawaida japo sijampanga tena sasa jana nilikuwa nae mida ya usiku hivi nkaomba nimtoe out to chill sehemu tulivu tuyajenge akasema sawa cha kushangaza nimempgia simu leo hii akaniuliza nani "wewe" doh kidume limenishuka nkakata simu nkamuuliza inamaana umefuta namba zangu akawa kimya hakujibu tena nkampigia nkamwambia mimi mtu fulani akajibu sawa ntakutumia sms bdae kuna kazi nafanya kwakweli mimi huwa sipendi sana kutumia nguvu kwenye kumtongoza mwanamke sasa swali je nini nifanye anielewe aache kuringaringa au dogo hajanielewa mchizi ni move mbele na mitikasi mengine.
NB: kuna jamaa yeye alimtongoza akajibiwa hapohapo kwamba hamuhitaji ila mimi ananikaushia naombeni mawazo yenu wataalam wa hizi kazi.
NB: kuna jamaa yeye alimtongoza akajibiwa hapohapo kwamba hamuhitaji ila mimi ananikaushia naombeni mawazo yenu wataalam wa hizi kazi.