the numb 1
JF-Expert Member
- Dec 15, 2020
- 1,573
- 2,940
STORY: JINI KURUTHUMU
EPISODE 1
Ni jumapili angavu ndani ya mji wa Moshi, mji uliosheni kila aina ya pilikapilika na purukushani. Jua lilikuwa likielekea magharibi na kulipisha giza lichukue nafasi yake. Jioni hiyo, Sudy Chinga kama wengi walivyopenda kuniita kutokana na kazi umachinga nilikuwa narudi masikani kwangu MLANDEGE.
Nikiwa natembea kutokea barabara ya Manyema kuelekea Mlandege, mbele yangu alitangulia msichana mrembo kupindukia. Alikuwa mrembo na mwenye mvuto wa aina yake. Binti huyu licha ya kujaaliwa kchwa kizuri chenye nywele ndefu na laini, alikuwa na uso mpana wa mviringo ulionashkiwa na macho makubwa yenye kurembua muda wote. Midomo yake mizuri, laini ambayo akikupiga busu, katu hutatamani abanduke mdomoni.
Kimwana huyu mwenye uzuri wa kuvunja mizani, alijaliwa kifua kipana kilichobeba maziwa madogo yaliyosimama wima kiasi cha kuwatoa udenda wanaume wakware pindi wamtizamapo. Alikuwa na umbo nzuri, umbo ambalo ni wasichana wachache sana waliopewa upendeleo na maanani kwa kuwa nalo.
Sudy Chinga sikuwa mtu wa wanawake kama walivyo vijana wengine ambao pindi wamuonapo tausi mzuri hawawezi kumuacha apite bure. Hata hivyo nilikuwa nimeoa na Mungu ameijalia ndoa yangu nikapata watoto wawili na mke wangu kwa jina Agness. Tuliheshimiana sana na mke wangu, na hivyo sikupenda kumsaliti mtu anayenipenda na ambaye amejitoa kuishi na mimi katika hali yoyote ile. Nitaanzaje kumsaliti mwanamke anayejiheshimu, mama bora wa familia anayejitambua, mcha-Mungu na asiyeendeshwa na mihemko ya kidunia?. Kwakweli isingewezekana hata kidogo.
Wakati nataka kumpita yule binti, gafla akanisemesha "Jamani kaka mbona wanipita bila hata salamu?" Aliniuliza kwa lafudhi tamu ya kimwambao.
"Aah nisamehe bure dada nilikuwa mbali mno kimawazo" Nilimjibu ningali napunguza mwendo. Kadri alivyonikaribia nikaanza kuhisi harufu ya manukato mazuri ambayo sikuwahi kuyahisi hapo kabla.
"Pole na kazi" Alinieleza baada ya kunifikia.
"Ahsante dada nishapoa!" Nilimjibu.
"Si vibaya kama tukifahamiana. Mimi naitwa Kuruthumu, sijui mwenzangu waitwa Nani?" Alinitupia swali tukiwa tunaendelea kutembea.
"Mimi naitwa Masudi ila ukiniita Sudy chinga kama wengi wanavyopenda kulikatisha jina langu ni vizuri pia"
"oooh Wow! jina lako zuri sana, je pengine una mchumba, mke au hata rafiki wa kike?" Alinihoji.
"Ndio, nina mke na watoto wawili"Nilijieleza bila kuficha chochote.
"Hongera sana kwani kwa umri wako si rahisi mtu kugundua kama umeoa. Ila nilikuwa na ombi? " alinieleza.
"Nieleze tu usijali" Nilimjibu.
"Ningefurahi sana kama tutakuwa marafiki, je hilo nalo unalichukuliaje?"
"Sawa, kuhusu hilo ondoa shaka dada yangu" Nilimjibu.
"Wow! Ahsate sana, si vibaya tukabadilishana namba za simu." alinieleza kisha tukabadilishana namba za simu na kuagana.
Kabla sijafika nyumbani kwangu, uliingia ujumbe wa maandishi aliotuma Kuruthumu kwenye simu yangu.
"Nakupenda sana Masudi ijapokuwa mwenzangu tayari umeoa ila chonde, naomba niwe hata mkeo wa pili. Nakuahidi hutojutia upendo wangu endapo ukinikubalia. nitakufanya uwe mtu katika watu, hutokuwa na sababu ya kuungua juani. Please Masudi Open your Heart"
Sikuijibu ile SMS mpaka ulipoingia ujumbe mwingine tena ulionishangaza sana.
"Endapo utajaribu kunikataa, nitamuua mkeo na wanao kwa mkono wako. by kuruthumu malikia wa bahari ya Hindi" Niliusoma ujumbe huo huku nikiwa nimeyatumbua macho yangu juu ya kiyoo cha simu yangu. Nikamjibu nimekubali kusudi familia yangu isije kupatwa na baya lolote. Kwa mara ya kwanza nikatia password kwenye simu yangu ili Kuruthumu akituma Jumbe zake mke wangu asizione.
Nilifika nyumbani saa tatu usiku tofauti na ilivyo kawaida yangu. Nilikuwa sina raha kabisa, nikakosa hata hamu ya kula kitendo ambacho kilizua hisia mbaya kichwani kwa mke wangu.
Mke wangu alipogundua hali hiyo, alisubiri mpaka watoto walipolala. Kisha tukabaki mimi na yeye sebuleni.
“Unawaza nini mpenzi wangu?” Mke wangu aliuliza
“Nothing. Siwazi chochote zaidi yako na wanangu”.
“Sasa mbona huna raha, unaonekana una mawazo hata chakula ni mpaka ubembelezwe?usinifiche mkeo, maana leo upo tofauti na nilivyokuzoea.”
Kufuatia swali hilo nikabaki kimia kidogo bila kujibu chochote.
“Ni kitu gani kinakusumbua Sudy mume wangu hebu niambie. Au kama kuna kitu nimekukosea niambie nijirekebishe maana tangu tumeanza mapenzi yetu sijawahi kukuona ukiwa katika hali hii. ” Alinieleza mke wangu.
Mke wangu akashindwa kujizuia na kuanza kulia kwa kwiwi. Nikamvutia kifuani kwangu kisha nikambusu na kumwambia.
“Usihofu kitu baby, hakuna kitu chochote kile kinachonisumbua, ila uchovu wa kazi ndio umenipelekea kuwa hivi. Yaani sijisikii hata kula lakini usijali nitakuwa sawa mamaa” Nikamueleza huku nikizichezea nywele zake laini. Nafsini niliumia sana kumficha mke wangu ila ilinilazimu kufanya hivyo kwani sikujua kwamba endapo ningemueleza ukweli nini kingetokea kati yangu na Kuruthumu.
“Pamoja na hayo dear, najua lazima kuna kitu kinachokusumbua akili na hutaki kuniambia ” Agness mke wangu alizidi kunidodosa.
“My dear Agi, wewe ndio maisha yangu, wewe ndiye mfariji wangu, wewe ndio kila kitu maishani mwangu sasa kwanini nikufiche kitu?au kama sitakuambia wewe nimwambie nani mwingine tena?”
Nilijitahidi kumtoa mke wangu wasiwasi, taratibu akaanza kurudi katika hali yake ya kawaida na ucheshi mkubwa mno. akanipeleka maji ya kuoga bafuni. Nikiwa humo bafuni, Kwenye simu yangu niliyoiacha sebuleni kuliingia ujumbe.
Mke wangu akachukua simu ili ajibu jumbe ile kwamba naoga。Kwa mara nyingine akajikuta akiwa na wasiwasi juu yangu baada ya kukuta password kwenye simu yangu, jambo ambalo sikuwahi kulifanya tokea tumeanza uhusiano wetu.
ITAENDELEA....
EPISODE 1
Ni jumapili angavu ndani ya mji wa Moshi, mji uliosheni kila aina ya pilikapilika na purukushani. Jua lilikuwa likielekea magharibi na kulipisha giza lichukue nafasi yake. Jioni hiyo, Sudy Chinga kama wengi walivyopenda kuniita kutokana na kazi umachinga nilikuwa narudi masikani kwangu MLANDEGE.
Nikiwa natembea kutokea barabara ya Manyema kuelekea Mlandege, mbele yangu alitangulia msichana mrembo kupindukia. Alikuwa mrembo na mwenye mvuto wa aina yake. Binti huyu licha ya kujaaliwa kchwa kizuri chenye nywele ndefu na laini, alikuwa na uso mpana wa mviringo ulionashkiwa na macho makubwa yenye kurembua muda wote. Midomo yake mizuri, laini ambayo akikupiga busu, katu hutatamani abanduke mdomoni.
Kimwana huyu mwenye uzuri wa kuvunja mizani, alijaliwa kifua kipana kilichobeba maziwa madogo yaliyosimama wima kiasi cha kuwatoa udenda wanaume wakware pindi wamtizamapo. Alikuwa na umbo nzuri, umbo ambalo ni wasichana wachache sana waliopewa upendeleo na maanani kwa kuwa nalo.
Sudy Chinga sikuwa mtu wa wanawake kama walivyo vijana wengine ambao pindi wamuonapo tausi mzuri hawawezi kumuacha apite bure. Hata hivyo nilikuwa nimeoa na Mungu ameijalia ndoa yangu nikapata watoto wawili na mke wangu kwa jina Agness. Tuliheshimiana sana na mke wangu, na hivyo sikupenda kumsaliti mtu anayenipenda na ambaye amejitoa kuishi na mimi katika hali yoyote ile. Nitaanzaje kumsaliti mwanamke anayejiheshimu, mama bora wa familia anayejitambua, mcha-Mungu na asiyeendeshwa na mihemko ya kidunia?. Kwakweli isingewezekana hata kidogo.
Wakati nataka kumpita yule binti, gafla akanisemesha "Jamani kaka mbona wanipita bila hata salamu?" Aliniuliza kwa lafudhi tamu ya kimwambao.
"Aah nisamehe bure dada nilikuwa mbali mno kimawazo" Nilimjibu ningali napunguza mwendo. Kadri alivyonikaribia nikaanza kuhisi harufu ya manukato mazuri ambayo sikuwahi kuyahisi hapo kabla.
