Hadaa Mpya kwa Watumishi wa Umma Kuelekea Uchaguzi Mkuu

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,802
71,229
Kweli homa ya uchaguzi mkuu ni mkali kuliko malaria au tishio kuliko huu ugonjwa wa sasa.

Serikali wakati huu wa janga la corona huku ikipita kuomba misaada kutoka kwa kina Rostam Aziz lakini imekumbuka kuwa uchaguzi waja na kura za watumishi ambao kwa miaka minne haijapata kuwaongeza mishahara wala annual increments zilizopo kisheria kamwe haiwezi kuzipata.

Hivyo imekuja na mkakati wa kuwapoza kwa kuwaambia yaweza kuwapa mikopo ya muda mrefu pesa za kununua magari au pikipiki.

Hivi watumishi wanahitaji magari na pikipiki au kuboreshewa maisha yao kwa kipato? Mbona serikali hii ya awamu ya tano inahusudu sana VITU kuliko maendeleo ya watu na maisha bora?

Hadaa hii kwa kweli ni ya kushangaza maana hata kupambana na gonjwa hili la sasa serikali inategemea kuchangiwa wakati wao wanajitapa kutaka kukopesha watumishi eti magari!

Je, hii sio hadaa ya kutaka kupata huruma ya kura za watumishi walio kasirishwa na kuonewa, kupuuzwa na kukandamizwa?

Watumishi mnasemaje, jee mko tayari kupokea hadaa hii kwa kuuza utu wenu na kutoyaona mapungufu yote ya awamu hii na kuipa support katika mitindo yake ya "bao la mkono"?

IMG-20200408-WA0026.jpeg
IMG-20200408-WA0027.jpeg

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivyo imekuja na mkakati wa kuwapoza kwa kuwaambia yaweza kuwapa mikopo ya muda mrefu pesa za kunu
Kwani ukichukua.mkopo ni lazima uipigie kura ccm?
Waacheni watumishi jamani,kila jambo analofanya mwajiri mnachukulia.kisiasa
Wapiga kura wote ni milioni 15,watumishi hawazidi hata laki saba,ni upuuzi tu kudhani kwamba kura za watumishi wa serikali zinatosha kuibakisha ccm madarakani
 
Kwani ukichukua.mkopo ni lazima uipigie kura ccm?
Waacheni watumishi jamani,kila jambo analofanya mwajiri mnachukulia.kisiasa
Wapiga kura wote ni milioni 15,watumishi hawazidi hata laki saba,ni upuuzi tu kudhani kwamba kura za watumishi wa serikali zinatosha kuibakisha ccm madarakani
Nyuma ya hao laki 7 kuna wangapi , na kwanini huu wema wenu uje karibu na uchaguzi ?
 
nina mashaka na hizi habari........kama sikosei zilitoka habari zifananazo na hizi siku si nyingi sana na zikakanushwa na mamlaka husika!
 
Nyuma ya hao laki 7 kuna wangapi , na kwanini huu wema wenu uje karibu na uchaguzi ?
Swali zuri sana hao laki 7 wana wangapi wanategemewa?mtumishi 1 ana watu kibao wanamtegemea kama hao watu hawapati kinachostahili unategemea nini?mtu anaropoka tu bila kujua watumishi ndo kila kitu hapa nchini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom