Nadhani kuna haja ya watu kueleweshwa tofauti kati ya kikundi cha gwaride(Guard) na kikosi.
Kikosi kwa lugha rahisi ni kituo kamili cha kijeshi mfano labda 502 KJ, hiyo KJ ni kifupisho cha neno "kikosi cha jeshi"
Kikosi cha jeshi ni kituo kamili chenye uongozi wake na mkuu wake ndo Commandant(Commanding Officer) wengi hufupisha kwa kuita CO, then ana wasaidizi wake na askari wengine kibao.
Jumla ya vikosi katika katika kanda (mikoa kadhaa) tunaita brigedi mfano brigedi ya kusini, hapa mkuu wa brigedi ndo kiongozi mkuu.
Otherwise niseme nami kile kikundi cha gwaride la kimyakimya(silent guard) kimefanya vizuri sanaaa
Hongera zao