"Pole na kazi" Alinieleza baada ya kunifikia.
"Ahsante dada nishapoa!" Nilimjibu.
"Si vibaya kama tukifahamiana. Mimi naitwa Kuruthumu, sijui mwenzangu waitwa Nani?" Alinitupia swali tukiwa tunaendelea kutembea.
"Mimi naitwa Masudi ila ukiniita Sudy chinga kama wengi wanavyopenda kulikatisha jina langu ni vizuri pia"
"oooh Wow! jina lako zuri sana, je pengine una mchumba, mke au hata rafiki wa kike?" Alinihoji.
"Ndio, nina mke na watoto wawili"Nilijieleza bila kuficha chochote.
"Hongera sana kwani kwa umri wako si rahisi mtu kugundua kama umeoa. Ila nilikuwa na ombi? " alinieleza.
"Nieleze tu usijali" Nilimjibu.
"Ningefurahi sana kama tutakuwa marafiki, je hilo nalo unalichukuliaje?"
"Sawa, kuhusu hilo ondoa shaka dada yangu" Nilimjibu.
"Wow! Ahsate sana, si vibaya tukabadilishana namba za simu." alinieleza kisha tukabadilishana namba za simu na kuagana.
Kabla sijafika nyumbani kwangu, uliingia ujumbe wa maandishi aliotuma Kuruthumu kwenye simu yangu.
"Nakupenda sana Masudi ijapokuwa mwenzangu tayari umeoa ila chonde, naomba niwe hata mkeo wa pili. Nakuahidi hutojutia upendo wangu endapo ukinikubalia. nitakufanya uwe mtu katika watu, hutokuwa na sababu ya kuungua juani. Please Masudi Open your Heart"
Sikuijibu ile SMS mpaka ulipoingia ujumbe mwingine tena ulionishangaza sana.
"Endapo utajaribu kunikataa, nitamuua mkeo na wanao kwa mkono wako. by kuruthumu malikia wa bahari ya Hindi" Niliusoma ujumbe huo huku nikiwa nimeyatumbua macho yangu juu ya kiyoo cha simu yangu. Nikamjibu nimekubali kusudi familia yangu isije kupatwa na baya lolote. Kwa mara ya kwanza nikatia password kwenye simu yangu ili Kuruthumu akituma Jumbe zake mke wangu asizione.
Nilifika nyumbani saa tatu usiku tofauti na ilivyo kawaida yangu. Nilikuwa sina raha kabisa, nikakosa hata hamu ya kula kitendo ambacho kilizua hisia mbaya kichwani kwa mke wangu.
Mke wangu alipogundua hali hiyo, alisubiri mpaka watoto walipolala. Kisha tukabaki mimi na yeye sebuleni.
“Unawaza nini mpenzi wangu?” Mke wangu aliuliza
“Nothing. Siwazi chochote zaidi yako na wanangu”.
“Sasa mbona huna raha, unaonekana una mawazo hata chakula ni mpaka ubembelezwe?usinifiche mkeo, maana leo upo tofauti na nilivyokuzoea.”
Kufuatia swali hilo nikabaki kimia kidogo bila kujibu chochote.
“Ni kitu gani kinakusumbua Sudy mume wangu hebu niambie. Au kama kuna kitu nimekukosea niambie nijirekebishe maana tangu tumeanza mapenzi yetu sijawahi kukuona ukiwa katika hali hii. ” Alinieleza mke wangu.
Mke wangu akashindwa kujizuia na kuanza kulia kwa kwiwi. Nikamvutia kifuani kwangu kisha nikambusu na kumwambia.
“Usihofu kitu baby, hakuna kitu chochote kile kinachonisumbua, ila uchovu wa kazi ndio umenipelekea kuwa hivi. Yaani sijisikii hata kula lakini usijali nitakuwa sawa mamaa” Nikamueleza huku nikizichezea nywele zake laini. Nafsini niliumia sana kumficha mke wangu ila ilinilazimu kufanya hivyo kwani sikujua kwamba endapo ningemueleza ukweli nini kingetokea kati yangu na Kuruthumu.
“Pamoja na hayo dear, najua lazima kuna kitu kinachokusumbua akili na hutaki kuniambia ” Agness mke wangu alizidi kunidodosa.
“My dear Agi, wewe ndio maisha yangu, wewe ndiye mfariji wangu, wewe ndio kila kitu maishani mwangu sasa kwanini nikufiche kitu?au kama sitakuambia wewe nimwambie nani mwingine tena?”
Nilijitahidi kumtoa mke wangu wasiwasi, taratibu akaanza kurudi katika hali yake ya kawaida na ucheshi mkubwa mno. akanipeleka maji ya kuoga bafuni. Nikiwa humo bafuni, Kwenye simu yangu niliyoiacha sebuleni kuliingia ujumbe.
Mke wangu akachukua simu ili ajibu jumbe ile kwamba naoga。Kwa mara nyingine akajikuta akiwa na wasiwasi juu yangu baada ya kukuta password kwenye simu yangu, jambo ambalo sikuwahi kulifanya tokea tumeanza uhusiano wetu.
ITAENDELEA....