Siku moja au mbili.....ukihitaji kuisoma yote waweza nicheki WhatsApp 0621567672Shusha shusha, kwani inatoka Kila baada ya muda gani?
HADITHI: ULIMWENGU WA WATU WABAYAHADITHI: ULIMWENGU WA WATU WABAYA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
MTUNZI : Bux the story teller
WHATSAPP : 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 13
UKURASA ULIOPITA TULIPO ISHIA.............
“Baba Calvin wako saivi amekuwa ni mwanaume haswa lakini kwa bahati mbaya huwezi hata kumsifia tena wala kumkumbatia, huwa kila nikilala nakumbuka usemi wako kwamba haipaswi mwanaume shupavu atoe machozi kwenye uso wake kwani ataonyesha udhaifu mkubwa sana mbele ya wale wanao mtegemea ikiwemo familia yake ambayo inamuangalia yeye kama kioo kwao na hilo nakuahidi kwamba huu uso wangu hautatoa machozi tena juu ya hilo jambo.
Nashukuru sana ulinipeleka kwa mtu sahihi sana kwenye maisha yangu, master Haru, kwangu yule ni zaidi ya mwalimu na kwangu ntamheshimu kama nilivyokuwa nakuheshimu wewe, atakuwa ni familia yangu kwa sasa.
Baba nakuahidi mbele ya uso wa dunia hii hautabaki hata mfupa ulio hai kwa yeyote aliye husika katika hili, kila mtu malipo yake yataendana na alicho kifanya, ila itabidi wafanyiwe kitu ambacho hata wenzao wakiona hawatakaa wakarudia kuichukua haki ya mtu mnyonge tena hapa duniani.
Mwanao naondoka leo na nitarudi tena kuwasalimia siku nikimaliza kazi hii nzito sana ambayo ipo mbele yangu, sayonora chichi to haha”. aliyaongea maneno hayo ya kijapani akimaanisha kwaheri baba na mama kisha akatoka mahali hapo bila kuangalia nyuma, akapanda gari lake na kupotea kwa kasi ya ajabu.
ENDELEA..........................
Alifika hotelini majira ya jioni kidogo na kupitiliza moja kwa moja chumbani kwake, akafika na kuwasha televisheni kabla hata hajaenda kuoga, akakutana uso kwa uso na taarifa moja ya kusisimua sana baada ya kumuona mtu ambae yeye huwa anamchukulia kama baba yake mdogo, hakuwa mwingine ni Juma wa kipindi cha nyuma leo tunamzungumzia Mr Fabian Decco akiwa anatangaza mbele ya uma kwamba mali zote za mzee Jackson Aron zipo chini yake baada ya mzee huyo kupoteza maisha na familia yake akiwa kwake Masaki.
Hiyo haikumshtua sana kwa sababu alifikiria kwamba labda itakuwa ameona ni muda mrefu sasa bila yeye kuonekana mbele yake ndiyo maana anataka kuzisimamia zile mali, kwahiyo Calvin alijua mr Decco alikuwa na maana nzuri tu ya kuendelea kuzilinda mali zao.
“mhhhhhhhh”aliguna baada ya kusikia akitangazwa mbele ya vyombo vya habari kwamba yeye amekufa, alishangaa imekuaje mpaka mzee huyo awe na ujasiri wa kumtangaza kwamba kafariki wakati hawajauona hata mwili wake, ni kama kichwani mwake kuna kitu alianza kuhisi kama hakipo sawa, akakumbuka tangu kwenye msiba wa wazazi wake kulikuwa na watu wenye suti nyeusi na miwani wakionekana kuwa walinzi wa mtu fulani, akifikiria tena alivyokuwa airport kuna watu walikuwa wanamfuatilia mpaka anafika nao Moscow katika nchi ya urusi, alifanikiwa kuwakwepa baada ya kwenda kununua sura ya bandia na kutotambulika mbele yao, hiyo ndiyo ilikuwa pona pona yake mpaka anafika airport kwa ajili ya kwenda kumtafuta mzee Haru ambae alielekezwa kumpata kwa namba maalumu nchini Japan. Akakumbuka vyema mpaka alivyoweza kuitoa ile sura bandia maeneo ya uwani pale airport na kufanikiwa kufika Japan akiwa salama kabisa.
“mbona haya mambo yananichanganya, inaonekana kuna kitu kimejificha hapa, huyu kwangu ni kama baba yangu sina imani kabisa kama anaweza kufanya kitu kibaya kwangu lakini kwa mtirirko wa haya matukio inanipa wasi wasi wa kumwamini moja kwa moja, hapa inanipasa kwanza nijue wale watu walitumwa na nani kunitafuta nadhani hapa nitakuwa nimepata sehemu nzuri sana ya kuanzia” Calvin alikuwa akiongea mwenyewe kisha akaondoka na kwenda kuoga.
IKULU DAR ES SALAAM
Ndani ya Ikulu katika moja ya ofisi kubwa na nyeti zaidi hapa naizungumzia ofisi ya mkurugenzi wa usalama wa Taifa anaonekana mzee Kasisi Chacha mkurya huyu akiwa anamsubiria kijana wake mmoja kutoka nchini Cuba aweze kufika baada ya kumaliza miaka mitano akiwa kwenye mafunzo ya kikomando ili aje kuhakikisha nchi yake inanufaika ipasavyo na uimara wake kuhakikisha amani ya kutosha.
“Ester, victor anafika sangapi airport?” mzee huyu alimwuliza secretary wake huyu ambaye alikuwa ni mzuri na alivutia sana kila ukimtazama.
“nimeongea nae sio muda sana kaniambia baada ya masaa mawili atakuwa ashafika na anakuja moja kwa moja ofisini kuripoti” alijibu kwa heshima Ester.
“fine waweza kwenda”.
Dakika ya saba tangu masaa mawili yakatike tangu mzee huyu alipo muulizia kijana wake ambaye alikuwa akimsubiri kwa hamu kubwa sana.
“bosi”
mzee huyu alijitoa mawazoni na kunyanyua uso wake baada ya kushtuliwa na sauti ya mtu akimuita, alifurahi sana baada ya kumwona huyu bwana mdogo ambae alikuwa anampenda kama mwanae wa kumzaa kwa sababu kamlea mwenyewe baada ya kumuokota siku moja akiwa katika hali mbaya sana mtaani aliko kuwa anapigwa na wenzake wakati wakigombea chakula.
Kiufupi Victor alikuwa mtoto wa mtaani lakini maisha yake yalikuja kubadilika baada ya kusaidiwa siku ile majira ya usiku na mzee huyu akiwa anatokea kwenye majukumu yake ya kazi. Mzee huyu hakubahatika kuoa baada ya mkewe kufa akiwa na ujauzito wa Watoto wawili yaani mapacha wakati anajifungua, tangu siku hiyo mzee Kasisi Marwa hakuwaza kuoa tena wala kuwa na familia ikiwa ni kama kumuenzi marehemu mkewe kwa jinsi alivyo kuwa akimpenda.
Victor aliweza kupelekwa kwenye shule bora sana kisha baadae kwenda jeshini na kuunganishwa moja kwa moja kwenye mafunzo ya kikomando baadae mbayo yalimpeleka mpaka Cuba ili kuweza kuimarika zaidi.
Masikio yake yalisikia jina hilo la bosi likiitwa na moja ya watu ambao alikuwa anawapenda sana, akatabasamu
“mwanangu umerudi huku akimkumbatia Victor”
“ndio baba nimefanya kama ulivyo niagiza”
“safi na najivunia kuwa na mtoto kama wewe”
“asante sana bosi”
“hahahahaa naona ubaba umeuweka pembeni, haya kuna kesi kesi zilikuwa zinaendelea na sikuelewa zimeishaje ila kwa sasa kapumzike nikikuhitaji nitakuita”
“Sawa mkuu” kisha Victor akatoka kwa furaha isiyo elezeka baada ya kumkuta mzee huyo akiwa na afya njema kabisa kwani hakuna binadamu ambae alikuwa ana mheshimu kama mzee huyu na ndiye alikuwa familia yake ya pekee hapa duniani. Wakati anakatiza mapokezi alipokelewa na tabasamu zuri sana la mrembo Ester ambae alikuwa ashaanza kumpenda mwanaume huyu kwa mvuto alio kuwa nao.
“Victor” alishtuka akiwa anaitwa na mrembo huyo
“oooh mrembo unaniita kumbe, japo sijakujua hata kwa jina”
“naitwa Ester”
“sawa Ester nambie”
“samahani sana, nilikuwa naomba namba yako wikiendi kama ukiwa na muda tuonane”
“haikuwa shida kwa victor kuitoa namba ambayo atakuwa anaitumia Tanzania kwani wakati akiwa nje walikuwa wanawasiliana kwa code maalumu tu”
Alitabasamu sana mrembo huyu huku akimkonyeza Victor, mwanaume akatabasamu na kuondoka mahali hapo,
Bibie Ester akatamka “lazima uwe wangu Victor nakupenda”.
UNGANA NAMI MPAKA MWISHO WA KIGONGO HIKI langu jina naitwa FEBIANI THOMASI BABUYA, kurasa zangu napatikana kwa jina la Bux the story teller.
Hotelini kwa Calvin, baada ya kutoka kuoga akaenda kwenye kioo na kujitazama namna mwili wake ulivyo gawanyika vyema ukichochezwa na mazoezi makali ya takribani miaka miwili na miezi kadhaa. Akiwa ndani ya taulo lake akalifuata begi ambalo lilikuwa na nguo, akalifungua kwa password(nywila) na kisha kutoa nguo zote kwenye hilo begi, baada ya hapo akakutana na kioo kigumu ambacho kilimdai nywila ili kulifungua begi hilo upande wa Chini, akalifungua vyema na kutoa ala (kifaa kinacho tumika kuhifadhia upanga hususani katika nchi ya Japan). Calvin aliutoa upanga ulio kuwa una’gaa sana. Akiwa ameushika upanga huo aliokuwa amepewa kama zawadi na mwalimu wake master HARU baada ya kufanya vizuri kwenye mazoezi yake, mawazo yakampeleka mbali sana. Akiwa ndani ya Japan baada ya kumalizana na Dr Sanjey Prakash rasmi sasa aliitwa tena ofisini kwa mzee Haruto Hinata Haru ikiwa ni mara ya pili kuingia ndani ya ofisi hiyo na ni kwa mara ya tatu kumuona mzee huyu tangu siku ya kwanza afike ndani ya ngome hii.
“Calvin Jackson Aron Mavunde, kwa sasa una miaka ishirini na minne na umekua sana, umetimiza miaka miwili ukiwa hapa na kwa sasa umebakisha miezi sita pekee ili niweze kukuruhusu kuondoka hapa. Nakumbuka ulishawahi kuniuliza siku moja kwamba mimi ni nani, nilijuana vipi na baba yako na kwanini ananiamini sana mimi ndiyo maana akakuelekeza uje nikupatie msaada, najua una hamu sana ya kuyajua haya ila miezi sita iliyobaki ndiyo itakayo amua kama nikujibu haya maswali au nisikujibu. Ili uweze kujibiwa kuna kazi ndogo sana unapaswa uifanye ila pia ni kazi ngumu sana kwa mwanadamu wa kawaida kuifanya na usipokuwa makini unaweza ukashindwa, ukishindwa maana yake utakuwa umefeli mtihani, hiyo ni ishara ya kwamba sitakwambia chochote na sitakuruhusu uondoke na inawezekana nisije nikakuruhusu kuondoka tena kwahiyo unapaswa kuwa makini sana na akili yako inapaswa kufanya kazi kwa zaidi ya asilimia tisini kwa hii miezi sita ambayo imebakia, ukiilaza akili yako kidogo tu basi ujue ushafeli mtihani maana hautaweza kuufanya kwa usahihi, unaweza ukawa una haraka sana ya kuhitaji kuujua mtihani huo ila utaambiwa siku unamaliza miezi sita iliyo baki”.
Aliyaeleza kwa usahihi sana maelezo yake mzee huyu kitu ambacho kilimshangaza Calvin kwani hata salamu yake haikuitikiwa kabisa lakini aliamua kutokuwa mwongeaji kwa kuuliza maswali mengi bado maneno ya Akio yalikuwa yanazunguka kichwani mwake “na nikuonye tu siku ukikutana nae chunga sana kinywa chako kwa sababu ukiongea vibaya hata neno moja tu kwake litakugharimu maisha yako yote, yule ni mtu hatari sana”. Calvin akaamua kuitikia kwa heshima
“sawa master nimekuelewa”
“kwa sasa nitapenda zaidi ukiwa unaniita baba nadhani nitafurahi zaidi”
“sawa”
“nenda kajiandae usiku sana uwe macho rasmi unaanza mazoezi namimi mwenyewe”
Yalikuwa ni maongezi mafupi kati ya Calvin na master Haru ambaye hakuwa mtu wa kuongea ongea sana.
Majira ya saa tisa na nusu usiku pembezoni mwa mto Yamato, wanaonekana wanaume wawili na si wengine ni mzee Haru na Calvin wakiwa wote wameshika mapanga lakini mzee Hinata alikuwa ameshika panga feki huku Calvin akiwa amebeba upanga mkali sana unaong’aa gizani.
******************************
Mzee Haru anaanza “kuna mazoezi mawili tu unayopaswa kufundishwa, zoezi la kwanza unapaswa ujue vyema sana namna ya kuutumia upanga na kwa spidi kubwa sana ambayo ni wanadamu wachache sana wanayo, wote tumeshika mapanga ambayo ni halisi kabisa kwahiyo unavyo pigana hesabia kwamba mimi haunijui na upo vitani kwahiyo ukicheza vibaya unakufa” sijajua kwanini mzee huyu aliamua kumtishia Calvin kwa kumwambia kwamba ana upanga halisi wakati haikuwa kweli. Basi mapambano yalianza vyema, Calvin alikuwa ameshaiva sana kwenye mapigano ya kila aina lakini kwenye upanga alikuwa kama kijana mdogo sana. Alishtuka na kuogopa baada ya upanga huo kupitishwa kwenye shingo yake akakaa chini kwa uoga akijua ndo anakufa hivyo, lakini alishangaa kutoiona alama yoyote ile ya damu alivyo mtazama mzee huyu alikuwa akicheka tu, akajua lile panga ni la mbao lakini limetengenezwa kwa namna ambayo ni ngumu sana mtu kulitambua. Basi alinyanyuka huku akiwa anajicheka kwa kufanywa mjinga, na rasmi mazoezi magumu ya kutumia upanga yakawa yameanzia hapo.
Miezi mitatu na nusu baadae majira ya saa tisa kamili usiku juu ya mti mmoja pembezoni mwa mto huo wa Yamato wanaonekana wale wale wanaume wawili wakiwa wanapigana vilivyo kwa kutumia panga ambazo zilikuwa na makali sana, haikuisha hata dakika moja walikuwa na mpambano mzito sana ambao ulipelekea matawi ya miti yote kudondoka chini.
“kuhusu kutumia upanga sasa umeiva vyema kama nilivyokuwa nahitaji na nakuomba tu usikae ukalitumia panga wala kutembea nalo sehemu nyingi unazo enda kwani siku utakayo amua kuutumia upanga wako inawezekana ukawa mtu hatari sana kitu ambacho kitapelekea kuleta taharuki kubwa miongoni mwa watu mbali mbali, kwahiyo hii italeta kukosekana kwa amani miongoni mwa watu wanao kuzunguka. Leo nakupa huu upanga kama zawadi ya pekee, huu ni upanga ambao nimekuwa nikiutumia Kwa zaidi ya miaka thelathini sasa na kuulinda sana kwa miaka yangu yote na kwa nguvu zangu zote, huu upanga ni hazina kubwa sana ndani ya nchi ya Japan kwahiyo unapaswa uutumie vyema ikiwemo na kuulinda kama unavyo yalinda macho yako.
Chamwisho huu upanga utumie pale itakapo kubidi ila tu usiutumie vibaya kwa kuwadhuru watu wasio kuwa na hatia yoyote ile hiyo itapelekea nikuue kwa mikono yangu mwenyewe kitu ambacho hakitakiwi kutokea kwa sababu mimi ndiye ninaye takiwa kukulinda kwa namna yoyote ile. Je Calvin atapewa mtihani gani na unadhani atafanikiwa Kutoka kwenye ngome hii?
Ukurasa huu unafika tamati, tukutane na Kalamu ya professor kwenye kurasa zijazo.
ULIMWENGU WA WATU WABAYA
mimi ni Bux the story teller.....ChaoView attachment 2280884
No, JM nilikuwa nimeitoa kwenye cm hivyo nikabase sana WhatsApp, then hii hadithi ilisha isha so nikawa sina application hiiMmmj hadth naona inatoka mara moja Kwa mwezi
Pole Sana, Kwahiyo unatuahidi Nini wapenzi wasomaji baada ya kurejea tena hewaniNo, JM nilikuwa nimeitoa kwenye cm hivyo nikabase sana WhatsApp, then hii hadithi ilisha isha so nikawa sina application hii
Mkuu nidondoshee bac pdf ya hii kitu nnapesa ya bado apaNo, JM nilikuwa nimeitoa kwenye cm hivyo nikabase sana WhatsApp, then hii hadithi ilisha isha so nikawa sina application hii
Ok 0621567672 ndio namba ya WhatsApp na malipo jina FEBIANI BABUYA......nicheki kwa hiyo nambaMkuu nidondoshee bac pdf ya hii kitu nnapesa ya bado apa
Now nimerudi so lazima mtaisoma haitachelewa kama mwanzo........Pole Sana, Kwahiyo unatuahidi Nini wapenzi wasomaji baada ya kurejea tena hewani
Ubarikiwe Sana Kwa kazi njema, shusha na vipande viwili kusindikizia comment yakoNow nimerudi so lazima mtaisoma haitachelewa kama mwanzo........
YesImefika patamu sana, shukrani mkuu endelea kubaki kwenye kutimiza ahadi Yako hivi si ulisema kimoja Kwa siku eee
Basi nipo hapa kusubiri kipande cha leo
Nimechanganya nadhani mambo mengi kichwaniumerudia